MZUNGUKO WA HEDHI,NAMNA YA KUFAHAM UREFU WA MZUNGUKO WA HEDHI NA SIKU ZA KUPATA UJAUZITO( MENSTRUATION CYCLES)

FAHAMU MAANA YA MZUNGUKO WA HEDHI,NAMNA YA KUFAHAM UREFU WA MZUNGUKO WAKO NA SIKU ZAKO ZA HATARI


Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, Ni matumaini yetu sote tunaendelea vyema kwa uwezo wake mwenyezimungu,walio wagonjwa na wenye matatizo Allah awajaalie wepesi katika matatizo na awape afya njema Ameeen.
Mpendwa msomaji wetu leo tunaangalia na kujifunza maana ya mzunguko wa hedhi na kuangalia namna gani tunaweza kujua siku bora ya kupata ujauzito,
Nianze kwa kusema wengi tunafahamu kuwa mzunguko wa hedhi wa mwanamke ni siku 28 na misemo mingi imekuwa ikitumika ikihusisha mzunguko huo na mwezi wa kalenda wa mwaka. Misemo kama kwenda mwezini, kuingia mwezini n.k. ni ya kawaida kuisikia. Jee, ulishawahi kudadisi uhusiano wa siku 29.5 za mwezi na mzunguko huu wa hedhi unaochukua siku 28? Tupate nadharia fupi:

Kama inavyojulikana kuwa jua na mwezi vina mchango katika maisha ya mimea na binadamu, homoni za binadamu hutolewamwilini kulingana na kiwango cha mwanga wa mwezi. Kabla ya ugunduzi wa umeme, utendaji kazi wa miili ya binadamu ulitegemea sana kiwango cha mwanga wa mwezi. Na akina mama wote walipata hedhi kwa wakati mmoja. Maisha ya sasa ambapo kuna vyanzo vingi vya mwanga usiku na mchana, mizunguko ya hedhi ya akina mama haiendani tena na uwepo wa mwanga wa mwezi.

Lakini hedhi ni nini na kuna uhusiano gani kati ya mzunguko wa hedhi wa mwanamke na siku za kubeba mimba mwanamke au kwa maneno mengine, katika mzunguko huo ni zipi siku ambazo mwanamke anaweza kupata mimba? Hayo ndiyo maswali ambayo yanawasumbua watu wengi kichwani nasi leo tutajaribu kuyajibu katika makala hii






 Mzunguko wa hedhi ni mfululizo wa mabadiliko katika mwili wa mwanamke katika kujiandaa kwa mimba ambayo inaweza ikatungwa. Kila mwezi ovari zinaachia yai moja lililokomaa (ovulation) na homoni katika mwili hubadilika kila wakati ili kuiandaa nyumba ya uzazi (uterus) kwa mimba itakayotungwa. Endapo yai lililoachiwa halitarutubishwa, ile ngozi nyororo inayotanda juu ya nyumba ya uzazi hujinyofoa na kutoka nje ya uke, na tendo hili ndilo linaloitwa hedhi yani mwanamke kutokwa na damu ya mwezi ukeni(menstruation).

Kuwa na mzunguko wa hedhi unaoeleweka ni ishara kuwa viungo muhimu katika mwili wa mwanamke vinafanya kazi vizuri.
Mzunguko wa hedhi huhesabiwa kutoka siku ya kwanza ya kuanza kutoa damu (period) hadi siku ya kwanza ya kutoa damu ya mwezi unaofuata.

Mzunguko wa hedhi huchukua wastani wa siku 28 lakini kila mwanamke ana tofautiana na mwingine. Mizunguko ya mwezi
huweza kuchukua kati ya siku 21 hadi 35. Msichana anapoanza kupata hedhi mizunguko yake huwa mirefu, isiyotabirika – na si ajabu akakosa kupata siku zake kwa kipindi fulani. Kadri umri wake unavyoongezeka, mizunguko yake hupungua siku na kuwa mifupi na inayotabilika zaidi.


Mzunguko wa mwezi wa mwanamke unaweza kujirudia kwa vipindi vilivyo sawa au vilivyo na urefu wa siku tofauti, damu inaweza kutoka kwa wingi au kidogo, ikaambatana na maumivu au isiwe na maumivu. Vyote hivi ni vitu vya kawaida kwa mwanamke, – “mzunguko wa kawaida kwa mwanamke ni ule aliouzoea.” Tunasema kuna mabadiliko au kuna matatizo katika mzunguko wa hedhi wa mwanamke pale mambo yanapokwenda tofauti na alivyoyazoea mwanamke mwenyewe katika mwili wake. Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha kuvurugika kwa mzunguko wa mwezi wa mwanamke. Baadhi ya sababu hizo ni kama zifuatazo:

Kubadili Njia Ya Mpango Wa Uzazi:Kubadili njia ya mpango wa uzazi kutoka moja hadi nyingine kunaweza kuvuruga mzunguko wa hedhi.


Kukosa Uwiano Wa Homoni: Ni kawaida kwa mwanamke kukosa uwiano mzuri wa homoni za estrogen na progesterone miaka michache baada ya kuvunja ungo na kabla ya kukoma hedhi. Hali hiyo huweza kusababisha mzunguko wa hedhi kuwa mrefu au mfupi na kutokwa na damu kidogo au nyingi kupita kiasi wakati wa hedhi.


Ujauzito Au Kunyonyesha: Kuchelewa kupata au kukosa hedhi ni dalili ya awali ya ujauzito. Kunyonyesha kwa kawaida humzuia mwanamke kurudia kuanza kupata siku zake baada ya mimba.


Matatizo Ya Ulaji, Mazoezi Mazito Au Kupungua Mwili: Matatizo katika ulaji wa chakula, kupungua uzito kwa kiwango kikubwa na kuongezeka kwa shughuli nzito za mwili huweza kusimamisha mzunguko wa hedhi.
Polycystic Ovary Syndrome (PCOS): Hii ni hali inayoweza kutokea ambapo vifuko vidogo vilivyojaa majimaji (cysts) huota kwenye ovari.  Dalili ya Polycystic ovary syndrome ni kupata hedhi zisizotabilika au hedhi fupi au kukosa kabisa hedhi. Hii ni kwa sababu mwanamke mwenye PCOS hawezi kutoa yai (ovulation) kila mwezi kama inavyotakiwa. Utengenenezaji wa homoni zake unaweza kuwa hauna uwiano unaotakiwa, na pengine kukawa na kiwango kikubwa mno cha testosterone.


Ovari Kuacha Kufanya Kazi Mapema – Premature Ovarian Failure: Hili ni tatizo ambapo ovari huacha kufanya kazi kama inavyotakiwa kwenye umri unaopungua miaka 40. Wanawake wenye tatizo hili huweza kuwa na siku ambazo hazitabiriki kwa kipindi kirefu cha maisha yao.


Pelvic Inflammatory Disease (PID):Maambukizi ya wadudu kwenye viungo vya uzazi huweza kumsababishia mwanamke apate hedhi zisizotabirika.


Uterine Fibroids: Uvimbe ulioota katika nyumba ya uzazi husababisha damu kutoka kwa wingi wakati wa hedhi na
kutokwa damu katikati ya hedhi.


Matatizo Ya Tezi Ya Thyroid: Tezi ya thyroid ambayo hupatikana katika eneo la shingo la binadamu hutoa homoni za kusimamia mwenendo wa kemikali zinazobadili chakula na kuleta nguvu katika mwili. Mabadiliko ya kiwango cha thyroid – kuwa na kiwango kidogo cha thyroid (hypothyroidism) katika mwili – huweza kusababisha kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi.


Kipindi hiki cha mzunguko huu wa hedhi kinagawanyika katika awamu nne zinazoongozwa na kupanda na kushuka kwa homoni katika mwili. Mwanamke kwa wastani hupitia mizunguko ya hedhi 450 katika maisha yake. Hapa chini tutaziona awamu hizo nne na kuelezea ni nini kinachotokea katika mwili wake katika kila awamu. Hapa chini tunazijadili awamu hizo nne za mzuguko wa hedhi:


HEDHI-KUMWAGA DAMU (THE BLEEDING PHASE)




Hedhi (menstruation) ni tendo linalotokea kila mwezi kwa mwanamke ambalo linahusisha utokwaji wa damu na vitu
vingine vilivyokuwa vinajijenga kwenye tumbo la uzazi, kupitia sehemu ya uke.

Msichana wa kawaida huanza kupata siku zake akiwa na umri wa miaka 12, hii ni wastani na haina maana wote wataanza kupata siku katika umri huo. Wapo wasichana wanaoanza kuona siku zao kwenye umri mdogo sana wa miaka 8 na wapo wanaochelewa hadi kwenye umri wa miaka 15. Mara nyingi wasichana huanza kuona siku zao miaka 2 baada ya maziwa (matiti) kuanza kuota.

Mwanamke anapoingia mwezini, utando uliokuwa umejijenga kuzunguka nyumba ya uzazi (uterus) pamoja na damu ya ziada
hutoka nje ya mwili kupitia sehemu ya uke. Utokaji huo wa vitu hivi unaweza kuwa unaolingana kila mwezi au ukawa tofauti mwezi hadi mwezi. Utokaji huo huweza kuwa tofauti kutoka mwanamke mmoja hadi mwingine. Damu inaweza kutoka kwa kiasi kidogo au nyingi na urefu wa hedhi (siku za kutoka damu) zinaweza kuwa tofauti kutoka mwezi mmoja hadi mwingine. Kwa kawaida mwanamke hutokwa damu kwa siku 3 hadi 5, lakini siku 2 hadi 7 bado inachukuliwa kuwa ni kawaida.

