FAHAMU CHANZO NA TIBA YA TATIZO LA MWANAUME KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA







CHANZO NA TIBA YA TATIZO LA MWANAMME KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA



Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul mpendwa msomaji wetu ni matumaini yangu kwamba wewe na familia yako mnaendelea vizuri kiafya leo napenda tulijadili tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa, kwa maneno lugha ya mitaani linaitwa tatizo la kukosa nyege. Tutajadili sababu zinasababisha mwanamme kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa, madhara yanayotokana na hali hiyo na kisha kuona ni nini cha kufanya ili kuongeza hamu ya kufanya tendo la ndoa au kuongeza nyege. Bahati nzuri ni kwamba kuna mambo unayoweza kuyafanya kupunguza ukubwa wa tatizo hili au kuliondoa kabisa. Watu wengine wanamini kuwa hamu ya kufanya tendo la ndoa inapungua kadri umri wa mwanamme unavyoongezeka. Wakati ni kweli kwamba hilo huwatokea wengi,ila sio lazima kwamba hamu ya kufanya mapenzi ipungue umri unapoongezeka. Kuna idadi kubwa tu ya wanaume ambao hamu yao ya kufanya tendo la ndoa imebaki vilevile hata umri wao ulipokuwa mkubwa kabisa. Kwanza tuanze kwa kutazama ukubwa wa tatizo hili.

UKUBWA WA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA

 Wanaume wengi hawapenzi kulizungumzia tatizo hili waziwazi na hata wanawake pia. Pamoja na kwamba tatizo hili halijitokezi sana kwa wanaume ukilinganisha na wanawake, inakadiriwa kuwa asilimia 15 hadi 16 ya wanaume wana tatizo hili, kwa lugha nyepesi kuna mwanamme mmoja mwenye tatizo hili baina ya kila wanaume sita au saba. Idadi ya wanawake wenye tatizo hili ni mara mbili ya wanaume. Tatizo hili huwakera zaidi wanaume kuliko wanawake kwa sababu wanaume huchukulia urijali kama sehemu ya ukamilifu wa mwanamme na hunyongea wanapoona wana mapungufu kuhusu mambo ya mapenzi, tofauti kabisa na wanawake.Idadi ya wanaume wanaoridhika kuishi na tatizo hili ni ndogo sana ukilinganisha na ile ya wanawake. Hata hivyo tatizo la mwanmme kukosa hamu ya kufanya mapenzi limebainika kuwa ndilo linaloongoza katika kuleta migogoro ya unyumba kuliko matatizo mengine yote.
 NAMNA UNAVYOWEZA KUGUNDUA KAMA UNA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA
Tatizo hili halitokei ghafla kama vile umelala halafu ghafla asubuhi unaamka una mafua, la hasha. Ni kitu kinachotekea pole pole na pengine mwenyewe usijigundue. Sanasana pima mwenendo wako wa masuala ya mapenzi kwa mwaka uliopita au miezi kadhaa iliyopita. Vile vile kutofanya tendo la ndoa kwa kipindi fulani haimaanishi kutokuwa na hamu ya kufanya mapenzi, pengine una hamu thabiti lakini mazingira hayakukuruhusu. Lakini iwapo hakuna kikwazo cho chote na upo na mwenzi wako halafu inapita wiki bila kufanya tendo la ndoa au unalifanya tendo hilo mara moja au mbili tu kwa mwezi, inabidi uanze kujiuliza maswali. Lakini ieleweke pia kuwa kuhesabu umefanya tendo la ndoa mara ngapi katika kipindi fulani si kipimo pekee cha tatizo hili. Mawazo yako kwa ujumla kuhusu tendo hili ni muhimu pia – jinsi unavyolichukulia na kuliwazia tendo hili kabla, wakati wa tendo na baada ya kumaliza tendo ni muhimu katika kujipima.
Viashiria vingine vyaweza kuwa: kumtomasa mkeo mkiwa ndani tu – chumbani na si penginepo. Iwapo tendo hili unalifanya pale tu mwezi wako anapokuanza na huwa unalifanya kama mazoea bila kuwa na mawazo ya kushiriki kikamilifu. Kama humwazii mpenzi wako anapokuwa hayupo kwamba angekuwapo ungeweza kufanya naye tendo la ndoa. Vitu hivi kama vinakutokea basi kuna dalili za kuwa unakosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na kwamba inabidi utafute suluhisho.

