FAHAMU CHANZO NA TIBA YA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA WANAWAKE





CHANZO na TIBA ya tatizo la WANAWAKE KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA



Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, Mpendwa msomaji ni matumaini yetu kwamba wewe pamoja na familia yako ni wazima karibu tena katika blog yetu tuweze kufahamu Tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa au kukosa nyege kwa lugha ya mitaani.
Tatizo hili ambalo huwatokea zaidi wanawake kuliko wanaume lakini ni wanaume wanaokerwa zaidi na tatizo hili kuliko wanawake. Wakati takwimu inaonyesha  ni asilimia 15 hadi 16 ya wanaume wenye tatizo hili, idadi ya wanawake ni mara mbili ya hii ya wanaume. Huku takwim ikionyesha  ni asilimia 23 ya wanaume wanaonyesha kuridhika kuishi na tatizo hili, asilimia 46 ya wanawake wapo radhi kabisa kuendelea kuishi na tatizo hili.
Si lazima kuendelea kuishi na tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa sababu kuna mambo mengi unayoweza kuyafanya ili kuondokana na hili tatizo.
Hali ya kupenda kufanya mapenzi au tendo la ndoa kwa mwanamke inabadilikabadilika sana ikipanda na kushuka kulingana na matukio mbalibali yanayomtokea katika maisha yake. Baadhi ya matukio yanayoathiri hamu ya mwanamke kufanya mapenzi ni pamoja na kuanza na kwisha kwa mahusiano ya kimapenzi na mwanamme, kupata ujauzito, na magonjwa. Kama wewe mwanamke umepatwa na hali hii unaweza kukabiliana nayo kwa kubalisha jinsi unavyoishi, kufanya mambo kadhaa yatakayo badilisha hali hii au kutumia baadhi ya dawa zinazosaidia kuondoa tatizo hili.

SABABU ZA MWANAMKE KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA

Sababu zinazoweza kupelekea mwanamke kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa ni nyingi lakini kwa ujumla karibu zote tunaweza kuzigawanya katika makundi manne:
1. Mahusiano Baina Ya Mwanamke Na Mwanamme                                     Kwa wanawake walio wengi ukaribu wa kihisia ndicho kitu cha kwanza katika kujenga mapenzi kati yake na mwanamme. Hivyo, mahusiano mabovu yaweza kuwa ndicho chanzo cha kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanamke. Mwanamke atakosa hamu ya kufanya mapenzi endapo hakutokuwa na mawasiliano baina yake na mumewe, kutakuwa na migogoro kati yake na mumewe isiyokwisha, kutakuwa na ukosefu wa mawasiliano kuhusu mahitaji yake ya kufanya mapenzi na jinsi ambavyo yeye angependa kufanyiwa kimapenzi na kama atahisi kuna ukosefu wa uaminifu katika ndoa au mahusiano yao.
2. Matatizo Katika Maisha                                                                              Matatizo mbalimbali katika maisha ya mwanamke humsababishia kukosa hamu ya kufanya mapenzi. Baadhi ya matatizo ambayo huweza kusababisha mwanamke kukosa hamu ya kufanya mapenzi ni pamoja na magonjwa, mabadiliko katika mwili wake na hata matumizi ya baadhi ya madawa:
Matatizo Katika Kufanya Tendo La ndoa. Kama mwanamke anapata maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa au kama mwanamke anakosa kufika kileleni, hali hii inaweza kusababisha akakosa kabisa hamu ya kufanya mapenzi.
Matatizo ya afya. Magonjwa mengi husababisha mwanamke akose hamu ya kufanya tendo la ndoa. Baadhi ya magonjwa ni Kansa,maambukizi katika via vya uzazi(pelvic inflammatory disease,shinikizo la damu, matatizo katika mishipa ya damu ya arteri na matatizo ya akili 
Matumizi ya madawa. Baadhi ya madawa yakitumiwa, huondoa kabisa hamu ya kufanya mapenzi kwa mwanamke. Mfano wa dawa hizo ni madawa ya kukabiliana na msongo wa mawazo.
Mtindo wa maisha. Matumizi ya pombe kuzidi kiwango, uvutaji wa sigara na madawa ya kulevya huathiri hamu ya kufanya mapenzi.
Upasuaji. Upasuaji uliofanyika katika maeneo ya maziwa au katika maeneno ya viungo vya uzazi humbadilishia mwanamke mwonekano wake, huathiri ufanyaji kazi wa viungo hivyo na mwisho kuathiri hamu yake ya kufanya mapenzi.
Uchovu. Uchovu unaotokana na kulea watoto wadogo au vikongwe huweza kuathiri hamu ya mwanamke ya kufanya mapenzi.
3. Mabadiliko Katika Mfumo Wa Homoni.                                                           Kukoma Hedhi. Mabadilko ya viwango vya homoni katika mwili wa mwanamke yanaweza kusababisha kukosa hamu ya kufanya mapenzi kwa mwanamke. Kupungua kwa Estrogen katika mwili wa mwanamke katika kipindi cha kuelekea kukoma hedhi kunaweza kusababisha ukosefu wa hamu ya kufanya mapenzi. Upungufu wa homoni hiyo husababisha uyabisi wa wa viungo vya sehemu nyeti na kusababisha maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Mwanamke pia huweza kuwa na upungufu wa homoni ya testosterone, homoni ambayo husaidia kuongeza hamu ya kufanya mapenzi kwa wanaume na wanawake, hivyo mwanamke huyo akapungukiwa na hamu ya kufanya mapenzi.
Pamoja na kuwa wanawake wengi huendelea kupata hamu ya kufanya mapenzi baada ya kukoma hedhi, baadhi kupungukiwa na hamu hiyo baada ya mabadiliko haya ya viwango vya homoni katika miili yao.
Ujauzito na kunyonyesha. Mabadiliko katika mfumo wa homoni wakati wa ujauzito, baada ya kujifungua na wakati wa kunyonyesha huweza kusababisha mwanamke kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa.
4. Matatizo Ya Kisaikolojia                                                                                             Matatizo ya kisaikolojia yana mchango katika kumfanya mwanamke akose hamu ya kufanya tendo la ndoa. Baadhi ya mtatatizo hayo ni:
  •  Waswasi na kuwa na msongo wa mawazo
  •  Kuwa na mawazo mengi kuhusu matatizo ya kifedha au kikazi
  •  Kuhisi kutothaminiwa katika jamii
  •  Kuwa na historia ya kunyanyaswa kimwili au kijinsia kama kupigwa   au kubakwa
  •  Kuwa na historia mbaya ya kimapenzi

