FAHAMU TATIZO lA HOFU NA WASIWASI ULIOPITILIZA (ANXIETY DISORDERS)



Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, Ni matumaini yetu unaendelea vyema mpendwa msomaji wetu,
Tunakuombea afya njema zaidi wewe pamoja na familia yako na wote unaowapenda
MWENYEZIMUNGU MTUKUFU AZIDI KUWAHIFADHI NA KUWAJAALIA REHMA ZAKE 
AMEEN!

Naam leo nimeona ni khery tukaongelea juu ya mada hapo juu kutokana na athari tunayoiona katika jamii zetu kwa watu wengi kuathirika kisaikolojia kwa kukosa uwezo wa kujiamini kwa kuathirika kwao kwa tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza,mathalani ni kitu cha kawaida mtu kupata wasiwasi au hofu pale anapopatwa na changamoto za kimaisha kwa kushindwa kupata ajira, kushindwa kufaulu shuleni, kusalitiwa ama kukosana na mpenzi wake,kufiwa,kufilisika,kuhofia usalama wa maisha yake na kadhalika  lakini endapo wasiwasi na hofu vikakufanya ushindwe kumudu maisha yako ya kawaida kama unavyopenda, hapo ndipo tunasema mhusika Ana tatizo la wasiwasi na hofu kupitiliza ( anxiety disorder/ugonjwa wa hofu na wasiwasi)

Kuna aina nyingi za tatizo la kuwa na wasiwasi na hofu kupitiliza (anxiety disorders)  na njia nyingi za kutibu au kumfanya mtu ajisaidie. Ukishakuwa umelijua tatizo lako hili la wasiwasi na hofu kupitiliza (anxiety disorder) kuna hatua za kuchukua ili kupunguza dalili zake au kurudisha udhibiti wa maisha yako hivyo usijali sana iwapo unasumbuliwa na hill tatizo


JE, TATIZO LA HOFU NA WASIWASI ULIOPITILIZA (ANXIETY DISORDERS) NI NINI?


Wasiwasi au hofu unaweza kuelezewa kuwa ni mwitiko wa mwili wako kwa vitu hatarishi kwa maisha yako vinavyokuja au unavyofikiria vinaweza kuja.
Wasiwasi unahusiana sana na hofu ambayo ni mwitiko wa mwili wako kukujulisha kuhusu hatari halisi (hatari iliyo mbele yako) au inayofahamika kuja siku za karibuni.
Hivyo Hofu na wasiwasi uliopitiliza ni hali ya ugonjwa wa kiakili ambao unamfanya muhusika kua na hofu muda wote na kukosa utulivu wa akili na hata kushindwa kutoa maamuzi.

Mfumo wa ubongo hudhibiti mwitiko huu wa mwili wa kupambana au kuyakimbia mazingira hatarishi, na mara nyingi huambatana na kupanuka kwa mboni za macho, kuongezeka kwa kasi ya mapigo ya moyo, na kuongezeka kwa jasho/uhemaji.

Mwitiko wa wasiwasi unaweza kuambatana na uangalifu zaidi wa mazingira na kukaza kwa misuli tayari kuikabili hatari.
Wasiwasi unaweza kuwa na manufaa, kama kuongeza ufanisi na kufanya vizuri zaidi kwenye michezo, au kuzungumza mbele ya kadamnasi. Pamoja na kuwa hii ni miitiko ya kawaida ya mwili na mara nyingi ni miitiko yenye manufaa wakati wa hatari, wasiwasi unaweza kuwa na athari endapo utazidi kiwango au ukiendelea kuwepo bila ya kuwepo kwa hatari
Wasiwasi mwingi uliokithiri(kupitiliza) unaweza kukukosesha raha, na kuharibu utendaji wako wa kazi, na huu ndio huitwa ugonjwa wa hofu na wasiwasi uliopitiliza (anxiety disorder)
Lakini pia tatizo hili lipo katika namna au aina nyingi.

Aina ZA HOFU NA WASIWASI ULIOPITILIZA (ANXIETY disorders)

Tatizo la hofu na wasiwasi mwingi uliopitiliza (anxiety disorders)hutofautishwa kufuatana na aina ya kitu au mazingira yanayosababisha woga na wasiwasi, pamoja na namna ya fikra anazokuwa nazo mtu akishikwa na hofu au wasiwasi.
Lakini Kusudi mtu aitwe ana tatizo hili, hofu na wasiwasi lazima viwe vya muda mrefu, vilivyodumu miezi 6 au zaidi.
Matatizo ya kuwa na wasiwasi kwa kawaida huanza utotoni lakini hudumu ukubwani.

Aina ya tatizo la kuwa na hofu na wasiwasi kupitiliza (anxiety disorder ni ;

Specific PHOBIAS ANXIETY DISORDERS
 Hii ni hali ya kuwa na hofu na wasiwasi uliokithiri kwa kuhofia kitu au mazingira fulani, mfano;kama buibui kuwa juu ya nyumba yako,kupanda ndege, au kukaa sehemu zilizofungwa Katika mambo ya kijamii.