VISABABISHI VYA TATIZO LA KUKOSA HAMU  YA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA WANAUME

Tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanamme linaweza kusababishwa na vitu vingi sana. Sababu hizo zinaweza kuwa za kimaumbile au kisaikolojia au za mchanganyiko wa vitu hivyo viwili. Hebu tuone baadhi ya vyanzo vya tatizo hili.

Mahusiano Baina Ya Mwanamme Na Mwanamke
Matatizo ya mahusiano kati ya mwanamme na mwanamke yana mchango mkubwa sana katika kusababisha tatizo la kukosa hamu ya mapenzi. Jee, unapata raha na una amani katika mahusiano yako na mpenzi wako? Huna wasiwasiwo wote na mahusiano yenu? Haya ni maswali ya msingi ya kujiuliza.
Kama mahusiano yako na mpenzi wako yamekuwa ya miaka mingi sana, unaweza kuwa umemzoea mno mkeo kiasi kwamba ukaanza kukosa hamu ya kufanya naye tendo la ndoa. Hili nalo hutokea mara nyingi.
 Kama kuna mambo yanasababisha tendo la ndoa lisifanyike kwa urahisi, ufanisi na kufurahia, hamu ya kufanya tendo hilo inaweza kupungua. Kwa mfano, kama mwanamme anawahi kufika kileleni au kama ana matatizo ya kushindwa kusimamisha uume tendo zima la ndoa halitakuwa la kukufurahisha sana hivyo unaweza kupoteza hamu ya kulifanya. Hebu fikiria tunda linalokufurahisha sana ukilila, ukilikosa kwa siku kadhaa, utalikumbuka na kulitafuta lakini ambalo halikufurahishi sana ukilila hutalikumbuka na kulitafuta.
 Mawazo Mengi Na Uchovu
Matatizo ya kikazi na hadhi yako kazini vyaweza kuchangia. Kama unabezwa sana kazini na kujiona hutimizi kazi yako ipasavyo au kama unachoka sana kazini unaweza pia kukosa hamu ya kufanya mapenzi urudipo nyumbani. Kukosa mpango mzuri wa shughuli zako za kila siku na kujaribu kulazimisha kufanya mapenzi katikati ya ratiba yako iliyojaa. Mahusiano ya kimapenzi yanataka yatengewe muda wake na unaotosha.
 Msongo Wa Mawazo
Msongo wa mawazo (depression) unatofautiana na kukosa raha au kujisikia si mtu wa thamani kwa kipindi kifupi. Msongo wa mawazo ni ugonjwa wa hali ya kuwa na mawazo makali ya muda mrefu ya kukukosesha raha kutokana na kujisikia si mtu wa thamani au kukosa starehe katika vitu ulivyozoea kuvifanya na kukufurahisha hapo zamani. Mawazo ya namna hii huathiri mwenendo wako wa maisha yako pamoja na matamanio yako ya kimapenzi.
Matumizi Ya Madawa Na Pombe
Matumizi ya baadhi ya madawa na unywaji wa pombe wa kupindukia huweza kuleta tatizo hili la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa. Madawa yanayochangia tatizo hili ni pamoja na:
– madawa ya high blood pressure
– madawa ya kuondoa msongo wa mawazo
– madawa yote yanayozuia ufanyaji kazi au uzalishaji wa testosterone, kwa mfano, cimetidine, finasteride na cyproterone
– na mengineyo
 Umri Kuwa Mkubwa
Homoni ya msingi sana kuhusiana na masuala ya mapenzi huitwa testosterone. Kwa mwanammme homoni hii hutolewa kwa kiwango kikubwa na korodani na kwa mwanamke hutolewa na ovari. Homoni ikipungua katika mwili wa binadamu, humfanya apoteze hamu ya kufanya tendo la ndoa. Kiwango cha testosterone katika mwili wa mwanamme hupungua kwa asilimia 1-2 kila mwaka kadri mwanamme anvyozidi kuwa na umri mkubwa. Kiwango cha testosterone kikishuka sana katika mwili wa mwanamme huyu humfanya asiwe na nguvu, ashindwe kutuliza mawazo kwenye jambo alifanyalo na apoteze hamu ya kufanya mapenzi.
