FAHAMU MATIBABU NA CHANZO CHA TATIZO LA MAUMIVU MAKALI YA NYAYO NA KISIGINO (PLANTAR FASCIITIS/POLICEMAN HEELS)


Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul ni matumaini yangu unaendelea vyema mpendwa msomaji wetu,pole kwa majukumu ya wiki nzima napenda kukukaribisha kwa mara nyingine tena katika ukurasa wangu huu upate kujifunza juu ya matibabu ya tatizo au ugonjwa wa maumivu ya nyayo na kisigino ambapo tatizo hili hujulikana kwa lugha ya kitaalam kama PLANTAR FASCIITIS/POLICEMAN HEELS.

Tatizo hili la maumivu makali ya nyayo na kisigino(Plantar fasciitis /policeman heels)ni moja ya sababu/chanzo kilichozoeleka juu ya tatizo la maumivu ya kisigino hivyo tatizo hili au ugonjwa huu tunaweza kusema kwa maana moja ni maambukizi yanayojumuisha kuvimba kwa bendi nene ya tishu ambayo hupatikana katika nyayo zetu miguuni ambayo inaunganisha mfupa wa kisigino na vidole vya miguu (Plantar fascias).

Kadhalika tatizo hili la maumivu makali ya nyayo na kisigino(Plantar fasciitis) husababisha maumivu makali ambayo mara nyingi hutokea asubuhi pale muhusika anapoamka na anapoweka miguu yake chini na kuanza kupiga hatua zake za kwanza asubuhi maumivu huwa makali sana ambayo hupungua kadri anavyopiga hatua lakini pia hali ya maumivu huweza kurudi baada ya muda mrefu wa kusimama au unaposimama baada ya kukaa.

Tatizo hili  la maumivu makali ya nyayo na kisigino (Plantar fasciitis)huweza kuwapata watu wa rika zote ingawa hutokea zaidi kwa watu wanaofanya mazoezi ya kukimbia sana kadhalika watu ambao ni wenye uzito mkubwa sana na wale ambao huvaa viatu visivyo na visigino na wale wanaovaa viatu vyenye visigino virefu mara kwa mara.


CHANZO/VISABABISHI


Inakadiriwa kuwa wanawake na wanaume walio katika umri wa miaka 40_70 wapo katika hatari kubwa ya kupata tatizo hili la maumivu makali ya nyayo na kisigino (plantar fasciitis), kadhalika wanawake wameonekana ndio wahanga wa kubwa wa tatizo hili la maumivu makali ya nyayo na kisigino ( plantar fasciitis)kuliko wanaume pia wanawake wajawazito nao wamekua wakisumbuliwa na tatizo hili vipindi vya mwisho vya ujauzito.

Lakini pia Mpendwa msomaji ili uweze kuelewa chanzo cha tatizo hili napenda kukujuza kua katika miguu yetu kuna tishu nyembamba ndefu  inayopatikana katika maunganio ya nyayo na kisigino ambayo iko moja kwa moja chini ya miguu yetu,tishu hii inasaidia upinde wa mguu wako na kutusaidia hasa wakati tunapotembea au kusimama.

Lakini Iwapo kutatokea mvutano na msukumo mkubwa juu ya mishipa, mvutano au msukumo huo mkubwa huharibu tishu hiyo na kupelekea kupatikana maambukizi ambayo ndio chanzo cha kupata maumivu makali ya nyayo na kisigino (plantar fasciitis).

DALILI


Mpendwa msomaji dalili zinazoweza kukujulisha kua una ugonjwa huu wa plantar fasciitis ni kupata maumivu makali chini ya miguu yako hasa eneo la kisigino.

Mgonjwa anapoamka na anapoweka miguu yake chini na kuanza kupiga hatua zake za kwanza asubuhi hupata maumivu makali sana ambayo hupungua kadri anavyopiga hatua lakini pia hali ya maumivu huweza kurudi baada ya muda mrefu wa kusimama au unaposimama baada ya kukaa.