THE FOLLICULAR PHASE



Hii ndiyo awamu inayofuatia mara baada ya awamu ya kwanza ya Kutoa Damu (The bleeding Phase). Awamu hii imepewa jina hilo kwa sababu tezi ya pituitary (Pituitary Gland) inatoa homoni iitwayo Follicle Stimulating Hormone (FSH) ambayo inatoa ishara ambayo itavifanya vifuko vinavyotunza mayai (follicles) kukomaa. Shughuli katika awamu hii ya mzunguko wa hedhi huanzia kwenye tezi ya hypothalamus inayopatikana katika ubongo. Tezi hii inashughulika na usimamiaji wa kiu, njaa, usingizi, hamu ya mapenzi n.k. Hypothalamus hutoa kemikali iitwayo Follicle Stimulating
Hormone Releasing Factor (FSH-RF) ambayo itaiamuru tezi ya pituitary kutoa homoni iitwayo Follicle Stimulating Hormone (FSH) na kiasi kidogo cha homoni ya Leutenizing Hormone (LH). Utolewaji wa homoni hizi katika damu husababisha vifuko vya mayai (follicles) kukomaa.
Vifuko vya mayai vikianza kukomaa vitatoa homoni nyingine iitwayo estrogen. Kadiri vifuko hivi vinavyozidi kukomaa katika siku saba, homoni ya estrogen hutolewa zaidi na zaidi. Pamoja na estrogen, testosterone homoni ya aina nyingine huongezeka katika damu. Kuongezeka kwa homoni hizi mbili huufanya mwili kupata nguvu na ufanyaji kazi wa ubongo huboreshwa. Mwanamke atasikia hali ya kujiamini na mwenye kupenda kuthubutu. Kuongezeka kwa testosterone kutamfanya ajisikie kupenda kufanya mapenzi wakati oestrogen itamfanya apende kuwa mtu wa kutoka na kuonekana
wakati huo hamu ya kula ikipungua. Ni kipindi cha kusikia ukamilifu na bora kwa kufanya maamuzi na kuthubutu mipango mikubwa na migumu.

Homoni ya estrogen huifanya ngozi nyororo inayotanda juu ya nyumba ya uzazi (uterus) kuwa nene na kuleta mabadiliko kwenye ute wa mwanamke (cervical mucous). Kiwango cha estrogen kikifikia kiasi fulani, hypothalamus hutoa Leutenizing Hormone Releasing Factor (LH-RF) ambayo itaifanya tezi ya pitutary kutoa kiasi kikubwa cha Leutenizing Hormone (LH). Tendo hili hukifanya kifuko cha yai kilichokomaa kupita vyote kupasuka na kuachia yai.


THE OVULATORY PHASE


Kutolewa kwa yai (ovulation) ni kilele cha shughuli zote zilizokuwa zikiendelea katika mwili wa mwanamke katika wiki chache sasa toka alipoanza kutoka damu. Yai lililotolewa na kifuko katika ovari lina uhai wa wastani wa saa 12 hadi 24 kabla ya kunywea.

Yai linapokaribia kuachiwa, kiwango cha damu kinachopelekwa kwenye ovari huongezeka na misuli inayoshikilia ovari hujikunja ili kusogeza ovari karibu na mrija wa uzazi (fallopian tube), kulifanya yai litakaloachiwa kuingia kirahisi ndani ya mrija wa uzazi. Muda mfupi kabla ya yai hili kuachiwa, mlango wa uke (cervix) hutoa ute kwa wingi. Ute huu unaonata huasidia mbegu za kiume kusafiri kuelekea kwenye yai. Baadhi ya wanawake hutumia ute huu
kama ishara ya siku ambazo wanaweza kupata ujauzito.

Yai likiwa ndani ya mirija ya uzazi husafirishwa kwa kutumia namna ya vijinywele viitwavyo “cilia” kuelekea kwenye nyumba ya uzazi (uterus). Yai hili litarutubishwa endapo kutakuwa na mbegu za kiume.

Tofauti na mwanamme ambaye hutengeneza mbegu za kiume kila siku na kwa karibu muda wote wa maisha yake, mwanamke
anazaliwa na mayai yake ndani ya vikapu vyake miwili – ovari. mwanamke huzaliwa na mayai yake haya machanga yapatayo milioni moja hadi mbili ndani ya ovari. Katika maisha yake mayai mengi hufa, kuanzia anapokuwa mchanga, na hubakia na mayai yapatayo 400,000 anapofikia kuvunja ungo. Kila anapoingia mwezini, mayai yapatayo 1,000 hupotea na ni moja tu linalofikia kukomaa (ovum) na kuachiwa liingie ndani ya mrija wa uzazi. Katika mayai yake yote milioni moja au ambili aliyozaliwa nayo, ni mayai kama 450 tu yatakayofikia kukomaa.

Ni kiasi kidogo sana cha follicles kitakuwa kimebakia mwanamke huyu anapofikia kukoma hedhi hali ambayo kwa wanawake wengi hutokea kwenye miaka kati ya 48 na 55.  Hata hivyo follicles hizi si rahisi kukomaa tena na kutoa mayai kutokana na mabadiliko ya homoni yanayoendana na kukoma kwa hedhi.

The luteal pHASE



Siku 2 hadi 3 baada ya yai kutolewa, viwango vya estrogen na testosterone vitaanza kushuka katika damu na homoni ya progesterone kuanza kutengenezwa. Progesterone ni homoni inayopunguza wasiwasi katika mwili hivyo kuufanya mwili kuwa tulivu. Katika siku zinazofuata, wanawake wengi hujisikia vibaya kutokana na Premenstrual Syndrome (PMS), tatizo ambalo limejulikana kwa miaka mingi.

Premenstrual Syndrome ni jumla ya matatizo yanayowapata wanawake na kuwafanya wajisikie vibaya kutokana na viwango
vya homoni kuwa juu kabla, na wakati mwingine, wakati wakiwa katika hedhi.

Aina moja ya PMS hujionyesha kwa mwanamke kuwa na wasiwasi, kuna na hasira na asiyetabirika. Mara nyingi hali hiyo  hupotea mara baada ya kuingia kwenye siku zake. Hii inaweza kutokana na uwiano wa estrogen na progesterone. Estrogen ikizidi, wasiwasi hutanda na progesterone ikizidi, hali ya kuwa na mfadhaiko hujionyesha.

Aina nyingine ya PMS ni kupenda sana sukari (chocolate, mikate , wali mweupe n.k.), uchovu wa mwili na maumivu ya kichwa. Hii inaweza kuwa inatokana na mwili kuongeza usikivu wa insulin unaotokana na kuongezeka kwa viwango vya homoni kabla ya hedhi.

Wakati huu kuna mabadiliko yanayotokea kwenye uterus na ovari. Kile kifuko kilichotoa yai hubadilika rangi na kuwa cha njano “corpus luteum.” Kifuko hiki kinavyoendelea kupona,  kinatoa homoni ya estrogen na kiwango kikubwa cha progesterone, homoni muhimu katika utunzaji wa mimba. Hapo baadaye endapo mimba haikutungwa, kifuko hiki hubadilika rangi na kuwa cheupe ” corpus albicans”.

Homoni ya progesterone huifanya ngozi laini inayotanda juu ya uterus (endometrium) kufunikwa na ute, unaozalishwa na tezi zilizopo katika ngozi hiyo. Kama yai halikurutubishwa na mimba kutungwa, arteri za kwenye ngozi nyororo ya juu ya uterus hujifunga na damu kusitishwa kuelekea kwenye ngozi hiyo. Vijibwawa vya damu katika veni hupasuka, pamoja na utando wa endometrium, hutoka nje ya mwili na kuwa ndiyo mwanzo wa hedhi. Urefu wa hedhi hutofautiana baina ya wanawake na hubadilika katika maisha yao.

JINSI YA KUFAHAMU UREFU WA MZUNGUKO WAKO NA SIKU ZA KUPATA UJAUZITO(SIKU ZA HATARI)

Ili kufahamu vizuri ni siku zipi ni hatari kwa mwanamke kupata mimba, unahitaji kwanza kujifunza jinsi mzunguko wa hedhi (menstrual cycle) unavyofanya kazi.

Kwa wastani, mzunguko wa hedhi huwa ni siku 28.

Mzunguko wa hedhi unaanza kuhesabiwa siku ya kwanza wakati mwanamke anaanza kuona siku zake (kublidi) na tunaiita ni siku ya Kwanza.

Baada ya kuuelewa vizuri mzunguko wa hedhi wa mwanamke, sasa tunaweza kuzungumzia siku za kupata mimba mwanamke. Kimsingi kuna siku 6 ambazo mwanamke anaweza kubeba mimba – siku 5 kabla ya kutoa yai na saa 24 baadaya yai kutolewa. Hii ni kwa sababu mbegu za mwanamme zina uwezo wa kukaa kwa siku 5 ndani ya mwili wa mwanamke kabla hazijafa na yai (ovum) la mwanamke lina uwezo wa kuishi kwa saa 12 hadi 24.
Mzunguko wa hedhi wa kawaida huwa una sifa madhubuti zifuatazo:

1. Idadi ya siku katika mzunguko mmoja (cycle length)

Kwa kawaida idadi ya siku katika mzunguko ambazo huhesabika kama ni mzunguko wa kawaida ni siku 21 hadi 35 (na ni hapo ndipo tunapata wastani wa siku kuwa 28 yaani [(21+35)÷2].

