FAHAMU MATIBABU YA TATIZO LA KUTOKWA DAMU KIPINDI CHA KUKOMA HEDHI,MAANA YA KUKOMA HEDHI,MATATIZO YANAYOTOKEA KIPINDI CHA KUKOMA HEDHI (POSTMENOPAUSE)

FAHAMU MAANA YA KUKOMA HEDHI,MADHARA YANAYOTOKEA KIPINDI CHA KUKOMA HEDHI NA MATIBABU YAKE


Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatuli nina imani sote hatujambo
Sifa na utukufu tumrudishie Mwenyezimungu na atujaalie khery zaidi katika maisha yetu
Ameen!
Naam kama ilivyo ada yetu rejea kichwa cha habari hapo juu kinaelezea mada ya kukoma kwa hedhi
Nina imani posti zangu nilizoanza Kuchambua mada hii ya mambo yote yanayohusu hedhi uliziona na ukasoma
Mpendwa msomaji kama hukusoma nakuomba urejee posti za nyuma ili upate faida za kufahamu mambo yanayohusu hedhi kiundani zaidi
Kutokana na mfululizo wa mada hii ya hedhi leo tun toahitimisha kwa kuelezea hatua ya mwisho kabisa katika mlolongo wa mada ya hedhi,tuanze kwa kujadili maana ya Kukoma HEDHI na matatizo yanayopatikana pia naatibabu yake

 MAANA YA KUKOMA HEDHI (MENOPAUSE)
Kukoma hedhi ni hali ya kawaida ambayo wanawake wote huipitia umri ukiwa mkubwa. Neno kukoma hedhi linaweza likaelezea mabadiliko yoyote yanayomtokea mwanamke muda mfupi kabla au baada ya kuacha kupata siku zake, ikiwa ni ishara ya mwisho wa kuzaa.

Mwanamke huzaliwa akiwa na idadi kamili ya mayai, ambayo hutunzwa ndani ya ovari. Ovari hizi pia hutengeneza homoni za estrogen na progesterone, ambazo husimamia hedhi na upevushwaji wa mayai hivyo tunaposema kukoma hedhi maana yake ovari kukoma kuachia yai kila mwezi na kusimama kuingia mwezini(kuona damu ya hedhi kila mwezi)

Kukoma hedhi ni sehemu ya kawaida ya mwili wa mwanamke kuzeeka na hutokea baada ya kufikia umri wa miaka 40. Lakini baadhi ya wanawake wangine wanaweza kukoma hedhi mapema zaidi, ikiwa ni matokeo ya upasuaji, kama hysterectomy, au uharibifu kwenye ovari, kama baada ya tiba ya chemotherapy hivyo Kukoma hedhi kabla ya miaka 40, kwa sababu yoyote ile huitwa premature menopause.

Tuelewe kuwa kukoma hedhi kwa kawaida hakusababishwi na upasuaji au madawa.
 Ni mabadiliko ya taratibu yaliyo kwenye hatua tatu:

. Perimenopause.
Hatua hii huanza miaka michache kabla ya kukoma hedhi (menopause), wakati ovari taratibu zinaanza kupunguza utengenezaji wa estrogen. Kipindi hiki huenda hadi unapokoma hedhi, pale ovari zinapokoma kuachia mayai. Katika mwaka 1 au 2 kabla ya kukoma hedhi, utengenezaji wa estrogen hupungua kwa kasi. Ni katika kipindi hiki, wanawake wengi huona dalili za kukoma hedhi.

. Menopause.
 Hapa ni wakati mwanamke anapona kuwa umepita mwaka mmoja tangu alipopata hedhi ya mwisho. Sasa ovari zilishaacha kutoa mayai na kutengeneza estrogen.

. Postmenopause.
Hatua hii ni miaka ya baada ya kukoma hedhi. Katika kipindi hiki, dalili za kukoma hedhi kama hot flashes hupungua kwa wanawake walio wengi. Lakini madhara ya kiafya yatokanayo na ukosefu wa estrogen huongezeka kadiri umri wa mwanamke unavyoongezeka.

VISABABISHI VYA MWANAMKE KUKOMA HEDHI MAPEMA

Kukoma hedhi mapema (premature menopause) kunaweza kusababishwa na urithi,
matatizo ya kinga za mwili (autoimmune disorders), au kutokana na tiba za
afya. Sababu nyingine zaweza kuwa:

. Premature ovarian failure.
Kwa kawaida, ovari hutengeneza vyote, estrogen na progesterone. Mabadiliko katika viwango vya homoni hizi mbili hutokea, kwa sababu zisizoeleweka, na kusababisha mayai kusimama kutengenezwa mapema. Hali hii ikitokea kwa mwanamke aliye chini ya miaka 40, huitwa premature ovarian failure. Tofauti na premature menopause, premature ovarian failure si lazima iwe ya kudumu.

. Induced menopause.
Hii hutokea pale ovari zinapoondolewa kwa upasuaji kwa sababu za kiafya, kama uterine cancer au endometriosis. Induced menopause huweza pia kutokea baada ya uharibifu wa ovari kwa tiba za mionzi au chemotherapy.

DALILI ZITAKAZOKUJULISHA MWANAMKE UPO KATIKA KIPINDI CHA KUKOMA HEDHI

Wanawake wengi wanaokaribia kukoma hedhi wanapata hot flashes, yaani  ghafla kusika joto linalosambaa sehemu ya juu ya mwili, vikiambatana na hali ya kutahayari na kutokwa jasho. Hali hii huwa si kali sana kwa wanawake wengi lakini kwa wengine huwa mbaya.

Dalili nyingine zinazotokea mwanamke anapokaribia kukoma hedhi ni pamoja na:

. Hedhi zisizo na mpangilio au zinazorukaruka
. Kukosa usingizi
. Kusikia hasira mara kwa mara
. Uchovu
. Mfadhaiko
. Moyo kwenda mbio
. Maumivu ya kichwa
. Maumivu ya joints na misuli
. Mabadiliko katika kusikia hamu ya tendo la ndoa
. Uyabisi wa uke
. Shida kudhibiti haja ndogo

Si wanawake wote wanaopata dalili hizi zote.

MADHARA YANAYOPATIKANA MWANAMKE AKIKOMA HEDHI

Matatizo Ya Muda Mrefu Yanaweza kutokea baada ya Kukoma Hedhi kwa
Kukosekana kwa estrogen ndani ya damu kunakosababishwa  na kukoma hedhi kumethibitika kusababisha baadhi ya matatizo ya kiafya yanayowapata wanawake wanapokuwa na umri mkubwa.
Matatizo hayo ni
. Maumivu ya nyonga kwa muda mrefu
. Magonjwa ya moyo
. Kibofu cha mkojo kutofanya vizuri na matatizo ya haja kubwa
. Hatari ya kupata ugonjwa wa kupotteza kumbukumbu
. Mikunyanzi ya ngozi
. Kukosa nguvu za mikono
. Kupungua kwa nguvu ya kuona.
. maumivu ya miguu

TATIZO LA KUTOKWA DAMU KIPINDI CHA KUKOMA HEDHI(POSTMENOPAUSE BLEEDING)

Kawaida mwanamke akiwa ameshaingia kipindi cha kukoma hedhi hapaswi kuona tena damu ikitoka kwakua kukoma hedhi maana yake, kutotokwa na damu kwa kipindi kizima cha mwaka mmoja hivyo Ukiona damu hata kama ni vijitone tu unashauriwa kumwona daktari, ili ajiridhishe kuwa si tatizo kubwa, kama vile saratani ya kizazi nk

 CHANZO CHA KUTOKWA DAMU KIPINDI CHA KUKOMA HEDHI(POSTMENOPAUSE BLEEDING)

Mambo mengi yanaweza kuwa sababu ya damu Kutoka wakati wa postmenopause nayo ni
Polyps
Hivi ni vivimbe vya tishu vinavyoota ndani ya nyumba ya uzazi au mkondo wa shingo ya uzazi, au kwenye cervix. Kwa kawaida si saratani, lakini vinaweza kusababisha vitone vya damu, kutoka damu nzito, au damu baada ya tendo la ndoa.