MATIBABU YA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA MWANAMKE

Hakuna dawa ya moja kwa moja toka hospitalini kwa sasa hivi kwa ajili ya kuondoa tatizo hili, hata hivyo wanawake wengi wanaweza kurudi kwenye hali zao za kawaida kwa kushirikiana na waume zao waelewa.
Katika nchi zilizoendelea, kila siku wamekuwa wakija na dawa na vifaa vipya vya kuondoa tatizo hili na vingi bado ni vya bei kubwa na/au vinapatikana kwa shida. Vipo ambavyo vimeonyesha mafanikio makubwa, mifano ya vitu hivyo ni Suction Vibrators, Desire Creams na Erection Drugs..

VYAKULA VINAVYOONGEZA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA WANAWAKE

Utafiti umeonyesha pasi shaka kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya chakula tunachokula na afya ya viungo vya uzazi. Baadhi ya chakula na virutubishi vimehusishwa na hamu ya kufanya mapenzi (nyege). Virutubishi ndani ya chakula ambavyo vinasaidia hali hiyo ni antioxidants, vitamin C, vitamin E, potassium na zinc. Kirutubishi cha zinc ambacho hupatikana ndani ya  vitunguu swaumu, mbegu za maboga, ufuta na mbegu za matikitimaji, kinaongeza mbegu kwa mwanamme (sperm count) hivyo humsaidia kuongeza hamu ya kufanya Ma ndoa. Chakula cho chote chenye virutubishi hivi kikiliwa, humfanya mlaji asikie hamu ya kufanya mapenzi au kwa maneno ya mtaani, chakula hiki kinasaidia kuongeza nyege. Baadhi ya chakula cha kuongeza nyege ni:
TIKITIMAJI


Hili linachukuliwa kuwa ndilo tunda bora katika kuboresha afya ya mapenzi. Tunda hili lina asilimia 92 ya maji na asilimia 8 zinazobakia zina phytonutrient citrulline ambayo hugeuzwa kuwa arginine. Arginine ni amino acid ambayo hufanya mishipa ya damu kuwa kwenye hali ya ubora wake na kusadia damu kupita vizuri zaidi. Tikitimaji kwa hiyo husaidia damu ifike kwa kiwango kizuri zaidi kwenye sehemu ambazo hutakiwa kutanuka wakati mtu akipata hisia za kufanya tendo la ndoa ambazo ni viungo vya ndani ya kisimi cha mwanamke