VIPIMO NA UCHUNGUZI

Mpendwa msomaji uchunguzi wa tatizo hili kawaida  hufanywa na daktari ama mtaalamu aliyebobea katika magonjwa ya mifupa hivyo baada ya kumuelezea daktari dalili zinazokusumbua daktari wako atachunguza mguu wako kwa umakini ambapo atalenga kutafuta ishara hizi:

Upinde wa juu au muelekeo wa juu ya kisigino chako

Eneo unalohisi maumivu chini ya mguu wako, iwapo ni mbele tu ya mfupa wa kisigino au la

Kuchunguza kujua maumivu makali unayapata wakati gani hasa hivyo daktari atajaribu kukupa mazoezi ili kuweza kubaini tatizo

Kadhalika daktari wako anaweza kukuagiza vipimo vifuatavyo 

X_Ray na MRI_SCAN 

Ili kujiridhisha kua hakuna chochote kingine kinachosababisha maumivu ya kisigino, kama vile kupasuka kwa mfupa(bone fractured)

MATIBABU

Mpendwa msomaji kuna aina kadhaa za matibabu ambazo daktari wako anaweza kukupatia ili kupunguza maumivu na kupunguza ukubwa wa tatizo. 

Kadhalika Daktari Anaweza kupendekeza kutumia matibabu kadhaa kwa wakati mmoja kama ifuatavyo;

MATIBABU YA DAWA 

Daktari huamua kukupatia dawa za kumeza aina ya Nonsteroidal  anti inflammatory drugs (NSAIDs) kama vile ibuprofen,naproxen sodium nk kwaajili ya kupambana na maambukizi pamoja na kusaidia kupunguza maumivu katika kisigino.

MATIBABU YA SINDANO

Daktari huamua kukupatia matibabu ya sindano zenye steroids iwapo maumivu ni makali na matibabu ya  dawa nilizoelezea hapo juu kushindwa kupunguza maumivu,

Hivyo daktari wako atakuchoma sindano ya steroid sehemu ambayo unahisi maumivu makali zaidi katika kisigino chako hii itakusaidia kupunguza maumivu kwenye kisigino kwa muda angalau wa mwezi mmoja au zaidi.

MATIBABU YA TIBA MWILI(PHYSICAL THERAPY)

 Ndugu mpendwa msomaji iwapo matibabu ya dawa,sindano na hata mazoezi kushindwa kusaidia kuondoa tatizo hili daktari atakupendekezea uende kwa mtaalamu wa viungo (physical therapist),Ambapo Utajifunza mazoezi ya kunyoosha na kuimarisha tishu zilizopo miguuni na misuli ya miguu ya chini. Kadhalika Mtaalam wako wa mwili anaweza pia kukupatia huduma zingine kama kukufanyia massage,kukushauri kutumia night splint,foot pads, na hata ultrasonography kusaidia kupona kwa muda mrefu.

Lakini pia Iwapo hauonyeshi maendeleo baada ya miezi kadhaa, daktari wako anaweza kupendekeza utaratibu mwingine kama vile Shockwave therapy, tenex na hata kushauri ufanyiwe upasuaji.

OPARESHENI

Daktari hufikia maamuzi ya kukufanyia upasuaji mara baada ya njia zote zilizotumika kushindwa kukusaidia yani kufanyiwa upasuaji kwa tatizo hili kawaida ni njia ya mwisho ikiwa una maumivu makali au jeraha la muda mrefu ambalo matibabu mengine hayakusaidia.