. Endometrial atrophy (thinning of the uterine lining):
Endometrium ni tishu inayotanda juu ya nyumba ya uzazi (uterus). Hupokea ishara za homoni kama estrogen na progesterone. Viwango vidogo vya homoni wakati wa postmenopause huweza kuifanya isinyae na kuwa nyembaba sana. Hii inaweza kusababisha kutoka damu.

. Endometrial hyperplasia (thickening of the uterine lining):
Baada ya kukoma hedhi, unaweza kuwa na estrogen nyingi zaidi na progesterone kidogo sana. Hali hiyo inaweza kupelekea endometrium kuwa nene zaidi na kutoa damu. Wakati mwingine seli ndani ya endometrium zinaweza kugeuka na kuwa si za kawaida. Hii inaweza kuleta saratani.

. Vaginal atrophy (thinning of vaginal tissue): Estrogen husaida katika afya ya uke. Baada ya kukoma hedhi, upungufu wa estrogen unaweza kusababisha
kuta za uke kusinyaa, kuwa kavu, na kuvimba. Hali hii mara nyingi husababisha kutoka damu baada ya tendo la ndoa.

. Cancer:
 Kutoka damu ni dalili inayoashiria zaidi uwepo wa saratani ya endometrium au uterus. Inaweza pia kuwa ishara ya saratani ya uke au saratani ya shingo ya kizazi.

. Sexually transmitted diseases:
 Baadhi ya magonjwa, kama ya chlamydia na gonorrhea, yanaweza kusababisha kutoka matone ya damu na damu baada ya tendo la ndoa.

. Madawa:
 Kutoka damu mara nyingi ni madhara yanayotokana na matumizi ya madawa, kama dawa za hormone therapy, tamoxifen, na dawa za kuifanya damu kuwa nyepesi.


MATIBABU YA TATIZO LA KUTOKWA DAMU KIPINDI CHA KUKOMA HEDHI (POSTMENOPAUSE BLEEDING)

Matibabu ya tatizo hili hutegemea chanzo kilichosababisha mgonjwa kutokwa damu.
Hivyo matibabu hutolewa kama ifuatavyo
. Estrogen therapy: Homoni hii hutolewa ili kutibu kusinyaa kwa uke au utando wa juu ya nyumba ya uzazi (vaginal and endometrial atrophy.) Daktari anaweza kushauri matumizi ya:

. Vidonge vya kunywewa
. Cream ya ukeni: Kifaa maalumu kitatumika kuingiza cream hii mwilini
. Vaginal ring: Namna ya pete ambayo daktari ataiweka kwenye uke. Pete hii hutoa estrogen kwa miezi 3.
. Vaginal tablet: Utakiweka ukeni kutumia kifaa maalumu. Utatakiwa kuweka kila siku, au mara chache katika wiki.

. Progestin therapy: Hii ni namna ya progesterone iliyotengenezwa kwenye maabara inayotumika kutibu endometrial hyperplasia. Dakatri anaweza kukuandikia vidonge au sindano, cream ya ukeni , au kifaa cha kuweka kwenye nyumba ya uzazi.

. Hysteroscopy: Njia hii huweza kuondoa polyps. Madaktari huitumia kuondoa sehemu zilizovimba za utando wa nyumba ya uzazi kutokana na endometrial hyperplasia. Ataingiza hysteroscope kupitia uke na kupitisha vifaa vidogo vya upasuaji kupitia kijibomba.


. D&C (dilation and curettage): Katika upasuaji wa aina hii, madaktari huipanua cervix. Kisha hutumia kifaa chembamba kuondoa polyps au sehemu zilizotuna za uterus zilizosababishwa na endometrial hyperplasia.

. Hysterectomy: Upasuaji huu huondoa sehemu au tumbo lote la uzazi. Hii ni tiba kwa saratani ya endometrium au cervix. Wakati mwingine, daktari ataamua kuondoa ovari zako, mirija ya uzazi, au sehemu za karibu (lymph nodes).

. Radiation, chemotherapy, and hormone therapy: Unaweza kupewa tiba zaidi ya kansa baada ya upasuaji. Daktari ataamua cha kufanya kutokana na aina ya kansa uliyo nayo na ipo katika hatua gani.

. Madawa: Daktari anaweza kukuandikia dawa kama za antibiotics kwa magonjwa ya ngono. Dawa hizi zinaweza pia kutibu maambukizi kwenye cervix au tumbo la uzazi.

MAMBO YA KUZINGATIA ILI UEPUKANE NA MADHARA YA KIPINDI CHA KUKOMA HEDHI

Kuna mambo ya kuzingatia na  hatua za kuchukua ili mwanamke uliye kwenye postmepause ujisikie vizuri na kuwa mwenye afya nzuri.

. Epuka kuvuta sigara, kafeini (kiambato ndani ya kahawa na chai), pombe, chumvi nyingi, na sukari
. Kula mlo kamili (balanced diet)
. Tumia calcium kuweka imara mifupa yako na kuepukana na ugonjwa wa osteoporosis
. Tumia pia vitamini D kuimarisha mifupa
. Fanya mazoezi, kila siku, angalau dakika 30(zingatia swala la uzito)
. Tumia chakula chenye mafuta kidogo (low saturated fat and cholesterol.)

 MAMBO YA KUFANYA KUPUNGUZA HOT FLASHES

Hot flashes ni dalili inayojionyesha zaidi kwa mwanamke aliyekoma  hedhi. Mwanamke hupatwa na vipindi vya joto la ghafla, sehemu za juu za mwili likiambatana na jasho. Hapa chini ni vidokezi vya namna ya kukabiliana hali hiyo:

. Epuka kuvaa nguo nyingi na lala sehemu zenye ubaridi
. Epuka kula chakula cha moto na chenye viungo vingi
. Epuka kunywa pombe
. Punguza mawazo
. Kula chakula chenye soya


MAMBO YA KUFANYA KUPUNGUZA UKAVU UKENI 

. Mwanamke akikoma hedhi asilimia kubwa huwa wakavu ukeni hivyo tunawashauri kutumia vilainishi na vitu vya kuongeza unyevunyevu (moisturizers.)ukeni
. Mwombe daktari akuongoze kuhusu vitu vinavyoongeza estrogen.


MAMBO YA KUFANYA KUPUNGUZA TATIZO LA MIFUPA

Ili kuweza kuepukana na matatizo ya mifupa inashauriwa kutumia calcium na vitamini D ya kutosha Pamoja na kufanya mazoezi


YA MAMBO YA KUFANYA ILI KUPUNGUZA MATATIZO YA MAGONJWA YA MOYO 

Yamkini ya kupata magonjwa ya moyo huongezeka umri unapokuwa mkubwa,mambo muhimu ya kuzingatia kulinda moyo wako ni pamoja na:

. Chukua vipimo vya cholesterol na blood pressure kila wakati
. Chukua hatua za kupunguza cholesterol na kunguza blood pressure kama vimepanda.
. Kama una kisukari, iweke sawa sukari yako kila wakati
.udhibiti uzito wako

MATIBABU YA MATATIZO YA HEDHI NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo lolote linalohusu hedhi,uzazi na magonjwa mbalimbali na umejaribu njia  kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kuondoa matatizo mbalimbali ya  hedhi mbovu,matatizo ya uzazi,kutoka harufu mbaya ukeni na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

0 comments:

FAHAMU MATIBABU YA UGONJWA WA KUOTA VINYAMA/CHUNJUA/VIGWARU/MASUNDOSUNDO/WARTS SEHEMU ZA SIRI NA MAENEO MBALIMBALI KATIKA MWILI(WARTS & GENITALS WARTS)

FAHAMU MATIBABU NA AINA MBALIMBALI ZA CHUNJUA/VIGWARU/MASUNDOSUNDO/VINYAMA VINAVYOOTA SEHEMU MBALIMBALI KATIKA MWILI (WARTS&GENITALS WARTS)

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul
Mpendwa msomaji nina imani kuwa unaendelea vyema wewe na familia yako nami niko salama Sifa na utukufu tumrudishie Mwenyezimungu ambaye katujaalia neema ya uzima na tuwaombee wagonjwa waliopo majumbani ama hospitalini Mwenyezimungu awape nafuu ya maradhi yao na wenye shida pia watatuliwe shida zao Ameen!