Hivyo mpendwa msomaji wangu usikariri kuwa mzunguko wa kila mwanamke ni siku 28. Wapo wanawake wana mzunguko wa siku 27, wengine 25, wengine 35, wengine 29.

2. Sifa ya pili ni uwiano wa idadi ya siku za mzunguko kati ya mzunguko mmoja na mwingine

Hili nalo ni miongoni mwa changamoto kubwa sana katika suala zima la tendo la ndoa kwani inaweza kuwa vigumu kuzitambua siku hatari kwa mwanamke kubeba ujauzito.

Ili tuhitimishe kwamba mwanamke ana mizunguko ya hedhi iliyo sawa (regular cycles), idadi ya siku za mizunguko ya hedhi haitakiwi itofautiane kwa zaidi ya siku 7.

Mfano, kama mwezi wa kwanza uliona siku zako baada ya siku 28, mwezi wa pili ukaona baada ya siku 30, mwezi wa tatu ukaona baada ya siku 35 na mwezi wa nne ukaona baada ya siku 21, bado mzunguko wako uko kwenye uwiano mzuri (regular cycle) kwa kuwa mzunguko mmoja na mwingine haujatofautiana kwa zaidi ya siku 7.

Hivyo usikariri kwamba siku za mzunguko wa hedhi kwa kila mwanamke ni siku 28, hilo halipo. Hizi siku 28 ni wastani tu.

Wengine wanaona siku zao kila baada ya siku 21, wengine kila baada ya siku 25, wengine 29, wengine 35 na bado tunasema mizunguko yao bado ni mizunguko ya kawaida.

Pia fahamu ya kuwa si lazima idadi ya siku katika mzunguko mmoja ilingane na mzunguko mwingine kwa mwanamke huyo huyo. Mfano usitarajie kuwa kama mwezi wa tatu (march) ameona siku zake baada ya siku 28 na mwezi wa nne (april) pia ataona siku zake baada ya siku 28. Si lazima itokee hivyo lakini pia huwa inaweza kutokea.

Mfano, mwanamke mmoja mzunguko huu anaweza kuona siku zake baada ya siku 28, mzunguko unaofuata baada ya siku 27, mzunguko mwingine baada ya siku 30, mzunguko mwingine baada ya siku 29, mzunguko mwingine baada ya siku 25 na bado yuko kwenye uwiano sawa kwakuwa tofauti si zaidi ya siku 7 kama nilivyoeleza pale juu.

3. Idadi ya siku za kuona siku zake

Usichanganye kati ya siku za hedhi (menstrual period) na mzunguko wa hedhi (menstrual cycle) kwani hivi ni vitu viwili tofauti kabisa.

Siku ya kwanza ya kuona siku zako ndiyo siku tunaanza kuhesabu mzunguko wako wa hedhi (day one) na siy siku ya kumaliza kuona siku zako (kublidi) kama wengi wanavyodhani.

Kawaida idadi ya siku za siku zako ni kati ya siku 3 mpaka 7. Kila mwanamke ana idadi yake kati ya hizo. Mwingine anaenda siku 3 amemaliza, mwingine siku 4, mwingine 5 mwingine 6 mpaka 7. Chochote zaidi ya siku 7 si cha kawaida na unahitaji kuonana na daktari kwa uchunguzi zaidi.

4. Wingi wa damu

Hii ni Sifa ya mwisho ya mzunguko wa hedhi na inaangalia kiasi cha damu inayotoka wakati wa hedhi. Hapa kuna wanawake wa aina mbili ambapo mwanamke anaweza kutoa damu ya kawaida (normal bleeding) na mwingine akatoa damu nyingi sana (heavy bleeding).

 NAMNA YA KUKOKOTOA MZUNGUKO WAKO WA HEDHI
Soma kwa umakini maelezo haya ili uweze kukokotoa mzunguko wako wa hedhi
Ikiwa ulipata bleed tarehe 12/10/2018
Basi tarehe 12/10/2018 inakuwa siku yako ya kwanza ya mzunguko wa hedhi,
Na tarehe 13/10/2018 inakuwa siku yako ya pili ya mzunguko wa hedhi
Na teherhe 14/10/2018 inakuwa siku ya tatu kadhalika
tarehe 15/10//2018 ni siku ya 4
tarehe 16/10/2018 ni siku ya 5
.
.
Nakuendelea, utakoma kuhesabu mzunguko wako wa hedhi mara tu unapopata hedhi ingine.

Ikiwa Utapata bleed ingine tarehe 10/11/2018  Basi siku ya mwisho ya mzunguko wako wa hedhi kwa mwezi wa kumi inakuwa tarehe 09/11/2018 Na tarehe 10/11/2018 inakuwa ni siku yako ya kwanza ya mzunguko wa mwezi wa 11

ZINGATIA mwezi unaweza kuwa na siku 31,28,29 au 30 - kwa hiyo kama hujui ukubwa mbalimbali wa miezi lazima utumie kalenda yako vizuri.
Kwa mfano kwa mwanamke mwenye mzunguko wa siku 28,kuipata siku ya ovulation tunachukua 28-14 tunapata 14, kwahiyo kutoka siku ya kwanza mwanamke alipoanza kubleed ni siku ya 14 ndipo yai linakuwa tayari kurutubishwa.

Kwa mwenye mzunguko wa siku 30, tunachukua 30-14 (luteal phase) =16, kwa hiyo mwanamke mwenye mzunguko wa siku 30, ovulation inauwezekano mkubwa wakutokea siku ya 16 na si ya 14 (kuwa makini hapo).

Yule mwenye mzunguko wa siku 35, ovulation day ni 35-14 = 21, kwa hiyo kwa mwanamke mwenye mzunguko wa siku 35, ovulation ina nafasi kubwa ya kutokea siku ya 21 na si ya 14.

Sasa baada ya kuijua siku ya ovulation lazima uwe makini na siku zinazokaribiana na siku ya ovulation kwani nazo ni siku hatari pia kwasababu Mbegu ya kiume inauwezo wa kuwa hai hadi masaa 48 (2 days) tangu shahawa zimwagwe[ejaculation] na yai lina uwezo wa kuwa hai hadi masaa 24 [one day] tangu lilipotoka kwenye ovary.

Kwaiyo kama mwanaume akijamiiana na mwanamke siku mbili kabla ya yai kutolewa kwenye ovary, mbegu inaweza kuwa hai bado na kutungisha mimba endapo yai litatolewa ndani ya siku mbili zijazo kwa mfano kama siku ya ovulation ya mwanamke ni siku ya 14, mwanamke akijamiiana na mwanaume siku ya 12, uwezekano wa kupata mimba ni mkubwa.

Kadhalika kama mwanamke ametoa yai siku ya 14 kisha akajamiiana ndani ya masaa 24 mbele, pia anaweza kupata mimba kwasababu kipindi mbegu zinamwagwa zinaweza kulikuta yai bado lipo hai na kutungisha mimba.

Kwa ufupi,ni siku tatu tu ndizo hatarishi sana kwa mwanamke kupata mimba,yaani,siku mbili kabla ya ovulation na ndani ya masaa 24 baada ya ovulation[narrow but dangerous window].

Kwa kuongezea,kipindi cha ovulation mwanamke anapata nyege kali sana kwasababu ni kipindi ambacho kuna homoni fulani[androgens] ambazo huchochea nyege huzalishwa kwa wingi. Pia kipindi hicho cha ovulation au karibia ovulation joto la mwili la mwanamke hupanda,anajihisi mwili kuchemka tofauti kidogo na ilivyo kawaida yake.

Sasa, kwa vile nimesema kuwa hatuwezi kuwa na uhakika kwa asilimia 100 wa siku ya kushika mimba, basi tunalazimika kutumia kanuni ya kuepuka tendo la ndoa kwa muda wa wiki nzima. Ambazo ni siku zilizo karibu sana na siku ya kushika mimba (ovulation days) kwa wale wanaotumia njia ya kalenda.

Mfano, kama una mzunguko wa siku 30, kuipata siku ya ovulation chukua 30- 14=16, kwa hiyo siku ya ovulation ni ya 16 tangia ulipoanza kuona damu siku ya kwanza. Sasa kama ni siku ya 16, ondoa siku nne kabla ya hiyo siku ya ovulation.

Kwahiyo kuanzia siku ya 12 hapo, usishiriki tendo la ndoa.

Pia jumlisha siku 3 mbele, ambapo mwanamke atatakiwa kuanza tendo la ndoa kuanzia siku ya 19 huko ili kuepuka mimba..