NAMNA UNAVYOWEZA KUJITIBIA NA KUPUNGUZA UKUBWA WA TATIZO LA MAUMIVU katika nyayo na visigino UKIWA NYUMBANI

Mpendwa msomaji wetu kuna njia nyingi anazoweza kuzitumia mgonjwa kujitibia au kupunguza ukubwa wa tatizo hili akiwa nyumbani lakini pia licha ya kuwa baadhi ya njia nimeziorodhesha hapa chini zimewasaidia wengi ila unahitajika kupata ushauri na vipimo kutoka kwa mtaalamu wa afya ili kujiridhisha juu ya tatizo hili kabla hujatumia njia yoyote ili akupatie ushauri ni njia gani inaweza ikakufaa bila ya kukuathiri iwapo utakua una matatizo mengine tofauti na tatizo hili.
Baadhi ya njia zinazotumika kupambana na tatizo hili ni;

1.PUNGUZA UZITO

Mpendwa msomaji napenda ufahamu kwamba Mtu kua na uzito mkubwa ni miongoni mwa vyanzo vya kupata tatizo hili kwani kua na uzito mkubwa huweka shinikizo au uzito zaidi kwenye tishu zilizopo miguuni. Hivyo Ikiwa una uzito mkubwa jitahidi upunguze japo kidogo ili kusaidia kupunguza shinikizo la uzito mguuni.
 Unaweza kuwasiliana na daktari wako ili akupatie mpango au ratiba ya milo inayozingatia lishe bora na mazoezi ya kawaida yatakayokusaidia kupambana na tatizo hili.

2.PUMZIKA

Mpendwa msomaji wakati mwingine maumivu ya nyayo na visigino ni ishara kwamba miguu yako inahitaji kupumzika tu, haswa ikiwa unafanya shughuli ngumu mara kwa mara kama vile kusimama kwa muda mrefu, kukimbia,kuvaa viatu virefu mara kwa mara hivyo basi unashauriwa kujitahidi Kujipatia mapumziko ya miguu yako kwa siku chache ili kusaidia kupunguza uvimbe na kuiruhusu tishu na misuli ya miguu kupumzika.

3.VAA VIATU VYENYE KISIGINO KIFUPI

Imeonekana kua Watu wanaovaa Viatu visivyo na visigino na viatu vyenye visigino virefu husumbuliwa sana na hili tatizo hivyo tunashauriwa kuvaa viatu vyenye visigino vifupi ambavyo vinatoa msaada mzuri kwa misuli ya miguu wakati tunapotembea au kusimama.

4.VAA PEDI ZA MIGUU

Mpendwa msomaji unaweza kununua/kuvaa pedi za miguu ambazo husaidia kupunguza maumivu na maambukizi  miguuni.
Pedi hizi zinapatikana katika baadhi ya maduka ya dawa
Hata ofisini kwangu unaweza kuzipata tuwasiliane kwa namba zifuatazo ujipatie pedi hizo iwapo utahitaji
+255746465095/+255657041420

5.INYOOSHE/KUKANDA NYAYO

Mpendwa msomaji wakati mwingine ili kutuliza au kupunguza maumivu yanayosababishwa na kuvimba kwa tishu, tunatakiwa kunyoosha au kujikanda na mafuta ya mzaituni kwa upole au taratibu.
Mara baada ya kumaliza shughuli zako usiku kabla hujalala paka mafuta katika nyayo zako na umuombe mkeo/rafiki/mumeo/ndugu akukande kwa muda wa dakika 15 kuanzia kwenye vidole,nyayoni akimalizia taratibu katika visigino hii husaidia hasa kuondoa maumivu na kuponya maradhi mengi na hata kuondoa uchovu wa mwili.

MATIBABU YA TATIZO LA MAUMIVU MAKALI YA NYAYO NA KISIGINO (PLANTAR FASCIITIS/POLICEMAN HEELS)  CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo hili la kupata maumivu makali chini ya nyayo na kisigino (plantar fasciitis/policeman heels) na umeshafanya matibabu kadhaa ila bado hujapata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam 
Tutakufanyia uchunguzi  kwa kina pia tutakupatia dawa stahiki zenye uwezo wa kukuponya kabisa.

Pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tunatoa huduma ya matibabu ya ushauri na dawa za kuondoa magonjwa mbalimbali katika mwili kama vile matatizo ya hedhi mbovu,matatizo ya uzazi,kutoka harufu mbaya ukeni na kadhalika karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nina imani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )


0 comments:

Copyright © 2017 Green health consultation centre