Nimepokea emals nyingi week hii za watu wenye matatizo ya kuota vinyama juu ya ngozi(chunjua/vigwaru/masundosundo/warts)
kwa muda mrefu tatizo hili limekua linasumbua vichwa vya madaktar na wagonjwa wengi kiujumla.
Nimeamua kulielezea tatizo hili kwa kina ili kila mmoja afahamu ugonjwa huu na namna ya kuepukana nao pia jinsi ya kupata matibabu


Chunjua/masundosundo/vigwaru ni ugonjwa wa kutokewa na vioteo/viuvimbe au vinyama vidogovidogo juu ya ngozi unaosababishwa na kirusi aitwaye human papillomavirus (HPV). Mathalani Kuna aina tofauti zaidi ya 150 za human papiloma viruses.
Aina nyingine ya kirusi huyu hushambulia sehemu za siri na sehemu za mdomo na kujenga uvimbe mkubwa , ambao mara nyingine huendelea na kuwa saratani.
Pia zipo aina nyingine za virus wa HPV hushambulia ngozi na kujenga uvimbe ambao hauhusishwi na saratani. Pamoja na kuwa chunjua huambukiza, si ajabu kuona kuwa mtu mmoja tu ndani ya familia ndiye aliyeathirika. Vile vile chunjua hushambulia sehemu moja tu ya mwili (kama vile mikono au miguu), ingawa huweza kuenea hadi sehemu nyingine za mwili. Aina ya chunjua inayotokea huendana na aina ya kirusi wa chunjua na kiungo kilichoshambuliwa. Kwa mfano, kirusi wa aina moja huweza kusababisha chunjua za aina ya ‘common warts’ kwenye mikono na vile vile akasababisha chunjua za aina ya plantar.


Virusi vya HPV(Human papiloma viruses)vimethibitika kuwa ni chanzo katika kukua kwa kansa za viungo vya uzazi kama kansa ya shingo ya kizazi na kansa za mkundu.
 HPV vile vile wamehusishwa na ukuaji wa kansa za kichwa na shingo zinazoanzia kwenye findo (tonsils).

Wapo pia virusi wa HPV wasio na madhara makubwa sana wenyewe huleta uvimbe sehemu za siri, genital warts. Wengine hushambulia ngozi na kuleta warts sehem mbalimbali za mwili.
Halikadhalikla kuna virus vya HPV wanaosababisha uvimbe kwenye viungo vya sauti (vocal cords).
Mathalani aina za chunjua zinazoonekana kwa wingi ni common warts, flat warts, plantar warts, periungual warts, filiform warts na genital warts.
Hapa chini tutaona aina hizo za warts na matibabu Yake.

CHUNJUA AINA YA FLAT WARTS

Flat warts ni viuvimbe/vigwaru/chunjua/warts/vinyama vinavyotokea juu ya ngozi iliyo laini, bapa, wenye rangi ya ngozi au kahawia ya
njano wenye ukubwa wa ncha ya sindano.
Mara nyingi hupatikana usoni, maeneo ya nyuma ya mikono au miguu na huwa kwenye kikundi cha chunjua 20 hadi 200 kwa pamoja. Chunjua hizi huwapata zaidi watoto wadogo na vijana. Flat warts husababishwa na kirusi ambaye anaambukiza, lakini asiye na madhara wala maumivu.

Pia Flat warts huingia kupitia majeraha ya kwenye ngozi. Wanaume hupata chunjua hizi baada ya kunyoa ndevu, wakati wanawake huwa na chunjua hizi miguuni.

Kama ilivyo kwa chunjua za aina nyingine, husababishwa na human papillomavirus (HPV). Flat warts husababishwa na HPV wa koo za 3, 10, 28 na 49. HPV hawa hawana madhara, tofauti na wengine, kama genital warts, wanaosababisha saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake. Flat warts wanaweza kuenezwa kwa kugusana na ngozi yenye chunjua au kutumia taulo au chombo ambacho kimetumika na mwathirika. Unaweza pia kueneza chunjua hizi kutoka sehemu moja ya mwili wako hadi nyingine.

Flat warts kwa kawaida huondoka zenyewe bila kuhitaji tiba. Unaweza kupata tiba ili kupona haraka zaidi. Daktari anaweza kukuandikia cream, lakini cream hizi huchubua ngozi ili kuondoa chunjua. Cream hizi ni kama:

. retinoic acid 0.05 percent cream
. Imiquimod 5 percent cream (Aldara, Zyclara)
. Topical 5-fluorouracil (Carac, Efudex, Fluoroplex, Tolak), 1 percent or 5 percent cream

Daktari anaweza pia kukuandikia 5 percent benzoyl-peroxide (Del Aqua, NeoBenz Micro, au Clearskin, EFFACLAR). 

CHUNJUA AINA YA PLANTAR WARTS

Plantar warts ni vijiuvimbe/vigwaru/warts/vijinyama vidogo vinavyotokea kwenye kisigino au sehemu ambazo zinabeba uzito za kwenye mguu. Mgandamizo kwenye maeneo hayo kunaweza kusababisha plantar warts kuota kuelekea ndani, chini ya tabaka nene la ngozi (callus).
Plantar warts husababishwa na HPV. Kirusi huyu huingia mwilini kupitia sehemu ndogo ulizojikata, au sehemu nyingine dhaifu za maeneo ya chini ya mguu.

Plantar warts nyingine hazihatarishi afya na hujiondokea zenyewe baada ya muda bila tiba yoyote.

Plantar warts zinasababishwa na HPV anapoingia kwenye tabaka la juu la ngozi ya kwenye unyayo kupitia vijijeraha vidogo au maeneo mengine yaliyo dhaifu yaliyo maeneo ya chini ya mguu.

HPV hupatikana kwa wingi, na kuna aina tofauti zaidi ya 100 ya kirusi huyu. Lakini ni aina chache tu ambazo zinaweza kuleta chunjua kwenye mguu. Aina nyingine zinaweza kuleta chunjua kwenye maeneo mengine ya ngozi au kwenye utando telezi.

Kila mtu ana kinga zake za mwili zenye uwezo tofauti wa kupambana na HPV. Si kila mtu atakayegusana na kirusi huyu atapata chunjua. Hata watu wa familia moja watahimili kirusi huyu kwa viwango tofauti.

HPV wanaoeneza plantar warts hawaambukizi kirahisi. Kwa hiyo chunjua hizi haziambukizi kwa kugusana. Lakini wanapenda kuishi kwenye mazingira ya vuguvugu, yenye unyevu. Kwa hiyo unawea kumpata kirusi huyu kwa kutembea peku kwenye mabwawa ya kuogelea. Kirusi akipenya sehemu moja, anaweza kuenea hadi maeneo mengine na kusababisha chunjua.

CHUNJUA AINA YA PERIUNGUAL WARTS


Chunjua za aina hii ya periungual warts hutokea kwa kujifunzajenga kuzunguka kucha za vidoleni au kwenye dole gumba. Zikikua huweza kukukosesha raha au kuleta maumivu na huweza kuathiri ukuaji wa kucha. Watoto na vijana wa umri wa balehe wana nafasi kubwa zaidi ya kupata periungual warts na hasa kama wana tabia ya kung’ata kucha zao.

Periungual warts huwa ndogo sana mwanzoni, ukubwa wa ncha ya sindano, zikiwa laini na za kung’aa. Katika wiki au miezi michache, huweza kufikia ukubwa wa njegere zikiwa na umbo la kaliflawa.

Periungual warts huweza kuwa na rangi ya kahawia, kujivu, au nyeusi. Baadaye hujijenga na kuwa nyingi kwa pamoja. Zikiwa kubwa huweza kuleta maumivu.