JEDWALI LINALOONYESHA SIKU ZA HATARI KWA MIZUNGUKO TOFAUTI





MATIBABU YA MATATIZO YA HEDHI NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo lolote linalohusu hedhi,uzazi na magonjwa mbalimbali na umejaribu njia hizo kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kuondoa tatizo la  hedhi mbovu,matatizo ya uzazi,kutoka harufu mbaya ukeni na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

4 comments:

FAHAMU CHANZO CHA UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE) NA MATIBABU YAKE

Ugonjwa wa vidonda vya TUMBO(PEPTIC ULCERS DISEASE) na matibabu YAKE


Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, Ni matumaini yetu unaendelea vyema mpendwa msomaji wetu,leo tutajadili ugonjwa wa vidonda vya tumbo ambapo tutaangalia chanzo cha ugonjwa huu na matibabu yake
Vidonda vya tumbo (Peptic Ulcers) ni ugonjwa unaompata mtu ambao hutokea vijitundu au michubuko katika kuta za ndani za viungo vya mfumo wa uyeyushaji chakula. Michubuko hiyo huweza kutokea katika eneo la mfuko wa tumbo, katika duodenum au katika eneo la koo.
Pia vidonda vya tumbo ni mojawapo ya ishara za mwili kuanza kuishiwa maji kutokana na uharibifu wa kuta za ndani ya tumbo.

Asilimia 94 ya damu ni maji, ubongo wetu una zaidi ya asilimia 85 za maji, na tishu zetu laini zina asilimia 75 ya maji.Tunatumia maji kupumua nje, kila masaa 24 tunapoteza glasi 4 za maji kwa kupumua tu nje.

Kwahvyo sehemu kubwa ya miili yetu huishiwa maji kutokana na sisi kusubiri kiu ndipo tunywe maji. Hivyo, haupaswi kusubiri kiu ndipo unywe maji, kiu ni ishara iliyochelewa ya mwili kuhitaji maji.

Seli ndani ya mwili lazima zibaki katika kiasi kidogo cha alkalini kutoka 7.2 mpaka 7.4, wakati 7.0 ni ya kati au husemwa sifuri katika kipimo cha PH yaani potential hydrogen. Chini ya 7.0 ni asidi na juu ya 7.0 ni alkalini.

Unaweza kukinunua kipimo cha PH na kupima Ph ya mate yako au ya mkojo wako kila mara ili kupata mwelekeo wa namna gani ufanye katika mwili wako ibaki kuwa ya 7.2 mpaka 7.4 kwenye seli ndani ya mwili wako.

Ikiwa mate yanasoma 6.0 au 6.5 ni kiashiria kuwa una asidi iliyozidi kwenye seli zako.

Kila mtu anapaswa kula zaidi vyakula vyenye alkalini yaani matunda na mboga za majani na kunywa vinywaji vyenye asidi chache na ikibidi basi atumie vinywaji vyenye alkalini nyingi kama juisi ya limau, juisi ya chungwa, ya zabibu na maji halisi.

Kwa maneno mengine, hali ya uasidi ndani ya mwili ndiyo hupelekea kusikia maumivu yatokanayo na vidonda vya tumbo.

 Inakadiriwa kuwa asilimia 5 hadi 10 ya watu hupatwa na ugonjwa huu angalau mara moja katika maisha yao. Huu ni ugonjwa ambao unaweza kumrudia mtu baada ya kupona endapo chanzo chake hakikudhibitiwa. Kama ugonjwa huu utamrudia mgonjwa , mtu huyu atakuwa amejiweka kwenye hatari kubwa ya kupata madhara makubwa zaidi kama kutokwa na damu au kutokea tundu kubwa katika kuta za mfuko wa tumbo.

VYANZO/VISABABISHI VYA UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)


Linapokuja suala la nini husababisha vidonda vya tumbo unaweza ukapata stori nyingi bila idadi, lakini kwa kifupi kabisa; vidonda vya tumbo ni ishara za mwili kupungukiwa maji na kama matokeo ya asidi kuzidi mwilini kuliko alkaline. Vinaweza pia kuletwa na bakteria ajulikanaye kama H.Pyroli.

Vitu vifuatavyo vinahusika katika kuleta vidonda vya tumbo mwilini:

1. Asidi iliyozidi mwilin

Kawaida mtu anapokaribia kutaka kula chakula chochote, au akiwaza kutaka kula au akiuona tu msosi kwa macho,tumboni huzalishwa haidrokloriki asidi ili kuuandaa na kuusaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Kadri unavyoendelea kuishi haidrokloriki asidi hiyo huenda kutoboa kuta za tumbo na hatimaye taratibu baadaye husababisha mtu kupata VIDONDA VYA TUMBO.

Aina zote mbili za vidonda vya tumbo hutokea kutokana na kutolingana nguvu kati ya nguvu ya mnyunyizo wa asidi ya tumbo katika kushambulia na uwezo wa kuta za tumbo katika kuzuia mashambulizi.

Utokeaji wa vidonda vya tumbo hutegemea zaidi juu ya vipengele viwili. Kwanza, vitu ambavyo huongeza mnyunyizo wa asidi katika tumbo, mfano vyakula vya kusisimua, vyakula vya mafuta, uvutaji wa sigara, utumiaji pombe, chai, kahawa, baadhi ya dawa tunazotumia kujitibu maradhi mbalimbali mwilini, n.k.

2. Mfadhaiko wa akili utokanao na shida za maisha:

Mfadhaiko wa akili utokanao na shida za maisha ni moja ya vipengele vikuu vinavyosababisha vidonda vya tumbo.

Mfadhaiko huongeza utiririkaji wa asidi ndani ya tumbo. Hii asidi ya ziada ambayo hutiririka ndani ya tumbo kama matokeo ya mfadhaiko na hakuna chakula cha kufanyiwa kazi au kumeng’enywa humomonyoa kuta za tumbo na hivyo kusababisha vidonda.

Utafiti uliofanywa katika miaka ya hivi karibuni umeonyesha kuwa akili hutumia sehemu kubwa ya nguvu ya mwili. Baadhi ya madaktari wamesema mfadhaiko huchangia sana katika kutokea kwa magonjwa mengi mwilini zaidi ya 50. !

Utafiti wa kisayansi unasema hisia zetu na hali zetu na jinsi tunavyomudu kudhibiti mifadhaiko inaweza kutusaidia kuelewa ni kwa kiwango gani afya zetu zilivyo madhubuti au zilivyo dhaifu.

Ingawa utafiti katika uwanja huu ni mpya, lakini utendaji kazi wa mfumo wa kinga ya maradhi ya mwili unaweza kukandamizwa na mfadhaiko wa akili au mawazo yatokanayo na shida za maisha.

Majaribio yaliyofanywa kwa watu wenye mifadhaiko sana kama wajane, watu waliopewa talaka na wale wenye kupambana na adui yalionesha kuwa watu hao huweza kupata maradhi mara kwa mara kutokana mfumo wao wa kinga ya maradhi kugandamizwa.

Mfano katika kukabiliana na adui, akili hutambua hofu na ubongo hupata taarifa; neva zenye kujiendesha zenyewe hupanda juu ili kukutana na adui. Hapo moyo huenda mbio, msukumo wa damu nao hupanda na damu huvimba kwenye misuli kwa ajili ya maandalizi ya mapigano au makabiliano na adui.

Oksijeni na virutubishi vingine hukimbilia kwenye ubongo vikimfanya mtu awe tayari zaidi kwa mapigano, na hapo myunyizo wa adrenalini, homoni inayohusika na uzalishwaji wa nguvu mwilini huongezeka.

Kadiri mfadhaiko unavyokuwa ni wa muda mfupi, ndivyo pia athari zake zinavyokuwa ni fupi. Lakini pindi mfadhaiko unapodumu kwa muda mrefu kama vile kipindi cha ndoa isiyo na amani au katika hali ya matatizo mengi kila mara, athari zake nazo hudumu kwa muda mrefu.

Dalili za mtu mwenye mfadhaiko

Ikiwa bila ya sababu yoyote, zaidi ya dalili sita katika hizi zifuatazo zitatokea, basi mtu amwone daktari kuhusiana na mfadhaiko. Dalili hizo ni:

1. Kujisikia huzuni sana kiwango cha kutokuwa na matumaini yoyote,
2. kupoteza kabisa uwezo wa akili kufurahi,
3. kupoteza kabisa hamu ya tendo la ndoa
4. Kupoteza hamu ya chakula
5. Kukosa usingizi
6. Wasiwasi unaosababisha hali ya kutotulia kwa ujumla
7. Kupoteza kumbukumbu au hali ya kusahausahau na kushindwa kuamua
8. Kughadhibishwa na vitu vidogo, yaani mtu kitu kidogo tu ameshachukia
9. Kujiona huna thamani na kujitenga na marafiki na ndugu.

3. Sababu ya tatu inayosababisha vidonda vya tumbo ni Haraka haraka

Maisha ya kisasa yanataka haraka katika kazi nyingi tuzifanyazo kila siku, ni lazima tufike mahala haraka na turudi haraka! Haraka hizi husababisha vidonda vya tumbo. Mbanano wa ratiba katika shughuli zako za kila siku pia husababisha matumbo nayo kubanana.

Malalamishi makubwa leo ya wagonjwa kwa madaktari wao ni: “Tumbo langu linanisokota na kuniletea matatizo, au nasikia kiungulia baada ya kula”. Haraka haraka na wasiwasi ni baadhi ya sababu ya matatizo haya.

Tumbo ni kama kioo cha akili. Akili ikihangaishwa, basi wasiwasi na msukosuko wa hisia hufungia breki kwenye viungo vya ndani. Akili iliyohangaishwa na kukimbizwa mbio mbio hupeleka hisia kwenye tumbo na kusababisha mkazo wa ghafla wa misuli na hapo husababisha kiungulia na maumivu.

