FAHAMU MATIBABU YA UGONJWA WA TUMBO KUJAA MAJI (EXCESS ABDOMINAL FLUIDS/ASCITES)

UGONJWA WA TUMBO KUJAA MAJI EXCESS ABDOMINAL FLUIDS/ASCITES


Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, mpendwa msomaji wetu tuna dhana njema juu yako tunaimani unaendelea vyema,tunakuombea afya njema zaidi wewe na familia yako
MWENYEZIMUNGU MTUKUFU AZIDI KUKUJAALIENI AFYA, HIFADHI NA USALAMA
Ameen!

Katika mada yetu ya leo ninakumbushia ugonjwa ambao nimekwishauzungumzia miaka ya nyuma ugonjwa ambao husababisha maji kujaa ndani ya tumbo na mara nyingine husababisha mgonjwa apate matatizo katika kupumua.
 Ni ugonjwa ambao baadaye huweza kusababisha maambukizi ya bakteria katika tumbo – spontaneous bacterial peritonitis (SBP) na kushusha kinga za mwili katika eneo hilo lililojaa maji. Ugonjwa huu huitwa excess abnominal fluids au Ascites


JE, TATIZO LA TUMBO KUJAA MAJI (EXCESS ABDOMINAL FLUIDS/ASCITES) NI UGONJWA GANI?


Ascites/excess abnominal fluids ni ugonjwa wa kujaa maji kupitiliza ndani ya tumbo. Maji haya hujaa ndani ya nafasi iliyopo katikati ya tabaka mbili za utando laini ambazo kwa pamoja hujenga peritoneum(mfuko laini)ambao hushikilia viungo vya ndani ya tumbo.
Kawaida tumboni kunakuwepo maji kiasi ndani ya nafasi hiyo (hadi mililita 20 kwa mwanamke na pungufu ya hapo kwa mwanamme). Kitaalamu maji hayo yanapozidi mililita 25, mgonjwa hutajwa kuwa ana ascites yani tumbo limejaa maji kupitiliza.
Kadhalika tatizo hili limegawanyika katika aina mbili.


AINA za TATIZO lA TUMBO kujaa maji(excess abnominal fluids/ascites

Tatizo hili limegawanyika katika aina kuu 2, yani transudative na exudative.
Mgawanyo huu hutegemea kiwango cha protini kinachoonekana ndani ya maji hayo. Namna bora zaidi iliyotumika ni kutazama kiasi cha albumin kilichopo ndani ya maji (ascitic fluid) kikilinganishwa na kiasi kilichopo ndani ya albumin iliyopatikana ndani ya damu. Hii huitwa Serum Ascites Albumin Gradient au SAAG. Tatizo la tumbo kujaa maji lilotokana na sababu ya pressure kwenye mishipa mikubwa ya damu ya ini (portal hypertension) huwa juu ya  wastani wa 1.1, na ukilinganisha sababu nyingine zilizosababisha tatizo hili  huwa chini ya wastani wa 1.1

CHANZO CHA TATIZO


Kuna vyanzo vingi vya kujaa maji tumboni, ikiwa ni pamoja na kusababishwa na uwepo wa ugonjwa wa kifua kikuu(tuberculosis) magonjwa ya figo(kidney diseases) maambukizi katika kongosho(pancreatitis) na udhaifu wa utendaji kazi wa tezi ya thyroid.
Lakini pia vyanzo vikuu vilivyo bainishwa kwa tatizo la maji kujaa ndani ya tumbo ni magonjwa ya ini yaliyo katika hali mbaya (cirrhosis).
 Pamoja na kwamba haijajulikana kwa hakika ni vipi tatizo la tumbo kujaa maji linatokea, nadharia nyingi zinaamini kuwa kuongezeka kwa msukumo katika mishipa ya kupeleka damu kwenye ini (portal hypertension) kuna mchango mkubwa zaidi kuliko sababu nyinginezo ambazo zimeorodheshwa.

Kanuni ya msingi inafanana na ile inayosababisha kuvimba (EODEMA) kwenye maeneo mengine ya mwili ambapo kunakuwa na utofauti wa msukumo kwenye sehemu mbili zinazopakana, sehemu moja ya ndani ikiwa ya msukumo mkubwa na ya nje, kwa hapa ni uwazi wa tumbo, ikiwa na msukumo mdogo.
Kadhalika Kuongezeka kwa pressure kwenye mishipa inayolilisha ini na kupungua kwa albumin (protini iliyopo ndani ya damu) vinaweza kuwa visababishi vya tofauti hizi za msukumo na kusababisha maji kujaa ndani ya tumbo kupitiliza (Ascites)

Pia visababishi vingine vinavyochangia tatizo la maji kujaa tumboni ni chumvi na kuzuiwa kwa maji.
Kadhalika damu iliyopo ndani ya mzunguko inaweza kuchukuliwa kuwa ni ndogo ikitazamwa na figo kwa sababu tatizo hili  linapoanza, hupunguza ujazo wa damu kwenye mzunguko. Hii huzifanya figo kuhifadhi chumvi na maji zaidi kufidia upungufu huo wa damu.