Periungual warts huletwa na baadhi ya koo za human papillomavirus (HPV). Kirusi  huyu huambukiza kupitia kugusana na mtu mwenye ugonjwa huu au kupitia mataulo. Kirusi huyu hupitia sehem zenye majeraha, na hii ndiyo sababu watu wanaopenda kutafuna kucha zao huwa kwenye hatari zaidi. Watu wenye upungufu wa kinga za mwili au wenye magonjwa ya ngozi nao huathirika kirahisi zaidi.

CHUNJUA AINA YA COMMON WARTS

Common warts ni chunjua ndogo zinazojengwa na uvimbe wa chambechembe ndogo za ngozi ambazo mara nyingi hutokea kwenye vidole au mikono. Chunjua hizi ambazo hukwaruza ziguswapo, mara nyingine huja kama vijidoa vyeusi, ambavyo ni mishipa midogo ya damu yenye damu iliyovia.

Common warts husababishwa na kirusi anayeenezwa kwa kugusana. Inaweza ikachukua miezi 2 hadi 6 chunjua kuanza kujijenga baada ya kugusa kitu chenye kirusi huyu. Chunjua hizi hazina madhara makubwa na baadaye hupotea zenyewe. Watu walio wengi huamua kuziondoa kwa sababu huona kama ni bughudha kwao.

Common warts kwa kawaida hutokea kwenye vidole au mikono na huwa:

Kama uvimbe mdogo uliojengwa kwa chembechembe ndogo za nyama
Zenye rangi ya nyama, nyeupe, pinki au hudhurungi
Zenye mikwaruzo zikiguswa
Zenye alama nyeusi zilizojitawanya, ambazo ni mishipa midogo ya damu.

Pia Common warts husababishwa na human papillomavirus (HPV). Kirusi huyu anapatikana kwa wingi sana na kuna aina tofauti zaidi ya 150 za kirusi huyu, lakini ni aina chache sana zinazoweza kuleta chunjua kwenye mikono. Aina nyingine za HPV hupatikana kwa kushiriki ngono. Aina nyingi zaidi hupatikana kwa kugusana ngozi au kuchangia vitu , kama taulo au vifaa vya kujioshea. Kirusi huingia mwilini kupitia michubuko kwenye ngozi. Kukata kucha kwa meno kwa weza kusababisha kusambaa kwa kirusi huyu kwenye ncha za vidole au kuzunguka kucha.
zaidi.

CHUNJUA AINA YA FILIFORM WARTS


Chunjua za aina hii zina mwonekano wa tofauti kabisa na nyingine. Filiform warts ni  michomozo mirefu myembamba yenye urefu wa kati ya milimeta 1 hadi 2 juu ya ngozi. Zinaweza kuwa na rangi ya njano, kahawia au rangi ya ngozi, na haijijengi kwa vikundi. Kwa vile hupenda kutokea kwenye kope au mdomoni, chunjui hizi huitwa pia facial warts. Chunjua hizi huweza kutokea pia kwenye shingo, kwenye vidole na miguuni. Zinaweza kusambaa kwa haraka sana kwenye sehemu nyingine za mwili.

Filiform warts husababishwa na human papillomavirus (HPV), ambaye huambukiza. Anaweza kuambukizwa kwa kugusana ngozi, na hasa kama kuna jeraha kwenye ngozi. Pamoja na kuwa haziwezi kusababisha saratani, huwa ni bughudha.


Dalili Za chunjua za filiform warts

Kwa kawaida chujua za filiform hazina maumivu na hazina dalili zo zote. Chunjua hizi hutambulika kwa macho. Dalili zinaweza kuonekana kama chunjua zitaota sehemu za ngozi zenye mikunjo. Na dalili zaweza kuwa:

. Kuwasha
. Kutoka damu
. Maumivu

Chanzo Cha Chunjua Za Filiform

Filiform warts husababishwa na HPV. Kuna aina tofauti zaidi ya 100 za HPV. HPV wa ukoo 1,2,4,27 na 27 ndiyo wanaojulikana kusababisha chunjua za filiform.

Tiba Ya Filiform Warts

Tiba nyingi zinalenga kuondoa chunjua, lakini hazimwondoi kirusi. Hakuna dawa ya HPV kwa sasa hivi, ispokuwa sindano ambazo zinalenga baadhi ya koo za HPV. Hadi sasa hakuna sindano kwa ajili ya filiform warts.

Kwa walio wengi, filiform warts huondoka zenyewe baada ya muda kwa msaada wa kinga zao za mwili.

CHUNJUA AINA YA GENITALS WARTS

Genital warts ni viuvimbe/vigwaru/chunjua/ vinyama vidogovidogo vinavyotokea sehemu za siri.
Chunjua hizi huenezwa sana kwa njia ya ngono.
Karibu watu wote wanaofanya mapenzi wamepata kuambukizwa na angalau aina moja ya human papillomavirus (HPV), kirusi anayeeneza genital warts, katika maisha yao. Wanawake kwa namna fulani wanakuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata chunjua za sehemu za siri.
Genital warts hushambulia maeneo yenye unyevunyevu sehemu za siri. Chunjua hizi huweza kuonekana kama vijiumbile vidogo vya nyama au vikawa na umbo kama la koliflawa. Mara nyingi genital warts ni ndogo mno kuonekana kwa macho na wakati wengine hutokewa kubwa zenye kuonekana kwa urahisi

Kama ilivyo kwa chunjua za aina nyingine, genital warts husababishwa na human papilloma virus (HPV). Koo nyingine za HPV husababisha genital warts, wakati nyingine huleta saratani. Sindano zinaweza kusaidia kujikinga na baadhi ya koo za genital HPV.

Chanzo Cha Genital Warts

Genital warts au chunjua za sehemu za siri husababishwa na human papilloma virus. Kuna koo tofauti zaidi ya 40 zinazoshambulia sehemu za siri. Genital warts huenezwa kwa kufanya tendo la ndoa. Wakati mara nyingine kinga zako za mwili huua virusi hawa na hupati athari zozote.


Madhara Yatokanayo Na Genital Warts

. Saratani
Saratani ya shingo ya kizazi inahusishwa sana na maambukizi ya genital HPV. Aina nyingine za genital warts zinahusishwa na kansa ya sehemu za nje ya uke, saratani ya kwenye mkundu, saratani ya dhakari, na saratani za mdomo na koo. Si kweli kwamba maambukizi yote ya HPV yanaleta saratani.

. Matatizo wakati wa ujauzito
Genital warts huweza kuleta matatizo wakati wa ujauzito. Chunjua hizi huweza kukua na kuwa kubwa kiasi cha kuziba mkojo usitoke vizuri. Chunjua hizi za kwenye kuta za uke huweza kupunguza mnyumbuko wa tishu za uke wakati wa kuzaa. Chunjua kubwa za nje ya uke au ndani ya uke zinaweza kutoa damu zikipanuliwa wakati wa kuzaa.

Yaweza tokea mara chache sana kwamba kichanga cha mama mwenye chunjua za ukeni kikawa na chunjua kwenye koo lake ambapo upasuaji utahitajika kuhakikisha njia zake za hewa hazijazibwa.


Matibabu
Hospitali kuna tiba nyingi zinazotumika, lakini hakuna yenye uhakika wa asilimia 100 katika kuondoa chunjua za sehemu za siri na kuzizuia zisirudie tana. Genital warts huweza kuondoka zenyewe kutoka asilima 10 hadi 20 ya watu walioathirika katika kipindi cha miezi 3 hadi 4.

. Cryotherapy: Njia hii hugandisha chunjua kwa kutumia naitrojeni ya maji (liquid nitrogen). Ni njia bora sana kwa sababu imetoa matokea mengi mazuri ikiwa na side effects chache sana.

. Laser treatment: Njia hii hutumika kwa chunjua za sehemu za siri zilizoenea au zinazojirudirudia. Mionzi ya laser huharibu kabisa uvimbe  uliotokana na HPV. Dosari ni bei yake kubwa, muda mrefu wa tiba, na kuacha makovu.

. Elecrodesiccation: Njia hii hutumia peni ya umeme kuua chunjua.