Ili kuepuka kufanya kazi zako kwa hali ya uharakaharaka unashauriwa kupanga kabla ni kazi gani na gani utaenda kuzifanya siku inayofuatia kwa kuziandika kabisa katika karatasi au kitabu maalumu kiitwacho kiingereza diary au kumbukumbu za kila siku kwa Kiswahili na mhimu ni uwe na kiasi kwa kila jambo kwani si lazima umalize kazi zote leo.

4. Sababu ya nne ya kutokea vidonda vya tumbo ni ulaji wa Vyakula vya kusisimua

Vyakula vya kusisimua ni hatari kwa neva za tumbo. Uchunguzi wa kitabibu unabainisha kuwa vyakula vya kusisimua kama vile ketchup, chill sauce, achali, pilipili na vingine vingi vya jamii hii huchangia kwa kiwango fulani kudhuru neva za tumbo na havitakiwi kuliwa hasa kwa mtu mwenye vidonda vya tumbo na mwenye tatizo la kutosagika chakula tumboni. Sababu ni kuwa, visisimuaji hivi huzichoma pia kuta za tumbo.

5. Vinywaji na vyakula vyenye kaffeina na asidi nyingi

Vinywaji vyenye kaffeina na asidi nyingi kama vile chai ya rangi, kahawa, soya sauce, mayonnaise, jibini, Vyakula jamii ya Mkate, samaki wa kwenye makopo, pombe, soda na juisi za viwandani pia huchangia kwa kiasi kikubwa katika kutokea kwa vidonda vya tumbo.

DALILI ZA UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)


Dalili zitakazokufanya ujihisi una vidonda vya tumbo ni kuchoka choka sana bila sababu maalum, kuuma mgongo au kiuno, kupungukiwa au kupoteza kabisa nguvu za kijinsia, kizunguzungu, kukosa usingizi, usingizi wa mara kwa mara. Maumivu makali sehemu ya mwili, kifua kwa ndani kana kwamba unachomwa na kitu cha moto au chenye ncha kali.

Maumivu hayo wakati mwingine hutokeza mgongoni na huchoma kama sindano yenye sumu na kuacha maumivu makali. Dalili zingine ni kichefuchefu, kiungulia, tumbo kujaa gesi, tumbo kuwaka moto, maumivu makali sehemu kilipo kidonda, kukosa choo au kupata choo kwa shida tena kikiwa kigumu na chenye kukatika kama cha mbuzi.

Kutapika nyongo, kutapika damu au kuharisha, sehemu za mwili kupata ganzi n.k. Pia dalili zingine ni kukosa hamu ya kula, kula kupita kiasi, kusahahu sahau na hasira. Kwa kweli ni vigumu kueleza maumivu yote apatayo mgonjwa wa vidonda vya tumbo hasa kwa mwenye vidonda sugu kwani hakuna hata kiungo kimoja mwilini atakachokuambia ni kizima.

VIPIMO NA MATIBABU YA UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)


Utambuzi wa kubainisha vidonda vya tumbo hufanyika hospitalini kwa kutumia mionzi au X-Ray,Upimaji wa tumbo na vilivyomo ndani yake unaweza pia kufanywa na njia inayojulikana kama ‘endoskopi’ au ‘biopsi’, ambayo huyakinisha hali halisi ya ugonjwa ulivyo baada ya vipimo tiba ya vidonda vya tumbo hutolewa kulingana na chanzo kilichosababisha ugonjwa huo kama ni bacteria au matumizi ya dawa. Lengo kubwa ni kupunguza makali ya tindikali katika tumbo ili vidonda vipone au kuua bacteria wanaosababisha ugonjwa huu.

 1. Dawa za Kuua bacteria (antibiotics) wa H. pyroli

Kama daktari atagundua kuwepo wa bacteria wa aina aina ya H. pyroli katika mfumo wako wa uyeyushaji chakula, atakuandikia mchanganyiko wa dawa za kuua bacteria hao ambazo utazitumia kwa kipindi cha angalau wiki mbili pamoja na dawa nyingine za kupunguza tindikali katika tumbo.

 2. Dawa za kuzuia utengenezaji wa tindikali na kusaidia uponyaji

Dawa hizi ambazo huitwa Proton Pump Inhibitors (PPIs) hupunguza tindikali katika tumbo kwa kuzuia ufanyaji kazi wa seli zinazohusika katika kutengeneza tindikali. Dawa hizi ni kama omeprazole (Prilosec), lansoprazole (Prevacid), rabeprazole (Aciphex), esomeprazole (Nexium) na pantoprazole (Protonix).

3. Dawa za kupunguza utengenezaji wa tindikali

Dawa hizi huitwa acid blockers au histamine (H-2) blockers. Hizi ni dawa zinazofanya kazi kwa kupunguza kiwango cha tindikali itakayoingizwa kwenye mfumo wa uyeyushaji chakula hivyo kupunguza maumivu na kusaidia uponyaji. Mfano wa dawa hizi ni ranitidine (Zantac), famotidine (Pepcid), cimetidine (Tagamet) na nizatidine (Axid).

 4. Matumizi ya antacids kupunguza makali ya tindikali

Dawa hizi hupunguza makali ya tindikali ambayo tayari ipo ndani ya tumbo na kumpa mgonjwa nafuu ya mara moja. Dawa hizi si za kuponya ugonjwa huu bali kukupa nafuu ya muda mfupi tu.

 5. Dawa za kulinda kuta za mfuko wa tumbo na utumbo mwembamba

Wakati mwingine daktari anaweza kukupa dawa za kulinda kuta za tumbo lako na utumbo mwembamba. Dawa hizi huitwa cytoprotective agents, nazo ni kama sucralfate (Carafate), misoprostol (Cytotec) na bismuth subsalicylate (Pepto-Bismol).

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA ILI UWEZE KUPONA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)


Kawaida ili uweze kupona vidonda vya tumbo, mara nyingi ni lazima kupunguza uzalishaji wa asidi tumboni au mwilini kwa ujumla.

Matibabu ya vidonda vya tumbo hujumuisha lishe na kubadilisha mitindo ya maisha na kutumia dawa maalumu.

Ikiwa matatizo kama kuvuja damu au vitobo sehemu ya kidonda yatatokea, basi hapo upasuaji huwa ni muhimu.

Vidonda vya tumbo kwa ujumla hupona ndani ya wiki 4 mpaka 6 za matibabu. Pia unashauriwa kufanya yafuatayo katika kujitibu au kujikinga na vidonda vya tumbo:

Moja; Punguza haidrokloriki asidi:

Kama tulivyoona kule mwanzoni kuwa moja ya sababu ya kutokea kwa vidonda vya tumbo mwilini ni uzarishwaji wa haidrokloriki asidi ambayo huzalishwa tumboni dakika chache kabla hujaanza kula chakula ili kuuandaa na kuusaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. HAIDROKLORIKI ASIDI hii ni lazima ipunguzwe makali (must be neutralized) kabla hujameza chakula, kwa kunywa maji kikombe kimoja au viwili nusu saa kabla ya kula chakula. Kwahiyo kama umepanga kuwa saa saba kamili mchana ndiyo utakula chakula cha mchana, basi saa sita na nusu unywe maji vikombe viwili. Kwa kufanya hivi kila mara kabla ya kula basi hakuna vidonda vya tumbo utakavyovipata kama matokeo ya hii haidrokloriki asidi.

Mbili; Pata usingizi wa kutosha:

Ukosefu wa usingizi ni maradhi makubwa katika zama zetu hizi. Haraka na pilikapilika za dunia yetu ya kisasa hazina mfano. Mvurugiko wa mawazo kutokana na mwenendo wa maisha uko kila mahali. Kutokana na mahitaji ya maisha, kuna idadi kubwa ya watu ambao neva zao hazitulii.

Kulala ni moja ya tiba za mwili. Usingizi husaga chakula na huondoa uvimbe katika tumbo, udhaifu na uchovu.

Kukesha usiku kucha husababisha kutosagika kwa chakula tumboni na hudhoofisha akili na pia husababisha akili kuvurugika. Kulala huleta pumziko kamilifu la mwili na akili.

Madaktari wetu wanasema kuwa, kulala ni muda ambao metaboliki ya mwili hufanyika polepole kiasi kwamba sehemu kubwa ya vyanzo vyake vya nishati hupatikana kwa ajili ya makuzi ya afya njema ya mwili na akili.

Sehemu ya kulala inatakiwa iwe ni tulivu na isiyo na kelele, pia iwe na hewa safi na asilia. Hewa asilia ina athari nzuri katika mwili wa mwanadamu, miongoni mwa athari zake ni kuiwezesha akili kufanya kazi barabara, na pia huongeza hamu ya kula.

Kiwango cha wastani cha kulala kinachotakiwa hutegemeana na umri. Katika umri wa miaka miwili, mtu hushauriwa kulala masaa 14 hadi 16 kwa siku. Miaka minne masaa 12 hadi 14 kwa siku, miaka sita hadi minane masaa 11 hadi 12 kwa siku, miaka minane hadi 11 masaa 10 hadi 11 kwa siku, miaka 14 hadi 18 masaa 8 hadi 9 kwa siku. Watu wazima wanahitaji saa za kulala kati ya sita na nane kwa siku.