PILIPILI
Kama tunavyojua wote mara nyingi chakul ambacho kimeungwa pilipili hufanya hat mapigo ya moyo kuwa tofauti na waka mwingine hata jasho kutoka au kama kutoka. Kwenye pilipili kuna kitu kinaitwa capsaicin ambacho hufanya pilipili iwe na hali ya ukali ambao huwezesha ubongo kutoa homoni ya endorphins ambayo katika hali ya juu huleta mgusu wa hisia za raha
Pia pilipili husisimua mfumo wa ufaham (nerves) wa ubongo na katika kufanya hivyo huwezesha kuamshwa haraka kimapenzi (kunyegeka) na pia ili ukiguswa au kubusiwa au kunyonywa au kupapaswa uweze kupata hisia kila sehemu 
NAFAKA
Nafaka zina nyuzinyuzi (fibre) na suka ngumu (complex sugar) ambazo kusaidi kutunza uzito wa mwili. Nafaka husaidi katika kuzalisha homoni za testosteron kwenye damu. Na pia nafaka huwezesh mtu kuwa na nguvu hatimaye kwend masafa marefu wakati wa tendo. Kula nafaka nzima kama vile brown bread badala ya white bread, pia kula nafaka halisi badala ya cornflakes ni jambo zuri linalokuhakikisha afya njema na mahusian mazuri ya ndoa yako 

MATUNDA NA MBOGAMBOGA ZA MAJANI
Mlo wenye matunda na mboga za maja una matokeo makubwa sana katika ham ya tendo la ndoa kwa njia nyingi. Kwanza matunda na mboga za majani hupunguza kiwango cha mafuta na unene (cholesterol kuongezeka kwa mafuta mwilini huzui mzunguko wa damu kwa kubana mishipa ya damu. 
Pia kula matunda na mboga za majani huhakikisha balance ya uzito kwa unene (obesity) kwa wanaume kuna matokeo mabaya katika kuzalisha home za testoeterone na hatimaye jogoo kushindwa kuwika na kuwa na libido kidogo. Na pia wanandoa wanapozidi kunenepeana ndipo na hali ya kufurahia na kutaka au hamu ya tendo la ndoa huzidi kupungua. 

TANGAWIZI
Tangawizi ni chakula ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini, na tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume. Inaweza kuliwa mbichi, au kupikwa na kuanikwa na kuwa kama unga. 

ASALI

Asali ina madini yanayoitwa boron, ambay husaidia mwili kutumia homoni ya estroge ambayo ni homoni inayohusika na viung ya uzazi na mapenzi kwa mwanamke. Pi kuna utafiti unaoonesha kwamba asa huongeza nguvu, kitendo ambach kitapelekea mwanamke kuwa uwezo n hamu ya tendo la ndoa au libido. 

KARANGA
Karanga huhusika moja kwa moja n kutunza mfumo wa mzunguko wa damu kuwa na afya (vascular system). Pia mfumo wenye afya (mzunguko wa damu) katika uke na uume huwezesha mwanaume na mwanamke kupata msisimko wa mapen haraka hatimaye tendo la ndoa kuwa zuri 
Pia karanga zina madini muhimu kama vile magnesium, asidi ya folic na zinc ambayo muhimu sana katika usalishaji wa mbegu za mwanaume. 

OYSTERS
Huwa na kiasi kikubwa sana cha madini ya zinc na haya madini ndiyo huhusika zai na uzalishaji wa homoni ya testosteron kwa wanaume. Pia imethibitika kwamba wanaume wenye ukosefu wa madini ya zinakuwa na matatizo ya nguvu za kiume na wakati huohuo kuwa na madini mengi ya zinc mwilini huongeza kiwango cha shahawa. 

SOYA
Pamoja na kuwa na kiwango kidogo san cha fat na pia kuwa na kiwango kizuri ch protein, soya zina phytoestrogens ambay husaidia sana wanawake ambao wamefiki menopause kutengeneza homoni estrogen y ziada. Husaidia uke kuwa laini (we lubricated) mwanamke akisisimliwa waka wa tendo la ndoa. 

CHOCOLATE
Chocolate ina phenylethylamine, kemika ambayo husababisha hisia (feelings) z furaha wakati wa mwanamke na mwanaume kufika kileleni (orgasm)


MATIBABU YA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA WANAWAKE CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na umejaribu njia hizo hapo juu bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255623026602/+255746465095)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kuongeza hamu ya tendo la ndoa na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI

KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255623026602/+255746465095(Dr Naytham S Masoud )

1 comment:

Copyright © 2017 Green health consultation centre