Dawa zinazotumika kutibu genitals warts

Kuna dawa kadhaa zinazotumika kutibu chunjua za sehemu za siri na unaweza kuzitumia kama mbadala wa tiba nyingine.

. Podophyllum resin ni dawa inayotolewa na mtaalamu wa tiba
. Podofilox (Condylox) ni dawa unayoweza kuitumia nyumbani na ina uwezo mkubwa wa kutibu kuliko podophyllum resin. Dawa hii pia hutumika kwa kinga.
. Trichloroacetic acid au bichloroacetic acid haina uhakika sana na chunjua huweza kurudi, inaweza kusababisha maumivu na kujisikia kama unaungua.
. 5-Fluorouracil (Efudex) hutumika kama cream, huchukua muda mrefu kutibu, na ina madhara mengine mengi ya kiafya.
. Interferon alpha -n3 (Alferon N) ni sindano inayotumika kwa chunjua ambazo hazisikii dawa nyingine, lakini ina madhara mengine mengi.
. Imiquimod (Aldara) hutumika kama cream na maumivu wakati ukipaka hutokea.

MATIBABU YA UGONJWA WA CHUNJUA/VIGWARU/MASUNDOSUNDO/VINYAMA VINAVYOOTA SEHEMU MBALIMBALI KATIKA MWILI(WARTS & GENITALS WARTS)CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo hili la kutokewa na chunjua/vinyama vidogovidogo vinavyotokea katika ngozi (warts/genitals warts) na umeshafanya matibabu kadhaa ila bado hujapata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam 
Tutakufanyia uchunguzi wa kujua ni aina gani ya chunjua ulizonazo pia tutakupatia dawa stahiki zenye uwezo wa kukuponya pasipo kukuunguza
Pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kuondoa tatizo la vinyama sehemu mbalimbali katika mwili,tatizo la hedhi mbovu,matatizo ya uzazi,kutoka harufu mbaya ukeni na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

0 comments:

FAHAMU CHANZO NA MATIBABU YA TATIZO LA MAUMIVU KABLA YA HEDHI(PREMENSTRUAL SYNDROME )NA MAUMIVU YANAYOTOKEA KIPINDI CHA HEDHI(DYSMENORRHEA)

FAHAMU CHANZO CHA MAUMIVU KABLA YA HEDHI (PREMENSTRUAL SYNDROME) NA MAUMIVU YANAYOTOKEA KIPINDI CHA HEDHI(DYSMENORRHEA)



Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul
Nina imani sote tuko salama Ashukuriwe Mwenyezimungu kwa kutupa pumzi
Wiki iliyopita tulijadili tatizo la kukosa  hedhi kwa muda,leo Katika mfululizo wa mada zetu,tutazungumzia matatizo yanayoambatana na hedhi. Wanawake wengi hupata matatizo kabla ya kuanza hedhi, wakati wa hedhi na mara ya baada ya kukoma hedhi.
 Katika kila moja ya hayo, tutajaribu kuona sababau za tatizo na jinsi ya kuepuka tatizo hilo.
Tunaanza kwa kulitazama tatizo la kupata maumivu kabla ya hedhi (Premenstrual syndrome).

MAUMIVU KABLA YA HEDHI(PREMENSTRUAL SYNDROMES)

Ni hali ambayo humwathiri mwanamke kihisia, afya yake na mwili na tabia yake katika kipindi fulani cha mzunguko wake wa hedhi, kwa kawaida kabla tu ya kuingia mwezini. Tatizo hili ni la kawaida kwa wanawake na huathiri karibu asilimia 85 ya wanawake wanaopata hedhi. Maumivu huanza siku 5 hadi 11 kabla ya kuanza hedhi.

Kuna mlolongo wa dalili za tatizo hili la maunmivu kabla ya hedhi, lakini mwanamke anaweza kupata baadhi ya dalili zifuatazo:

Dalili Za Kihisia Na Kitabia

shida za hedhi
. Kuwa na msongo wa mawazo au wasiwasi
. Kuwa na mfadhaiko
. Kulialia
. Madadiliko ya mara kwa mara ya kihisia na hasira
. Mabadiliko ya ulaji na kupenda sana kula
. Matatizo ya kupata usingizi
. Kujitenga na jamii
. Kushindwa kutuliza mawazo



Dalili Na Mabadiliko Katika Maumbile ya Mwili


. Maumivu kwenye maungio ya mifupa na misuli
. Kuumwa kichwa
. Uchovu
. Kunenepa
. Maumivu kwa mbali maziwa yakiguswa
. Kuchipuka kwa chunusi
. Kukosa choo au kuharisha

Kwa baadhi ya wanawake, mabadiliko haya ya kitabia na maumivu ya mwili yanaweza kuwa makubwa kiasi cha kuathiri shuguli zao. Pamoja na kuwa wengine huathirika sana, matatizo haya huisha ndani ya siku nne baada ya kuanza hedhi.

Kwa wanawake wachache, maumivu haya ya kabla ya hedhi huwafanya washindwe kabisa kuendelea na shughuli zao za kila siku, na huwatokea kila mwezi. Aina hii ya PMS huitwa premenstrual dysphoric disorder (PMDD).

Dalili za premenstrual dysphoric disorder ni pamoja na mfadhaiko, hisia za ghafla zinazobadilika, hasira, wasiwasi, kushindwa kufikiri, hasira za ghafla na kuwa na msongo wa mawazo.


CHANZO CHA MAUMIVU KABLA YA HEDHI (PREMENSTRUAL SYNDROME)


Chanzo kamili cha tatizo la kupata maumivu kabla ya hedhi hakijathibitika, lakini sababu zifuatazo zimeonyesha kuwa na mchango mkubwa:

. Mabadiliko Katika Mzunguko Wa Homoni. Dalili za maumivu kabla ya hedhi zinabadilika na mabadiliko ya homoni katika mzunguko wa hedhi. Viwango vya homoni ya estrogen na progesterone huongezeka wakati fulani katika mwezi. Mwongezeko huu husababisha mabadiliko ya mara kwa mara ya namna mwanamke atakavyojisikia, kuleta wasiwasi na kusababisha hasira za haraka.

. Mabadiliko ya viwango vya kemikali katika ubongo. Mabadiliko katika viwango vya serotinin katika ubongo vinaaminika kusababisha premenstrual syndrome. Viwango vya Serotinin huathiri namna mwanamke atakavyojisikia. Serotinin ni kemikali katika ubongo inayoamsha namna ya kujisikia, hisia na mawazo. Kuwa na kiwango kidogo cha serotinin kunasababisha mfadahiko, uchovu, kupenda kula sana na kukosa usingizi.

. Mfadhaiko. Wanawake wengine waliobanika kuwa na matatizo mazito ya maumivu kabla ya hedhi, walikuwa na mfadhaiko, ingawa mfadhaiko huo haukuwa sababu ya matatizo yao yote.

Mambo Ya Kufanya Kupunguza Maumivu Ya Kabla Ya Hedhi

Mpendwa msomaji unaweza kuondokana au kupunguza makali ya tatizo la maumivu kabla ya hedhi kwa kufanya mabadiliko katika namna ya kula, kufanya mazoezi na namna unavyoishi kwa ujumla. Unaweza kujaribu yafuatayo:

Badili Namna Ya Kula

. Punguza mlo, kula mara nyingi zaidi kuzuia tumbo kuvimba na hali ya kujisikia tumbo limejaa

. Punguza chumvi na chakula chenye chumvi nyingi kuzuia tumbo kujaa
. Chagua chakula chenye complex carbohydrates, kama matunda, mboga za majani na nafaka nzima

. Chagua chakula chenye uwingi wa calcium
. Jizuie kutumia kahawa na pombe

Jipangie Ratiba Ya Mazoezi Ya Mwili

Panga ratiba ya kutembea angalau kwa dakika 30, kuendesha baiskeli, kuogelea au mazoezi mengine ya kukutoa jasho siku kadhaa kwa wiki. Mazoezi ya kila  siku yataboresha afya yako na kukuondolea baadhi ya dalili, kama uchovu na mfadhaiko.