Tatu; Dhibiti mfadhaiko:

Mbinu ya tatu katika kujikinga na kujitibu vidonda vya tumbo ni kujitahidi kwa kila namna kudhibiti mfadhaiko. Tambuwa kuwa kila mtu ana matatizo na kila mtu hufeli katika mipango yake na kila mtu hupata hasara. Tofauti ni kwamba wakati baadhi ya watu wanaweza kumudu kudhibiti mvurugiko wa mawazo, wengine hawajui kabisa nini cha kufanya na matokeo yake hupatwa na mfadhaiko ambao huweza kusababisha maradhi kama vidonda vya tumbo, maradhi ya moyo, n.k.

Mfadhaiko unaweza kuwa wa muda au wa kudumu. Matokeo yake yana madhara makubwa kama hautadhibitiwa. Ni vipi unaweza kudhibiti mfadhaiko wa akili utokanao na shida za maisha? Unachotakiwa kufanya ili kujidhibiti na mfadhaiko wa namna hii ni kuridhika na maisha.

Kama utakubali kuyapokea maisha kama yanavyokuja, ukaacha kuyakopa maisha ya jana na ukaacha kuhofu maisha ya kesho, ni hakika kabisa tumbo lako pia litatulia.

Inaelezwa na wataalamu kwamba karibu asilimia 50 ya wafanyabiashara wote duniani wanasumbuliwa na maradhi ya kutoridhika, kufunga choo, vidonda vya tumbo na maradhi ya moyo. Na wafanyabiashara ambao hawajui namna ya kupambana na wasiwasi au mashaka hufa wakiwa vijana.

Wasiwasi na hofu ya maisha humfanya yeyote kuwa mgonjwa. Mvurugiko wa hisia una matokeo chanya katika mwili, pia wasiwasi na hofu ya maisha huweza kuleta magonjwa yanayoweza kuuwa kabisa sawa sawa kama inavyotokea pia kwa magonjwa yale yatokanayo na lishe dhaifu. Baridi yabisi, maradhi ya moyo, tezi, kisukari, vidonda vya tumbo, kansa, yote yanaweza kusababishwa na mvurugiko wa mawazo.

Nne; Punguza au acha kabisa vinywaji na vyakula vifuatavyo:

Chai ya rangi, kahawa, pombe, soda, juisi za viwandani, sigara na tumbaku zote mpaka hapo utakapopona. Kama wewe ni mpenzi wa kunywa chai asubuhi au jioni basi sijasema usinywe chai, bali unachotakiwa kufanya ni kuchemsha maji yako ya chai na uiunge na ama tangawizi, mdalasini, au mchaimchai na uendelee na chai yako, kinachoepukwa hapa ni yale majani meusi ya chai ambayo ndani yake huwa na kaffeina na asidi nyingi na hivyo kuwa chanzo cha vidonda vya tumbo. Lakini pia tambuwa kuwa tangawizi peke yake ni dawa ya zaidi ya magonjwa 72 mwilini, hivyo unapokunywa chai ya tangawizi faida nyingine unayopata zaidi ya kuondoa njaa au kushiba ni dawa iliyomo ndani yake, hivyo unashiba huku unajitibu.

DAWA MBADALA ZA KUTIBU VIDONDA VYA TUMBO

Zifuatazo ni dawa mbadala zinazoweza kukutibu vidonda vya tumbo,Chagua dawa 3 kati ya hizi na uzitumie kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri haraka zaidi. Sasa usinywe zote wakati mmoja, moja tumia asubuhi, nyingine mchana na nyingine jioni. Kumbuka usitumie dawa yoyote bila uangalizi wa karibu wa daktari.

KABEJI



Kabeji ni moja ya dawa bora za asili zinazoweza kutibu vodonda vya tumbo. Kabeji inayo ‘lactic acid’ na husaidia kutengeneza amino asidi ambayo huhamasisha utiririkaji wa damu kwenda kwenye kuta za tumbo jambo linalosaidia kuuongezea nguvu ukuta wa tumbo na hatimaye kutibu vidonda vya tumbo.

Kabeji pia ina kiasi kingi cha vitamini C ambayo imethibitika kuwa na faida kubwa kwa watu wenye vidonda vya tumbo vilivyosababishwa na maambukizi ya bakteria aitwaye ‘H. pylori. Pia majaribio yamethibitisha kuwa juisi ya karoti freshi inayo vitamini U mhimu kwa ajili ya kudhibiti vidonda vya tumbo.

*Kata kabeji nzima mara mbili na uchukuwe nusu yake, chukuwa karoti mbili na ukatekate vipande vidogo vidogo na utumbukize vyote kabeji na karoti kwenye blenda na uvisage ili kupata juisi yake.

*Kunywa kikombe kimoja cha juisi hii kila nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni na kikombe kimoja kabla hujaingia kulala.

*Rudia zoezi hili kila siku kwa wiki kadhaa na hakikisha unatumia juisi freshi pekee na siyo ukanunue juisi ya kabeji au karoti ya dukani.

NDIZI

Ndizi zilizoiva na hata ambazo hazijaiva zote ni nzuri kwa ajili ya kudhibiti vidonda vya tumbo. Kuna aina maalumu ya muunganiko wa vimeng’enya vilivyomo kwenye ndizi ambavyo huzuia kuongezeka au kuzaliana kwa bakteria wa vidonda vya tumbo ‘H. Pylori’.

Ndizi pia huulinda mfumo wa kuta za tumbo kwa kuiondoa asidi iliyozidi tumboni na hivyo kusaidia kuuondoa uvimbe au vidonda tumboni na pia kuuongezea nguvu ukuta wa tumbo.

Ili kutibu vidonda vya tumbo, kula walau ndizi zilizoiva 3 kwa siku.

Au menya ndizi 2 au 3 na uzikate katika vipande vidogo vyembamba (slices) na uanike juani mpaka zikauke kabisa. Kisha saga vipande hivyo ili kupata unga na uchanganye vijiko vikubwa viwili vya unga huu na kijiko kikubwa kimoja cha asali na ulambe mchanganyiko huu mara 3 kwa siku kwa wiki 2 hivi.

UNGA WA MAJANI YA MLONGE

Mlonge ni mti mhimu sana katika utabibu kama tiba mbadala, majani, maua, mbegu na mizizi yake hutumika sana katika kutibu magonjwa mbalimbali. Mlonge una kiasi kingi cha vitamin C, Madini ya chuma, protini, Vitamini A na potasiamu.

Ongeza kijiko kimoja cha chakula kwenye bakuli ya mboga unapokula chakula cha mchana na jioni. Unaweza pia kunywa unga huu wa mlonge pamoja na juisi au unaweza kuuchanganya kwenye chakula kama vile wali na hivyo ukajiongezea kinga zako dhidi ya vidonda vya tumbo.

ASALI MBICHI


Asali mbichi, ile nzuri kabisa ambayo haijachakachuliwa inao uwezo mkubwa katika kutibu vidonda vya tumbo. Kama ujuavyo asali ni dawa karibu kwa kila ugonjwa. Kuna kimeng’enya kilichomo kwenye asali kijulikanacho kama ‘glucose oxidase’ ambacho huizalisha ‘hydrogen peroxide’ ambayo yenyewe inayo uwezo wa kuuwa bakteria wabaya mwilini ambao husababisha vidonda vya tumbo. Pia hii ‘glucose oxidase’ huulainisha ukuta wa tumbo na kupunguza muwako au vidonda tumboni.



Lamba vijiko vikubwa viwili kutwa mara tatu au vijiko vikubwa vitatu kutwa mara mbili. Itasaidia kusafisha tumbo, itaimarisha ukuta wa tumbo na kuzuia na kutibu vidonda vya tumbo. Fanya hivi kwa wiki 3 hadi 4. Hakikisha unapata asali mbichi salama ambayo haijachakachuliwa.

 NAZI

Nazi ni nzuri sana katika kutibu vidonda vya tumbo sababu ya sifa yake na uwezo wa kuua bakteria. Nazi huziua bakteria zinazosababisha vidonda vya tumbo. Pia tui la nazi na maji ya nazi (dafu) vyote vina sifa na uwezo wa kutibu vidonda vya tumbo.

Kunywa vikombe kadhaa vya tui freshi la nazi au maji ya nazi kila siku. Pia unaweza kuitafuana nazi yenyewe mara kwa mara. Fuatisha mlolongo huu walau kwa wiki 2 ili kupata matokeo chanya.

Au kunywa kijiko kikubwa kimoja cha mafuta ya asili ya nazi asubuhi kabisa na kingine usiku kwa wiki 2 hivi.


JIBINI NGUMU ILIYOSAGWA(GRATED CHEESE)

Kula jibini ngumu husaidia kufunika vidonda vya tumbo hivyo hupunguza maumivu makali ya vidonda kwa hiyo iliwe kwa wingi na mtu mwenye tatizo hili na kwa wale ambao vidonda vyao vina muda mfupi tangu kujitokeza hupotea baada ya muda mrefu wa matumizi ya mara kwa mara ya chakula hiki.

UWATU

Uwatu unajulikana sana kwa uwezo wake wa kutibu maradhi mengi mwilini. Unaweza pia kuutumia katika kutibu vidonda vya tumbo. Kwakuwa uwatu inayo gundi maalumu au ulimbo ambayo huulinda ukuta wa tumbo kwa kuufunga au kuufunika kama utando na hivyo kurahisisha hatua za kutibu vidonda vya tumbo.

Chemsha mbegu za uwatu kijiko kidogo cha chai ndani ya vikombe viwili vya maji, chuja na uongeze asali kidogo na unywe kwa pamoja kutwa mara 2 kwa wiki 2 au zaidi.