Matatizo mengine yanayohusiana na utofauti wa pressure ya pande mbili ni congestive heart failure na uharibifu wa figo ulio mkubwa ambao huzuia maji ndani ya mwili.

Kadhalika ni Mara chache sana mwongezeko wa pressure kwenye mishipa ya damu ya ini hutokana na kuzibwa kwa ndani au nje kwa mishipa hiyo, hivyo kusababisha portal hypertension bila uharibifu wa ini (cirrhosis). Mifano ya hali hii ni kama uvimbe kugandamiza juu ya mishipa hiyo kutoka kwenye uwazi wa tumbo au damu iliyoganda kuziba ndani ya mishipa hiyo na kusababisha mwongezeko wa pressure (mfano, Budd-Chiari syndrome.)

Pia tatizo hili huweza kujitokeza vile vile kwa sababu ya kansa, ambayo huitwa malignant ascites,aina hiyo mara nyingi ni ishara ya kansa zilizokomaa ndani ya tishu zilizomo kwenye uwazi wa tumbo, kama saratani ya utumbo mkubwa, saratani ya kongosho, saratani ya tumbo, saratani ya matiti, lymphoma, saratani ya mapafu, au saratani ya ovari.

Dalili 

Mpendwa msomaji wetu fahamu kua kunaweza kusitokee dalili zozote za kukujulisha kua una tatizo la kujaa maji tumboni hasa wakati tatizo ni dogo (maji pungufu ya mililita 100-400 kwa mtu mzima). Kadiri maji yatakavyoongezeka, kipimo cha mzunguko wa tumbo na ukubwa wa tumbo vitaongezeka na kuonekana kwa macho.
Kadhalika dalili hizi zitakua ni zenye kujitokeza yani
Kupata maumivu ya tumbo
Kukosa raha
Kuvimba au kuwamba kwa tumbo kutaonekana.
Kukosa pumzi kutajitokeza pale tumbo litakapojaa sana kutokana na kuongezeka kwa pressure kwenye diaphragm na majimaji kuvuka diaphragm na kusababisha maji kuingia kwenye mapafu.
Kuhisi kichefuchefu,
kutosikia njaa,
uchovu, kuziba choo na kupata haja ndogo ya mara kwa mara.


VIPIMO na maTIBABU

Daktari anaweza kubaini tatizo hili kwa kuangalia tumbo la mgonjwa kadhalika vipimo vifuatavyo hutumika kubaini tatizo hili vipimo hivyo ni
Blood tests, fluids sample analysis, abdominal ultrasound,MRI,na X-RAYS.
Matibabu ya tatizo hili la maji kujaa tumboni kwa kiasi kikubwa hutegemea kuangalia chanzo halisi cha ugonjwa huu.
 Kwa mfano, ikithibiti mgonjwa ana peritoneal
 carcinomatosis au malignant ascites to atatibiwa kwa kufanyiwa  upasuaji kuondoa eneo lililoathirika na saratani au kupatiwa tiba ya mionzi (chemotherapy), wakati ascites iliyotokana na matatizo ya moyo itadhibitiwa kwa dawa za kutibu chanzo cha moyo kushindwa kufanya kazi vizuri au  mgonjwa atapatiwa ushauri wa vyakula.

Kadhalika endapo maji kujaa tumboni kumetokana na kuharibika kwa ini (cirrhosis), mgonjwa atasaidiwa kwa kushauriwa kupunguza matumizi ya chumvi na kumeza vidonge vya kutoa maji yaliyozidi mwilini. Vidonge hivyo vitamfanya atoe haja ndogo mara nyingi zaidi huku vikizuia utunzwaji wa maji mwilini. Pamoja na kuwa hii ni njia bora, aina nyingine za ugonjwa huu hazisikii tiba hii.

Hali ikiwa mbaya sana, operesheni ya kubadilisha ini inaweza kuwa ndiyo uamuzi wa mwisho.
Kadhalika tiba nyingine zinazotumika kutibu tatizo hili ni kama ifuatavyo:

Paracentesis

 Hii ni tiba ambayo hutumika kama tiba nyingine hazikutoa msaada mkubwa au kama maji ni mengi sana, tiba ya abdominal paracentesis hutumika. Hii ni njia ambapo daktari huingiza sindano tumboni na kutoa maji yaliyozidi nje ya mwili.
Lengo ni kupunguza msukumo ndani ya tumbo, na kumfanya mgonjwa ajisikie vizuri. Maji yanayotolewa yanaweza kufika lita 5, ingawa kuna wagonjwa wenye hali mbaya zaidi ambao hutolewa maji zaidi ya lita 10.

shunts

Kadhalika tiba hii hutumika endapo maji yamejaa tumboni kutokana na kansa hivyo daktari anaweza kutumia mpira kuondoa maji kutoka kwenye tumbo na kuyaingiza kwenye mtiririko wa damu.
Daktari huchoma sindano kwenye neva ya shingoni na kuweka shunt kupitia
kifuani. Shunt hiyo huunganisha uwazi wa tumbo na shingo, na kuingia kwenye veni. Na hivyo maji hutiririka kupitia mrija huo hadi kwenye mzunguko wa damu.

chemotherapy

Matibabu ya chemotherapy yanaweza kutumika kudhibiti saratani. Inaweza kufanywa kutumia mpira unaoingizwa tumboni, ingawa hakuna ushahidi wa kuwa njia hii ina matokeo bora.