Punguza Msongo Wa Mawazo

. Pata usingizi wa kutosha
. Fanya mazoezi ya misuli au upumuaji mzito ili kuondoa maumivu ya kichwa, wasiwasi na matatizo ya kukosa usingizi
. Jaribu kufanya yoga au massage ili kuondoa msongo wa mawazo.

TIBA YA MAUMIVU KABLA YA HEDHI


Kwa wanawake walio wengi, kubadli mtindo wa maisha kunaweza kuwasaidia kuondokana na PMS. Kulingana na ukubwa wa tatizo, daktari anaweza kukuandikia dawa moja au zaidi ya dawa za kusaidia PMS. Utendaji kazi na msaada wa dawa hizi hutofautiana kutoka mwanamke mmoja hadi mwingine. Dawa ambazo hutolewa ni pamoja na:

. Antidepressants
. Nonsteroidal anti-inflammatory drugs (NSAIDs)
. Diuretics

Tiba Mbadala Ya Maumivu Kabla Ya Hedhi
Kuna vitu vinafahamika kuondoa au kupunguza makali ya tatizo la maumivu kabla ya hadhi:

. Calcium. Kupata calcium ya kutosha katika mlo au matumizi ya vidonge vya calcium kunaweza kuondoa dalili za maumivu kabla ya hedhi – premenstrual syndrome.
. Magnesium. Kutumia magnesium kila siku kutasaidia kuondoa maumivu ya kwenye maziwa na kujaa kwa tumbo kunakoambatana na premenstrual syndrome.

. Vitamin E. Matumizi ya vitamini E ya kila siku yanaweza kuondoa PMS kwa kuzuia utengenezaji wa prostaglandins, namna ya homoni inayosababisha mkakamao wa misuli na maumivu kwenye maziwa.

. Tiba ya mimea. Baadhi ya wanawake wameeleza kupata nafuu ya PMS kwa kutumia mimea kama ginkgo, tangawizi, chasteberry na mingine ingawa njia hii haijathibitishwa na vyombo vya kusimamia chakula na dawa.

Mpendwa msomaji hapo juu tumeona Maumivu yanayotokea kabla ya hedhi hivi sasa tutazungumzia maumivu wakati wa hedhi ambayo huitwa menstrual cramps au kitaalamu Dysmenorrhea.

MAUMIVU YANAYOTOKEA KIPINDI CHA HEDHI (MENSTRUAL CRAMPS/DYSMENORRHEA)

 ni maumivu ya kukakamaa kwa misuli ya eneo la chini ya tumbo. Wanawake wengi hupata maumivu haya kabla kidogo au wakati wakiwa kwenye siku zao. Kwa baadhi ya wanawake, maumivu haya huwa ni ya kuwakosesha raha. Kwa wengine, huwa ni makubwa kiasi cha kuwafanya washindwe kuendelea na shughuli zao za kila siku kwa siku kadhaa kila mwezi.
Maumivu haya yamegawanyika katika makundi mawili nayo ni  yafuatayo ;

Primary dysmenorrhea ni maumivu ya wakati wa hedhi ambayo hujirudiarudia kila mwezi na ambayo hayatokani na magonjwa mengine ya mwili. Maumivu haya ya wakati wa hedhi ambayo hayana sababu za kueleweka, hupungua kadri mwanamke anavyozidi kuwa na umri mkubwa na mara nyingi hupungua sana mara baada ya kuzaa.

Secondary dysmenorrhea ni maumivu ya wakati wa siku za mwanamke ambayo yanatokana na dosari katika viungo vya uzazi vya mwanamke, kama endometriosis, adenomysis, uterine fibroids au maambukizi ya wadudu.

CHANZO CHA MAUMIVU YANAYOTOKEA KIPINDI CHA HEDHI(DYSMENORRHEA)


Wakati wa hedhi, nyumba ya uzazi hujiminya ili kuondoa utando wake wa juu. Vitu vilivyo mfano wa homoni – prostaglandins – vinavyohusika na maumivu na uvimbe, huchagiza kujiminya kwa misuli ya nyumba ya uzazi (uterus). Uwepo wa prostaglandins kwa wingi kunahusishwa na maumivu makali ya hedhi.
Kujiminya kwa misuli yangu uterus kukiwa kwa kiwango kikubwa mno, kunaweza kuziba mishipa ya damu inayoilisha nyumba ya uzazi (uterus). Maumivu yatokanayo yanaweza kulinganishwa na maumivu ya kifuani wakati mishipa ya damu ikiziba na kusababisha baadhi ya sehemu za moyo kukosa chakula na oksijeni.
Maumivu ya wakati wa hedhi yanaweza pia kusababishwa na:
. Endometriosis. Hii ni hali ambapo tishu ambazo kwa kawaida hujenga ndani ya uterus, zinajenga nje , hasa kwenye mirija ya uzazi (fallopian tubes), kwenye ovari au juu ya tishu zinazofunika pelvis.
. Uterine fibroids. Uvimbe usio wa saratani juu ya ngozi ya nyumba ya uzazi waweza kuleta maumivu.
. Adenomyosis. Hali hii ni pale tishu zinazofunika uterus zinapojijenga kwenye misuli ya kuta za uterus.
. Pelvic inflammatory disease (PID). Maambukizi kupitia ngono ya bakteria kwenye viungo vya uzazi vya mwanamke.
. Cervical stenosis. Baadhi ya wanawake wana vijitundu vidogo mno vya kwenye cervix vinavyozuia mtiririko wa damu wakati wa hedhi na kusababisha maumivu kutokana na msukumo wa ndani ya nyumba ya uzazi.

Dalili Za Maumivu Ya Hedhi (Menstrual Cramps)

. Maumivu ya kukakamaa kwa misuli sehemu ya chini ya tumbo yanayoweza kuwa makali
. Kichwa kizito na maumivu ya kichwa endelevu
. Maumivu yanayoenea sehemu za mgongoni na kwenye mapaja
Wanawake wengine hupata:
. Kichefuchefu
. Haja kubwa mara kwa mara
. Maumivu ya kichwa
   Kizunguzungu

Tiba Ya Maumivu Ya Hedhi

Maumivu ya wakati wa hedhi yana tiba tofauti. Daktari anaweza kukupa:
. Dawa za kupunguza maumivu.
Daktari anaweza kukushauri kutumia dawa za kupunguza maumivu unapoanza siku zako au mara unapoanza kusikia dalili za maumivu na kuendelea kuzitumia dawa hizo kwa siku 2 au 3, hadi dalili zinapoondoka.
. Hormonal birth control. Vidonge vya kunywa vya uzazi wa mpango vina homoni inayozuia upevushwaji wa yai na kuondoa maumivu ya hedhi. Homoni hizi zinaweza kutolewa kwa njia nyingine kama sindano, kitu cha kuvaa juu ya ngozi, kitu kinachowekwa chini ya ngozi ya mkono au namna ya pete laini inayoingizwa ukeni.
. Upasuaji. Kama matatizo yako yanasababishwa na kitu kinachoeleweka kama endometriosis au fibroids, upasuaji unaweza kuondoa matatizo ya maumivu ya hedhi. Upasuaji kuondoa nyumba ya uzazi (uterus) unaweza kuwa ni chaguo endapo hufikirii kuendelea kuzaa.

Mambo Ya Kufanya Kuondoa Maumivu Ya Wakati Wa Hedhi

Unaweza kufanya yafuatayo kujaribu kuondoa au kupunguza maumivu ya wakati wa hedhi:
. Mazoezi. Utafiti umeonyesha kuwa mazoezi ya mwili yanapunguza maumivu ya hedhi.
. Joto. Kutumbukia kwenye bafu la maji ya moto au kutumia chombo cha kupasha moto sehemu za chini ya tumbo kunaweza kupunguza maumivu ya wakati wa hedhi. Upashaji huu wa moto sehemu za tumboni unaweza kufanya kazi vizuri sawa na kutumia dawa za kuondoa maumivu haya.
. Chakula. Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa matumizi ya vitamini E, omega-3 fatty acids, vitamini B-1 (thiamine), vitamini B-6) na magnesium yanaweza kuondoa maumivu ya wakati wa hedhi.