Unaweza pia kutumia kijiko kidogo kimoja cha chai cha unga wa mbegu za uwatu ukichanganya kwenye kikombe cha maziwa ya moto.

Au unaweza kuchemsha kikombe kimoja cha majani freshi ya uwatu, ongeza asali kidogo na unywe mara 2 kwa siku kwa wiki 2 au zaidi.

Ingawa maziwa hayashauriwi sana kutumika kwa mtu mwenye vidonda vya tumbo, hivyo unaweza kutumia maji ya uvuguvugu badala ya maziwa kama vidonda vyako vimeshakuwa sugu sana au ikiwa unahitaji upate nafuu ya haraka na hatimaye kupona.

KITUNGUU SWAUMU

Kitunguu swaumu pia husaidia kutibu vidonda vya tumbo. Watafiti katika kituo cha utafiti wa kansa cha Fred Hutchinson Cancer Research Center in Seattle waligundua kuwa uwezo ambao kitunguu swaumu kinaweza kudhibiti na kuua bakteria mbalimbali mwilini pia kudhiti bakteria anayesababisha vidonda vya tumbo ajulikanaye kama Helicobacter Pylori (H. pylori).

Chukuwa punje 6 za kitunguu swaumu, menya na ukate vipande vidogo vidogo kisha umeze pamoja na maji vikombe viwili kutwa mara 1 kwa wiki 2 au 3

MKAA WA KIFUU CHA NAZI

Mkaa pia hutibu vidonda vya tumbo hasa mkaa utokanao na vifuu vya nazi. Chukua vifuu vya nazi vitano au kumi vilivyokauka, viweke juu ya jiko la mkaa au popote na uvichome moto, mwishoni chukua mkaa wake usage kupata unga, kisha chota kijiko kikubwa kimoja na uweke ndani ya kikombe kimoja cha maji changanya vizuri na unywe kutwa mara 3 kwa wiki 2 au 3.

MAJI

Tiba hii inafaa kwa kutibu vidonda vya tumbo vilivyo katika hatua za awali.
Mgonjwa anapaswa kunywa lita moja ya maji masafi na salama alfajiri kabla ya jua kuchomoza na kabla hajakisafisha kinywa chake wala kunawa uso au kupata kifungua kinywa.  Kisha mgonjwa anapaswa kusubiri kwa dakika 45 kabla ya kupata chakula cha mchana na asinywe maji yoyote baada ya kula chakula hicho cha mchana kwa dakika 45
Wakati wa usiku mgonjwa anapaswa kunywa maji lita dakika 45 kabla ya kula chakula cha usiku na akae dakika 45 kabla ya kwenda kulala.
Tiba hii huchukua muda wa siku kumi mpaka mwezi mmoja kabla ya kupata nafuu.  Katika kipindi hiki chote mgonjwa anapaswa kuzingatia masharti juu ya ulaji na vitu vya kuepukwa.

MADHARA YA UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)

 Madhara ya ugonjwa huu ni mengi sana na miongoni mwa madhara ya ugonjwa huu ni
Kupata matatizo Wakati Wa Kumeza: Mtu mwenye vidonda vya tumbo hupata matatizo pale anapojaribu kumeza chakula au hujisika vibaya mara baada ya kupata chakula
Kutapika kabla na baada ya kula
Kupata tatizo la upungufu wa nguvu za kiume 
Kukonda kutokana na kukosa hamu ya kula chakula
Kutapika damu na kupata choo kilichochanganyikana na damu nyeusi



MATIBABU YA UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama wewe ni mgonjwa wa vidonda vya tumbo(peptic ulcers)na umejaribu njia hizo hapo juu bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kutibu ugonjwa wa vidonda vya tumbo (peptic ulcers) na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

0 comments:

FAHAMU CHANZO NA TIBA YA KUTOKWA NA HARUFU MBAYA UKENI






FAHAMU CHANZO NA TIBA YA TATIZO LA kUTOKA HARUFU MBAYA UKENI


Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, Ni matumaini yetu unaendelea vyema mpendwa msomaji wetu,leo tutajadili mada hiyo hapo juu ambayo ni miongoni mwa matatizo yanayotusumbua katika jamii tunayoishi
Tatizo la kutokwa na harufu mbaya ukeni ni moja ya matatizo yanayowasumbua wanawake wengi nchini na ni tatizo linalokera na gumu kuongeleka kutokana na wanawake wengi kuona aibu na kuhisi ni hali mbaya kwa mtu mwingine kuifahamu. 
Kutunza uke na kulinda afya ya uke ni jambo la muhimu sana kwa mwanamke, kutokwa na harufu mbaya ukeni ni kiashiria kwamba unaumwa na hayuko sawa. Hali hii inaweza kuathiri heshima ya mwanamke na pia mahusiano na mwenza wake.
Harufu mbaya ukeni kwa kiasi kikubwa husababishwa na bacteria wa vaginosis japo siyo kila mara ndio maana kuna umuhimu wa kutafuta chanzo cha tatizo la kunuka uke. Kama wewe muhanga wa tatizo hili basi tambua kwamba kuna njia za asili unaweza kuzitumia ikiwemo lishe na ukarudi katika hali ya kawaida,kama tatizo litazidi kuendelea basi itatakiwa uende hospitali ili upate uchunguzi.
Ni kawaida kwa mwanamke kupata harufu ukeni kutokana na hali ya uke kujisafisha kutoa vimelea wabaya. Lakini pale harufu inapokuwa kali sana mfano wa harufu ya shombo ya samaki basi ujue kuna tatizo kubwa. Kutokwa na harufu mbaya ukeni huwa inaambatana na dalili zingine kama kuwasha na kuchomachoma na kutokwa na majimaji au uchafu kama mtindi ukeni.

VISABABISHI NA VYANZO VYA TATIZO LA KUTOA HARUFU MBAYA UKENI

UKUAJI WA BACTERIA WA VAGINOSIS

Miongoni mwa sababu kuu ya kupata harufu mbaya ukeni ni ukuaji wa bacteria wa vaginosis,ukuaji wa bacteria usio wa kawaida kwenye uke husababishwa na kubadilika kwa mazingira ya ukeni na kushuka kwa kinga
 bacteria vaginosis ni chanzo namba moja kinachosababisha uke kutoa harufu mbaya.
Inawezekana ukawa msafi mpaka mwisho lakini ukisumbuliwa na hili tatizo basi lazima uke wako utatoa harufu mbaya.
Kila uke una bacteria ambao wapo naturally kwa ajili ya afya njema ya uke wako,Lakini kama ikitokea hawa Bacteria wakazidi na kuwa wengi kupita kiasi ambacho uke wako unaweza kuhimili ndipo tatizo hili hutokea

Sababu zinazosababisha bacteria vaginosis hazijulikani kwa usahihi lakini madaktari wanasema inaweza ikasababishwa na kitendo cha kupeana Raha na Utamu bila condom na hasa  kama vitu vilivyoingia kwenye uke wako wakati wa kupeana Raha na Utamu vilikuwa vichafu(mfano vidole au uume au dildo nk),lakini pia tatizo hili la ukuaji wa bacteria vaginosis hutokea bila sababu.

Ukitaka Kujua kuwa unasumbuliwa na bacterial vaginosis utajikuta unapata Dalili zifuatazo;

Uke kutoa maji maji mazito au mepesi yenye rangi ya njano au brown yenye harufu mbaya
Maumivu kwenye maeneo ya kiuno au nyonga
Unaweza usipate au ukapata maumivu ya kichwa.
Uke wako unaweza ukawa unawashwa au usiwashwe
Pia Ukuaji wa bacteria wa vaginosis ndani ya uke wanaweza kupelekea mimba kutoka, kujifungua kabla ya wakati na kuongezeka kwa hatari ya kupata magonjwa mengine ya ngono. dalili mojawapo ya kwamba tayari una maambukizi ya bacteria ni kutokwa na uchafu unaoambatana na harufu kali mfano wa harufu ya samaki wabichi


UGONJWA WA TRICHOMONIASIS

Trichomoniasis ni moja ya ugonjwa wa ngono unaosababisha harufu kali ukeni. Ugonjwa huu husababishwa vimelea na huambatana na kutokwa na uchafu ukeni,kuwasha, na maumivu makali wakati wa kukojoa. trichomoniasis inaweza kuwaathiri wajawazito na kuleta hatari ya mimba kutoka. Kama utagundua una Trichomoniasisi basi wewe na mwenza wako mnatakiwa kutibiwa. Hakikisha pia unatumia condom vizuri kila unapofanya ngono kama kinga dhidi ya magonjwa

MABADILIKO YA HOMONI

Mabadiliko ya homoni kutokana na mzunguko wa hedhi huweza kuchangia harufu mbaya ukeni,wanawake wanaokaribia kukoma hedhi wako kwenye hatari zaidi kwani homoni ya estrogen hupungua sana hivyo kusababisha tishu kuwa na tindikali kidogo

YEASTS INFECTIONS

Hili Pia ni Tatizo,lipo kama la Bacterial Vaginosis.tofauti yake ni kuwa kwenye Bacterial Vaginosis waliokuwa wamezidi ni bacteria lakini huku wanaozidi ni fungus candida albicans.
Ni wanawake wachache huwa wanapata Bacterial Vaginosis lakini wanawake wengi lazima wapate Yeast infection japo mara moja katika maisha yao.