HATUA ZA KUFATA KUTIBU/KUPUNGUZA UKUBWA WA TATIZO LA TUMBO KUJAA MAJI (EXCESS ABDOMINAL FLUIDS /ASCITES)

Kuna mambo kadhaa yanayoweza kukusaidia kuweza kutibu au kupunguza ukubwa wa tatizo hili ambalo hukuweka katika hatari ya kupata tatizo la ini na saratani au matatizo ya figo,mapafu na magonjwa mengine mbalimbali

Unashauriwa kuacha kunywa pombe.

Kupunguza uzito uwe na uzito stahiki katika afya(usiwe na uzito mdogo sana au mkubwa Sana)

Dumu kufanya mazoezi mara kwa mara.

Acha kuvuta sigara,bangi na kula mirungi

Punguza matumizi ya chumvi katika vyakula vyako

Kama umeoa au kuolewa unashauriwa kushiriki tendo la ndoa mara kwa Mara ili kupunguza nafasi ya kupata ugonjwa wa hepatitis (epuka ngono zembe kuepusha kuambukizwa ugonjwa wa hepatitis)

Epuka kutumia dawa hovyo hovyo pasipo kupata ushauri kutoka kwa daktari

Pata usingizi wa kutosha na ondoa msongo wa mawazo

VIFAHAMU VYAKULA VYENYE KUSAIDIA KUPUNGUZA MAJI YALIYOJAA TUMBONI

1)KITUNGUU SAUMU(GARLIC)
Vitunguu saumu vimeonekana kuwa na uwezo wa kuponya tatizo la tumbo kujaa maji (ascites). Chukua punje 20 za vitunguu saumu na maji kiasi cha 125 mls visage kwa pamoja
Kisha kunywa mchanganyiko huo mara kwa mara kwa siku moja uwe umeumaliza
Kadhalika ili kupata matokeo mazuri tengeneza mchanganyiko huo kila siku na uwe unafululiza kunywa angalau kwa siku 14 utaona matokeo.

2) MBEGU ZA UWATU(FENUGREEK SEEDS)

Ili uweze kutumia mbegu za uwatu kutibu tatizo la tumbo kujaa maji loweka mbegu za uwatu kiasi cha gram 25 usiku kisha unywe maji hayo asubuhi
Unashauriwa kuendelea na zoezi hili kwa muda usiopungua wiki mbili ili kupata matokeo mazuri

3) VITUNGUU MAJI(ONIONS)

 ni miongoni mwa viungo vyenye nguvu katika kutibu magonjwa mbalimbali. Kwa hivyo, unashauriwa  kuvijumuisha katika lishe yako  kwa kuvitafuna vibichi kila siku.
Hii itasaidia kuyatoa maji yaliyokusanywa tumboni  kupitia njia ya mkojo
Unashauriwa kutafuna walau vitunguu maji vikubwa vitatu kila siku


4) MAFUTA YA UFUTA (SESAME OIL)NA MAFUTA YA MNYONYO(CASTOR OIL)
Unashauriwa kulikanda kanda tumbo kwa kutumia mafuta ya ufuta(sesame oil) au mafuta ya mnyonyo (castor oil) kwakua kulikanda tumbo inasaidia kuondoa maji kupita kiasi kutoka ndani ya mwili

NOTED
Mpendwa msomaji wetu fahamu kua tatizo hili la tumbo kujaa maji ni tatizo la hatari lisipotibiwa mapema linaweza kusababisha madhara makubwa kwa mgonjwa kama vile kupata maradhi ya KANSA,INI, MAPAFU NA FIGO pia huweza kupata magonjwa ya moyo.
Iwapo wewe au ndugu yako ana tatizo hili mshauri apate kufika hospital iliyo karibu naye kwa msaada wa huduma ya matibabu zaidi.

MATIBABU YA TATIZO LA TUMBO KUJAA MAJI(EXCESS ABDOMINAL FLUIDS/ASCITES NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER



Mpendwa msomaji Kama una tatizo hili au ndugu yako ana hili tatizo la tumbo kujaa maji na magonjwa mengine mbalimbali na umejaribu njia kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)


Green health consultation center tutakufanyia uchunguzi kujua chanzo cha tatizo kisha tutakupatia huduma na tutakupatia ushauri sahihi wa kupambana na ugonjwa huo na magonjwa yote yanayokusumbua karibu sana ofisini kwetu tuweze kukuponya tatizo lako


Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud ) 

0 comments:

Copyright © 2017 Green health consultation centre