. Kuacha pombe na tumbaku. Vitu hivi vinaweza kuongeza makali ya maumivu ya wakati wa hedhi.
. Kupunguza msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo unaweza kuongeza uwezekano wa kupata maumivu ya hedhi au kuongeza makali ya maumivu hayo.

MATIBABU YA MATATIZO YA MAUMIVU YA HEDHI NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo lolote linalohusu hedhi,uzazi na magonjwa mbalimbali na umejaribu njia hizo kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kuondoa tatizo la  hedhi mbovu,matatizo ya uzazi,kutoka harufu mbaya ukeni na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

0 comments:

FAHAMU CHANZO CHA TATIZO LA MWANAMKE KUKOSA HEDHI KWA MUDA MREFU, DALILI NA MATIBABU YAKE(AMENORRHEA)


CHANZO CHA MWANAMKE KUKOSA HEDHI KWA MUDA MREFU NA MATIBABU YAKE (AMENORRHEA)



Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul nina imani wewe ndugu yangu msomaji wa makala hii unaendelea vyema nami nakuombea MWENYEZIMUNGU akujaze afya iliyo njema zaidi na baraka katika maisha yako

Katika mfululizo wa mada zetu za mzunguko wa hedhi wiki iliyopita tulijadili maana ya mzunguko wa hedhi na jinsi ya kujua siku za hatari
 leo tutajadili tatizo la kukosa hedhi kwa muda mrefu ambapo kitaalamu huwa tunaita amenorrhea.
Mwanamke anakuwa na tatizo hilo pale ambapo anakosa hedhi kwa kipindi cha miezi mitatu mfululizo, au msichana ambaye hajaanza kupata hedhi akiwa na umri wa miaka 15.

Sababu ya kawaida ya kukosa hedhi ni ujauzito. Sababu nyingine ya kukosa hedhi ni dosari katika viungo vinavyojenga mfumo wa uzazi au tezi zinazosaidia kudhibiti viwango vya homoni katika mwili. Tiba ya chanzo cha tatizo mara nyingi huondoa tatizo hili la mwanamke kukosa hedhi.

Amenorrhea hugawanywa katika aina mbili ambazo ni  Primary amenorrhea na Secondary Amnorrhea

. Primary amenorrhea ni kukosekana kwa hedhi na mabadiliko ya kijinsia (kama kuota maziwa na kuota mavuzi) kwa msichana wa miaka 14 au kukosekana kwa hedhi kukiwa na mabadiliko ya kijinsia kwa msichana wa miaka 16.

. Secondary amenorrhea ni kukosekana kwa hedhi kwa mwanamke ambaye awali alikuwa anapata hedhi lakini baadaye akasimama kwa miezi 3 au zaidi bila ya kuwa na ujauzito, bila ya kuwa na maziwa ya kunyonyesha, bila kuzuia mzunguko wa wa hedhi kwa vidonge, au kukoma hedhi.

Ili mwanamke awe na mzunguko wa hedhi mzuri, hypothalamus, tezi ya pituitary, ovari, na uterus vyote vinatakiwa vifanye kazi ipaswavyo. Hypothalamus huiamuru tezi ya pituitary kutoa homoni za follicle-stimulating (FSH) na luteinizing (LH). FSK na LH husababisha ovari kutoa homoni za estrogen na progesterone. Estrogen na progesterone zinahusika katika mzunguko wa mabadiliko katika endometrium (utando unaofunika uterus), pamoja na hedhi. pamoja na hayo yote, mkondo wa uke lazima uwe wazi ili kuruhusu damu ya hedhi.


 VISABABISHI VYA KUKOSA HEDHI KWA MUDA MREFU(AMENORRHEA)


Amenorrhea inaweza kutokea kwa sababu nyingi. Baadhi zikiwa ni za kawaida katika maisha ya mwanamke, wakati nyingine zikisababishwa na matumizi ya madawa au zikiwa ni ishara ya tatizo la kiafya. Tatizo la kukosa hedhi linaweza kusababishwa na dosari yo yote kwenye hypothalamus, pituitary, ovari, mkondo wa uke au ya kiutendaji kimwili.

Sababu za kawaida

. Ujauzito
. Kunyonyesha
. Kukoma hedhi

Dawa za Kuzuia Mimba

Wanawake wengine wakitumia vidonge vya kuzuia mimba hukosa hedhi. Hata baada ya kuacha matumizi ya vidonge hivyo, huwachukua muda miili yao kurudi kwenye hali za kawaida na kuanza kuona hedhi zao. Njia za sindano au kupandikiza zaweza pia kuleta tatizo la kukosa hedhi.

Mitindo Ya Maisha

Baadhi ya mitindo ya maisha huweza kuchangia mwanamke kukosa hedhi. Kwa mfano:

. Kuwa na uzito mdogo sana. Kuwa na uzito mdogo kupita kiasi – asilimia 10 chini ya uzito wa kawaida – husimamisha shughuli nyingi za homoni ndani ya mwili, hivyo kusimamisha uzalishaji wa mayai

. Mazoezi zaidi ya kawaida. Wanawake wanaoshiriki shughuli zinazodai mazoezi ya juu, hujikuta wakipoteza hedhi zao. Baadhi ya sababu zinachangia kwa wanariadha, ikiwa ni pamoja na uzito mdogo, kuwa na mafuta kidogo ndani ya mwili, msongo wa mawazo na matumizi makubwa ya nishati ya mwili.

. Msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo huweza kubadilisha kwa muda utendaji kazi wa hypothalamus – sehemu ya ubongo inayosimamia homoni zinazoratibu hedhi. Uzalishaji wa mayai na hedhi, hivyo vyaweza kusimama. Hedhi za kawaida hurudi baada ya msomgo wa mawazo kupungua.

Kukosa Uwiano Wa Homoni

Matatizo kadhaa katika viungo vya mwili huweza kuvuruga mpangilio wa homoni katika mwili, ikiwa ni pamoja na:


Sababu Zinazotokana Na Hypothalamus
. Uvimbe karibu na tezi ya pituitary (Craniopharyngioma)
. Kallman syndrome (upungufu wa gonadotropins, homoni zenye uwezo wa kusimamia ukuaji na ufanyaji kazi wa viungo vya uzazi )
. Upungufu wa lishe
. Uzito mdogo au kuchelewa kukua

Sababu Za Tezi Ya Pituitary
. Uwingi wa homoni ya prolactin, homoni inayosimamia utoaji wa maziwa wakati mama ananyonyesha, katika damu. Hali hii kitaalamu huitwa prolactilemia na husababishwa na uvimbe (prolactinoma) katika tezi ya pituitary.

. Dosari zinazoanzia kwenye uvimbe wa aina nyingine wa kwenye pituitary (kama, cushing syndrome, acromegaly, au thyroid-stimulating hormone)
. Kufa kwa seli za pituitary baada ya mwanamke kujifungua

. Seli za pituitary kufa baada ya kushambliwa na kinga za mwili (autoimmune hypophysitis)

. Uvimbe ndani ya tezi ya pituitary

. Ugonjwa ambao hushambulia pituitary (sarcoidosis)

Sababu Zinazotokana Na Ovari

. Kutozalishwa kwa mayai (anovulation)

. Kuwa na uwingi wa homoni za kiume ndani ya damu (hyperandrogenemia)

. Kuvurugika kwa homoni (Polycystic ovary syndrome)

amenorrhea polycystic ovarian syndrome

. Kufeli kwa ovari mapema

. Ugonjwa wa kurithi unaodumaza ovari,  kuzuia hedhi (Turner syndrome)

. Seli za ovari kushambuliwa na kinga za mwili (Autoimmune oophoritis)

. Mionzi au tiba za chemotherapy

. Ugonjwa wa kurithi unaojaza galactose ndani ya damu (Galactosemia)

. Dosari za kimaumbile katika mkondo wa njia ya uzazi

Sababu za Kiutendaji

. Kuwa na uzito mdogo kwa sababu ya kuogopa kula (anorexia)/kula kupita kiasi (bulimia)

. Magonjwa sugu kama TB

.Kunenepa au kukonda kupita kiasi

. Utapiamlo

. Mfadhaiko au matatizo mengine ya kiakili

. Msongo wa mawazo wa kupitiliza

Matatizo Ya Kimaumbile

Matatizo katika viungo vya uzazi yanaweza kusababisha amenorrhea. Mifano ni kama:

Makovu kwenye tumbo la uzazi. Tatizo lilitwalo Asherman’s syndrome – kujenga kwa makovu juu ya ngozi ya juu ya uterus – huweza kutokea baada ya oparesheni ya uzazi, au baada ya tiba ya fibroids. Makovu kwenye uterus huzuia ujenzi wa kawaida na kujibandua kwa ngozi hiyo ya juu.