Mara nyingi yeasts infection hutokea tu au inaweza kusababishwa na aina ya vyakula au vinywaji unavyokula au kunywa hasa kama vimejaa yeast(vyakula vyote vinavyotengenezwa na hamira,pombe etc)
Ukitaka kujua kama unasumbuliwa na yeast infection utajikuta unapata Dalili zifuatazo;

Uke wako ukawa unawashwa au usiwashwe
Maumivu kama uke unaungua pale unapokuwa unajisaidia haja ndogo
Uke kutoa maji maji mazito yenye rangi nyeupe kama jibini


KUTOZINGATIA USAFI 

Ni wazi kwamba uchafu na kuwepo kwa unyevunyevu sehemu za siri huzalisha harufu mbaya. Kisayansi ni kwamba tezi zilizopo ndani ya mwili (apocrine sweat glands )hutengeneza mafuta kuelekea kwenye maeneo kama kwapa, pua, ndani ya sikio, uke, na kwenye chuchu, bacteria waliopo maeneo hayo huchakata mafuta haya na hivo kuzalisha harufu kali. Uvaaji wa nguo zilizobana na uzito kupita kiasi huchangia kuhifadhiwa kwa jasho kwenye mikunjo ya ngozi na hivo kuleta harufu.

VAGINAL/CERVICAL CANCER(KANSA YA UKE/KANSA YA MLANGO WA KIZAZI)

Unapokuwa una kansa ya uke au kansa ya mlango wa kizazi ni kawaida kutokwa na maji maji yenye harufu mbaya ambayo ni sehemu ya dalili za kansa ya uke,.Unapojiona kuwa una tatizo la uke kutoa harufu mbaya,ni heri na itakuwa busara ukienda hospitali,kupima na kama ni kansa ya mlango wa kizazi itakuwa sio ngumu kuitibu kama ukiwahi mapema kuanza matibabu


  • KUVAA PEDI MOJA MUDA MREFU

Pedi inapovaliwa kwa muda mrefu husababisha ngozi kucharuka,kututumka na kuwasha na pia kuchangiwa kukua kwa bacteria na fangasi wabaya ambao ni chanzo cha harufu..

MATIBABU 
Matibabu ya tatizo hili hupatikana katika hospital zote nchini na matibabu hutolewa baada ya vipimo vya kitaalamu kuchukuliwa na daktar au nesi mwenye uzoefu wa kutosha juu ya magonjwa ya wanawake
Dawa za kupaka(ointment/cream) na Dawa za kumeza (pills) huweza kumaliza tatizo hili
 Kumbuka: Ni makosa kutumia dawa bila kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa daktari au nesi

MAMBO 6 UNAYOWEZA KUFANYA KUPUNGUZA UWEZEKANO WA KUPATA TATIZO LA KUTOKWA NA HARUFU MBAYA UKENI

  1. Siku zote vaa nguo za ndani zisizobana sana na za pamba
Nguo zilizobana zinazuia kupita kwa hewa safi kuelekea ukeni na hivo kusababisha unyevunyevu ambao ni mbolea kwa bacteria na fangasi wanaoleta harufu mbaya kwenye uke. Hakikisha unabadilisha chupi kila baada ya masaa 12 inasaidia kuzuia kukua kwa bacteria wabaya.
2.Badili Nguzo zako Kila Baada ya Kufanya Mazoezi
Nguo zenye unyevu ni mbolea nzuri kwa ukuaji wa bacteria hivo hakikisha unavaa nguo zilizokauka na kubadilisha kila baada ya kutoka mazoezini.
  1. Punguza uzito kama Inawezekana
Uzito mkubwa unakufanya utokwe na jasho kwa wingi zaidi hasa kwenye uke. Na kama tulivojifunza pale juu, jasho na unyevunyevu  inaleta fangasi na bacteria wabaya.
  1. Epuka Kuflash Uke Kila Mara (Douching)
Kusafisha uke kila mara hasa kwa kutumia kemikali na sabuni inaharibu mazingira ya bacteria wazuri ambao ni walinzi, na hivo kuacha nafasi kwa uke kushambuliwa na bacteria wabaya pamoja na bacteria wa vaginosis
  1. Epuka Kutumia Spray na Marashi ili Kuondoa Harufu Mbaya Ukeni au Kuweka Harufu Nzuri Ukeni.
    Ukweli ni kwamba ngozi ya uke ni laini sana kwa hiyo inanyonya kwa urahisi kemikali zilizopo kwenye spray kuingia kwenye damu. Usiingie kwenye mtego huu, kumbuka miili yetu imeumbwa kujisafisha yenyewe, Pale unapoongeza kitu cha ziada basi unaharibu normal flora na kuharibu kinga ya mwili.
  2. Epuka Baadhi ya Vyakula Ambavyo ni Adui wa afya yako
    Kuna aina nyingi ya vyakula ambavyo vinaweza kukuathiri wewe kama mwanamke kwenye swala la uzazi, vyakula hivi vinaharibu mazingira ya uke, kuua bacteria wzuri na kubadili PH. Vyakula vyenye sukari, Pombe, ngano na vyakula vilivyosindikwa huchochea ukuaji wa bacteria wa vaginosis.

MAMBO YA KUFANYA ILI KUKATA HARUFU MBAYA UKENI

Harufu kali kwenye uke mara nyingi inagundulika zaidi baada ya kufanya ngono na pia kwenye hedhi. kwahiyo badala ya kukimbilia spray na kujisafisha ukeni ili kuondoa harufu tumia njia zifuatazo kwa muda kabla hujamuona dactari wako ama kupata Dawa za kutumia

APPLE CIDER VINEGAR (SIKI YA TUFAA

Vinegar imejaa viini ambavyo ni antibacterial na antiseptic ambavyo vitakusaidia kupambana na harufu hii kali. Chukua kiasi kidogo cha vinegar changanya na maji kwa uwiano wa 1/10  na uoshe eneo la uke. Tumia pia kiasi kingine kwa uwiano huo huo changanya na maji ya kunywa chukua glass moja kwa vijiko viwili vya apple cider vinegar na unywe kila siku.... NB siyo kila vinegar itakusaidia hakikisha unatumia Apple cider vinegar. 

MBEGU ZA UWATU(FENUGREEK SEEDS)
Loweka kijiko kidogo cha mbegu za uwatu (fenugreek seeds) ndani ya maji glasi moja na uache kwa usiku mzima. Kesho yake asubuhi maji haya yaliyolowekwa mbegu za uwatu kabla ya kula au kunywa chochote.
Uwatu husaidia kuweka sawa homoni za mwili na kuweka sawa mzunguko wa hedhi.

BAKING SODA(MAGADI SODA)
Baking soda inaweza kutumika ili kubalansi pH kwenye mwili. Kumbuka mwanzo tulivosoma kuhusu madhara ya kubadilika kwa pH. Ukibalansi pH basi tatizo la harufu kali linakuwa limeisha. Unaweza kutumia pia baking soda kama body spray na ukaepuka kujaza sumu mwilini. Chukua nusu kikombe cha baking soda weka kwenye beseni kubwa la maji ya kuoga kisha kaa tulia kwa dakika 15 mpaka 20 kwenye maji. Baada ya hapo Jifute kwa taulo sehemu zote usiache unyevu kabla ya kuvaa nguo

MAZIWA MTINDI
Chukua mtindi ujazo wa kijiko kidogo cha chai na tumbukize ndani ya uke wako na uache huko usiku mzima. Mtindi una bakteria wazuri wanaohitajika ukeni kuweka sawa usawa wa PH (alikalini na asidi) na hivyo kuondoa maambukizi,Pia unashauriwa kunywa maziwa mtindi mara mbili kwa siku kuongeza kinga ya mwili wako kwa ujumla dhidi ya magonjwa mbalimbali

MATUNDA NA MBOGAMBOGA

Matunda yenye uchachu mfano machungwa, mapera na strawberries yana Vitamn C kwa wingi sana ambayo huimarisha kinga ya mwili na kusaidia utoaji wa sumu mwilini. Chakula kama Parachichi na mboga za kijani ina Vitamn B6 na madini ya potasium ambayo huongeza hamu ya tendo la ndoa na kujenga kuta za uke hivo kuzuia hatari ya kushambuliwa mara kwa mara

KITUNGUU SAUMU
Kitunguu saumu kinafahamika tokea miaka ya zamani kwa uwezo wake mkubwa wa kuimarisha kinga na kupambana na maambukiz ya bacteria na fangasi. Unaweza kula punje 6-10 za vitunguu saumu kwa siku ama ukatengeneza juice ya vitunguu saumu ukawa unakunywa asubuhi kabla ya kula chochote

KARANGA/ALIZETI NA MBEGU ZA MABOGA
Matumizi ya karanga na mbegu kwenye mlo wako wa kila siku huzuia kukauka kwa uke kwa sababu kuna Vitamin E kwa wingi. Unaweza kutafuna mbegu za maboga,karanga, na alizeti kila siku kuweza kujitibu na kujikinga dhidi ya tatizo hili


MATIBABU YA TATIZO LA KUTOA HARUFU MBAYA UKENI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo la kutoa harufu mbaya ukeni na umejaribu njia hizo hapo juu bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tuna Dawa za kuondoa tatizo la kutoka harufu mbaya ukeni na Dawa za kila ugonjwa karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

1 comments:

Copyright © 2017 Green health consultation centre