Matatizo Katika Mfumo Wa Homoni
Tumeshaona kwamba upungufu wa homoni inayoitwa testosterone unasababisha kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa. Matatizo mengine katika mfumo wa homoni huchangia tatizo hili. Kama thyroid haitoi homoni za kutosha, tatizo hili huweza kutokea ingawa mchango wa thyroid katika tatizo hili ni mdogo sana. Thyroid ni kiungo cha kuzalisha homoni kilichopo katika eneo la shingo.
Tatizo hili linaweza kutokea pale homoni zinapozalisha kitu kinachitwa prolactin kwa kiwango kikubwa mno na kukisambaza ndani ya mfumo wa damu. Hali hii kiutaalamu huitwa hyperprolactinaemia.
Matatizo Ya Kiafya
Matatizo ya kiafya ya muda mrefu husababisha kupungua kwa hamu ya kufanya tendo la ndoa. Matatizo ya moyo ya muda mrefu, kuwa na kisukari kwa muda mrefu, kansa ya muda mrefu na hali ya kuwa na unene wa kuzidi kiwango ni baadhi tu ya matatizo yanayochangia tatizo hili.
 MATIBABU YA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA WANAUME
 Kuna mambo ambayo unaweza kuyafanya kuongeza na kudumisha hamu ya kufanya tendo la ndoa. Tatizo hili halijapatiwa dawa za kwenye mahospitali isipokuwa pale unapogundulika kuwa una kiwango kidogo cha testosterone ambapo utaandikiwa namna ya kukiongeza kiwango chako. Fanya yafuatayo kuongeza hamu yako ya kufanya mapenzi.
1. Tafuta mchezo ambao unaweza kushiriki au fanya mazoezi kama vile ya kutembea au kukimbia. Kila siku ufanyapo mazoezi yako jaribu kila siku kufikia kiwango cha juu zaidi ya kile ulokwisha kifikia.
2. Inasaidia kufahamu kuwa ni asilimia 40 hadi 50 ya matendo ya ndoa mnayoyafanya yatawaridhisha wote wawili. Kukosa kumridhisha mwenzio iwe changamoto ya kukufanya ufanye utafiti na utundu wa kuboresha tendo mtakapokutana tena.
3. Kama nilivyodokeza hapo juu, jaribuni kwa pamoja kujadili jinsi ya kuboresha namana yenu ya kushiriki katika tendo la ndoa kila mmoja akieleza kile ambacho angependa afanyiwe. Inasaidia kusoma maandishi kutoka sehemu mbalimbali na kutazama mikanda mbalimbali.
4. Kufanya tendo kwa kushitukiza inapendeza wakati fulani. Lakini hili kidogo linaweza kuwa si zuri ukizingatia majukumu ya kila siku ya maisha ya sasa, si rahisi kupata muda wa kutosha wa kustarehe na mpenzi wako. Kuwa na mpango na ratiba ni bora zaidi na inasaidia kuleta hamu mtu anapokisubiri kitu kilichopangwa siku fulani na muda fulani – fikiria unaposubiri mechi kubwa ya timu yako. Mletee zawadi mpenzi wako, weka muziki mororo ulikuwa unaupenda siku zile, zimisha simu na hakikisha kuna mazingira ya utulivu na ukimya.
5. Hamu huongezeka inapoona kitu kipya. Ukienda na mwenzi wako kwenye sherehe nje ya nyumba yenu, utapata fursa ya kumwona mkeo kwa namna nyingine. Utaweza kuuona uzuri wake na yeye pia atakuona wewe kwa namna nyingine. Wote mtakumbuka vitu ambavyo kila mmoja wenu vilimvutia kwa mwenzie

MATIBABU YA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA WANAUME KUPITIA VYAKULA ASILI

Historia yetu inaonesha kuwa kwa kipindi kirefu, wanawake na wanaume wamekuwa wakitumia chakula kumvutia mpenzi. Mara nyingine chakula hicho kinakuwa kinaongeza hamu ya kujamiiana na kuna wakati ni harufu au ladha ya chakula hicho ndiyo inayokufanya kupata hisia hizo. muonekano wake, ladha yake unapokila, uhaba wake.