Kukosa Viungo Vya Uzazi. Wakati mwingine matatizo yanaanzia kwenye ukuaji wa mtoto tumboni yanayosababisha msichana azliwe bila baadhi ya viungo vya uzazi, kama uterus, cervix au uke. Kwa sababu viungo vyake havikukua vizuri, haweza kupata hedhi.

Dosari Za Kimamumbile Za Uke. Kitu kitakachoziba njia ya uke kinaweza kusababisha kuonekana kwa hedhi ya wazi. kunaweza kukatokea utando au ukuta katika uke ambao utazuia utokaji wa damu kutoka kwenye uterus na cervix.


DALILI ZITAKAZOKUJULISHA KAMA UNA AMMENORRHEA

Amenorrhea ni dalili ya kuwa kuna tatizo lililochificha na si ugonjwa Wenyewe. Dalil nyingine huweza kutokea kulingana na chanzo cha tatizo hilo la kukosa hedhi.

. Kutoka maziwa kwa mwanamke ambaye hana ujauzito, hali ambayo kitaalamu huitwa Galactorrhea, maumivu ya kichwa, kutokuona vizuri kingo za vitu vinaweza kuwa dalili za uvimbe ndani ya fuvu la kichwa.

. Kuongezeka kwa uotaji wa nywele kwa mtindo wa kiume (hirsutism), sauti nzito, chunusi kunaweza kusababishwa na kuzidi kwa androgen (homoni inayochangaia ujenzi wa tabia za kiume).

. Uyabisi wa uke, vipindi vya mwili kuwa na joto, kutoa jasho usiku, kukosa usingizi mzuri vinaweza kuashiria dasari katika ovari au kufeli kwa ovari.

. kuongeza kwa mwili au kukonda.
. Kuwa na wasiwasi kunaweza kujitokeza kwa mwanamke mwenye matatizo ya kiakili

VIPIMO NA UCHUNGUZI WA TATIZO LA AMENORRHEA



Msichana yeyote aliyefikia umri wa kubalehe na kuvunja ungo na ambaye bado hajaanza kupata mabadiliko yeyote ya kubalehe katika mwili wake hana budi kumuona daktari kwa ajili ya uchunguzi zaidi. Aidha msichana aliyefikia umri wa miaka 16 na ambaye bado hajaanza kupata hedhi anatakiwa pia kumuona daktari kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Kwa wanawake waliokuwa wakipata hedhi kama kawaida lakini ghafla wakaacha kupata kwa muda wa miezi mitatu mfululizo au zaidi nao pia hawana budi kumuona daktari kwa ajili ya uchunguzi wa tatizo hili.
Vipimo vifuatavyo vinaweza kufanywa kuchunguza sababu za kukosa hedhi kwa mwanamke:
  • Kupima damu kwa ajili ya kuchunguza kiwango cha homoni za FSH, LH, TSH na prolactin ambazo uzalishwaji wake unachochewa na tezi ya pituitary, na pia kupima kiwango cha homoni ya estrogen inayozalishwa na ovary.
  • Kipimo cha ultrasound ya nyonga kwa ajili ya kuchunguza uwepo wa matatizo katika njia ya uzazi na pia kuchunguza hali ya ovary.
  • CT scan au MRI ya kichwa kwa ajili ya kuchunguza uwepo wa matatizo kwenye tezi ya pituitary au hypothalamus.
  • Vipimo vya kufahamu ufanyaji kazi wa tezi ya thyroid
  • Kupima damu ili kufahamu kiwango cha homoni ya prolactin katika damu
  • Kuchunguza uterus kwa kutumia aina ya X-ray inayoitwa Hysterosalpingogram na kipimo kingine kiitwacho Hysteroscopy ambacho huchunguza chumba cha uterus.
Matibabu ya kukosa hedhi
Matibabu ya kukosa hedhi yanaweza kufanyika nyumbani bila kuhitaji dawa, ingawa pia, kutegemeana na chanzo cha tatizo, yanaweza kuhitaji dawa na hata upasuaji wakati mwingine.
Matibabu yasiyohitaji dawa
  • Baadhi ya wanawake wanaopata tatizo la kukosa hedhi kwa sababu ya kujinyima kula (wanaofanya dieting) na hivyo kupata upungufu wa virutubisho mwilini, wanashauriwa kula lishe bora.
  • Baadhi ya wanawake wanaopata tatizo hili la kukosa hedhi kwa sababu ya kuongezeka uzito kupitiliza, wanashauriwa kuwa makini katika aina ya vyakula wanavyokula ili kuwa na uzito unaotakiwa.
  • Wanawake wanaokosa hedhi kwa sababu ya kufanya mazoezi ya mwili kupita kiasi wanashauriwa kujiwekea kiasi katika ufanyaji wao wa mazoezi.
  • Iwapo kukosa hedhi kumesababishwa na msongo wa mawazo, ni jambo jema kutafuta njia za kushughulikia matatizo hayo na kuyatatua ili kuondoa msongo wa mawazo
  • Inashauriwa kutokuvuta sigara na kuacha kunywa kunywa pombe.
Matibabu yanayohitaji dawa
Matibabu ya kukosa hedhi hutegemea chanzo cha tatizo. Matibabu huelekezwa katika kutibu chanzo, na iwapo chanzo cha tatizo ni matatizo ya kimaumbile, upasuaji unaweza kufanyika.
Kwa wanawake wenye matatizo ya kuwa na kiwango kingi cha prolactin, daktari anaweza kushauri matumizi ya dawa aina ya bromocriptine au pergolide.
Kwa wanawake wenye upungufu wa homoni ya estrogen au wale wenye matatizo katika ovary zao, dawa zenye kurejesha homoni hiyo zaweza pia kutumika. Wakati mwingine dawa za uzazi wa mpango zaweza kutumika kurejesha mzunguko wa hedhi na pia kusaidia kuongeza kiwango cha homoni ya estrogen mwilini.
Upasuaji
Upasuaji unaweza kufanywa iwapo kuna
  • Uvimbe katika ubongo unaoathiri tezi ya pituitary na hypothalamus
  • Matatizo katika njia ya uzazi ya mwanamke
 MADHARA YA KUKOSA HEDHI YANAWEZA KUSABABISHA KUKOSA MTOTO
Ikumbukwe kuwa, kukosa hedhi si ugonjwa bali ni dalili ya kuwepo tatizo hivyo basi iwapo tatizo hilo lina uhusiano na kutunga mimba na kupata mtoto, uwezekano wa kupata mtoto utakuwa mdogo ikiwa tatizo hilo halitashughulikiwa. Matatizo kwenye tezi za pituitary, hypothalamus pamoja na ovary ambayo yana uhusiano mkubwa na kukosa hedhi, husababisha pia tatizo la ugumba. Iwapo matatizo hayo yatashughulikiwa ipasavyo, uwezekano wa kupata kupata hedhi na hatimaye kupata mimba huwa mkubwa

MATIBABU YA MATATIZO YA KUKOSA HEDHI NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo lolote linalohusu hedhi,uzazi na magonjwa mbalimbali na umejaribu njia hizo kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kuondoa tatizo la  hedhi mbovu,matatizo ya uzazi,kutoka harufu mbaya ukeni na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako Pia tutakuelimisha vyakula vinavyohitajika kurekebisha homoni mwilini 
Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI


KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

0 comments:

Copyright © 2017 Green health consultation centre