ASALI

Pamoja na utamu wake, asali ina nafasi kubwa ya kuongeza hamu ya kujamiiana kwakuwa ina aina zote za madini ya Vitamin B, ambayo ndio yanasaidia sana kuupa mwili nguvu.

Unaweza kula vijiko kadhaa kila siku, wengine huichanganya wakiwa wanaotengeneza keki, kuipaka kwenye mkate au chakula chochote.

SHAYIRI

Maji ya shayiri asubuhi au jioni yanasaidia kuongeza hamu ya kujamiiana. Shayiri madini ya L-arginine yanayoongeza homoni za testosterone, pia ina wingi wa kundi la Vitamin B. Shayiri huuzwa bei nafuu na ni njia rahisi sana ya kuongeza msukumo wa damu, jambo ambalo hutokea unapofanya mapenzi. Shayiri inapotumiwa kwa muda mrefu inasaidia kupunguza uwezekano wa kupata matatizo ya kusimama kwa uume.

PARACHICHI

Wataalamu wa masuala ya mapenzi wanasema kuwa parachichi linaingia kwenye kundi hili kwakuwa umbo lake linafananishwa na maumbile ya mwanaume au mikunjo katika mwili wa mwanamke na kwamba ulaini wake na jinsi linavyotoa majimaji huongeza hisia za mapenzi. Yanaweza kuliwa yenyewe au kwa kuchanganywa kwenye vyakula vingine.

Yana kiwango kikubwa cha mafuta na vitamin E vyenye kazi ya kuongeza msukumo wa damu, hivyo kuongeza kiwango cha utengenezwaji wa testosterone. Kama hutaki kutumia parachichi kwa kazi hii, basi litakusaidia kwa kung’arisha ngozi kutokana na madini ya vitamin E.

MBEGU ZA MABOGA

Mbegu za maboga zina wingi wa madini ya tyrosine (aina mojawapo ya asidi aina ya amino inayosaidia kuchangamsha mwili). Mbegu hizi pia zina virutubisho vingi vinavyosaidia kuongezeka kwa msukumo wa damu mwenye viungo vya uzazi.

Unaweza kuzioka kwenye oveni, kuzisaga au kula kwa kuzichanganya na vyakula vingine, ikiwamo asali pia – ili kuongeza faida zaidi.

TIKITI MAJI

Wataalamu wanasema kuwa watu wengi hawajui jambo moja kuhusu tiketi: kwamba kama ambavyo tiketi linaweza kukata kiu yako kwa wingi wa maji yaliyomo, ndio hivyo hivyo inavyoweza kukusaidia kwenye maswala ya kujamiiana. Utafiti umeonesha kuwa tunda hilo lina kiwango kikubwa cha viambata aina ya citrulline, ambayo ina kazi sawa na dawa aina ya Viagra kwa mwanaume.

TANGAWIZI
Tangawizi inafanya damu iende kwa kasi jambo linaloweza kusababisha mwili uweze kupata msisimko wa kimapenzi kirahisi sana. Pia inasaidia kuboresha mfumo wa usagaji wa chakula, jambo linalosaidia sana kukufanya ubaki kuwa na hamu ya kufanya mapenzi kama umekula chakula kingi.

CHOCOLATE

Wataalamu wanasema kuwa dawa pekee ya ukweli kwenye maswala ya mapenzi ni cocoa. Cocoa inachochea uzalishaji wa homoni zinazofanya ujisikie vizuri aina ya serotonin na dopamine, na ina kemikali aina ya phenylethylamine, inayotengenezwa kwa wingi kwenye ubongo unapoingia mapenzini. Cocoa inafanya kazi hii hasa inapochanganywa na chokoleti kwakuwa inayeyuka kirahisi na kuleta hamasa ya kimapenzi mdomoni. Kwakuwa chokleti ni nzuri unapoila—na inafanya tujisikie vizuri baada ya kuila—zawadi inayomfanya mtu apate hisisa nzuri siku zote lazima itapendwa.

MATIBABU YA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA WANAUME CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na umejaribu njia hizo hapo juu bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255623026602/+255746465095)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kuongeza hamu ya tendo la ndoa na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako
Mpendwa msomaji nashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

0 comments:

Copyright © 2017 Green health consultation centre