SociAL PHOBIA/PERFORMANCE ANXIETY DISORDERS

Hii ni hali ambayo mtu anakuwa na wasiwasi na hofu kubwa kwa kuogopa kushiriki shughuli za kijamii, au mazingira yanayomfanya watu wamwone au kumjadili.

GENERALIZED ANXIETY DISORDERS(GAD)

 ni aina ya tatizo linalojitambulisha kwa mtu kuwa na wasiwasi na hofu kubwa inayodumu kwa kipindi kirefu inayotokana na maeneo tofauti ambayo ni vigumu kuyadhibiti.
Woga unaoendana na aina ya tatizo la wasiwasi aina ya GAD huathiri uwezo wa mtu wa kufikiri, kupata usingizi, au kufanya shughuli fulani.
 Dalili zake hujionyesha kwenye hisia na tabia na namna ya kufikiri ambavyo ni matokeo ya hali ya mwili kufikiria kuwa kuna hatari.
Ukiwa na aina hii ya wasiwasi GAD, utapata wasiwasi kutokana na vitu vinavyowapa wasiwasi watu wote, lakini wewe utaupeleka wasiwasi huo kwenye ngazi nyingine, ya juu zaidi
Mfano;
Mfanya kazi mwenzako akitoa maoni yake kuhusu hali ya uchumi kwako shida utaanza kufikiri sana na kuwa na hofu
rafiki yako asipotoa majibu kwa simu yako haraka, unaanza kufikiri kuwa mahusiano yenu si mazuri.
Wakati mwingine hata wazo tu la kuwa utashinda kazini kwako ni mwanzo wa wasiwasi. Unaendesha shughuli zako ukiwa umejaa hofu isiyobainika, na hata kama hakuna kitu cha kuanzisha hofu hizo.

Waweza kuwa unatambua kuwa wasiwasi wako unazidi hali halisi, au unaamini kuwa wasiwasi wako unakulinda kwa namna fulani, mwisho wake ni ule ule. Huwezi kuyafuta mawazo yanayokuletea wasiwasi. Yanazidi kutembea kichwani mwako, yakijirudiarudia  bila kufika mwisho.

SEPARATION ANXIETY DISORDERS
Imezoeleka kuona watoto wadogo ndio wao  pekee ambao huhisi hofu au wasiwasi wakati mtu wanayempenda anaondoka,lakini kumbe Mtu yeyote anaweza kupata hofu na wasiwasi na kujitenga kwa kuwaza au kuhofia juu ya mtu wao wa karibu kua kuna tatizo linaweza kumtokea.

SELECTIVE MUTISM ANXIETY DISORDERS
Hii ni aina ya hofu na wasiwasi wa kijamii ambao watoto wadogo au watu wakubwa ambao huongea kawaida na familia zao lakini wanakua na hofu na wasiwasi yani hawawezi kuzungumza hadharani kama shuleni,kazini nk
Yani kushindwa kuzungumza kwenye baadhi ya mazingira ya watu wengi kama shuleni,kazini nk

AGORAPHOBIA ANXIETY DISORDERS
Hii ni aina ya hofu au wasiwasi uliopitiliza ambao humfanya mtu kuogopa sana kuwa katika mahali ambapo inaonekana kuwa ngumu kutoroka au kupata msaada ikiwa dharura itatokea.
Mfano:
Unaweza kuwa na hofu au kuhisi kuwa na wasiwasi unapokuwa kwenye ndege, usafirishaji wa majini nk

PANIC ANXIETY DISORDERS
Hii ni aina ya wasiwasi au hofu kubwa ambayo inaleta shambulio la hofu Sana kwa ghafla linapotokea jambo unaweza kutokwa kwa jasho kuwa na maumivu ya kifua na kuwa na maumivu ya pigo la moyo wakati mwingine unaweza kuhisi ni kama unavunja au kuwa na mshtuko wa moyo kutokana na hofu kupitiliza

MEDICATION INDUCED ANXIETY DISORDERS
Baadhi ya dawa huweza kusababisha dalili fulani za hofu na wasiwasi
uliopitiliza


CHANZO CHA TATIZO LA HOFU NA WASIWASI ULIOPITILIZA (ANXIETY DISORDERS)

Hadi sasa hakujaweza kupatikana chanzo cha moja kwa moja kinachosababisha tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza,ila kuna mambo kadhaa yanaweza kuelezwa kuwa ni chanzo kutokana na ufuatiliaji wa chanzo kwa muda mrefu imeonesha kuwa tatizo la hofu na wasiwasi inaweza kurithiwa kutoka  katika familia yako pia vyanzo vingine vyenye kufikiriwa ni 
Baadhi ya magonjwa: Utafit unaonyesha kuwa kuna magonjwa yanayohusishwa kuwa ni chanzo cha mtu kupata tatizo la hofu na wasiwasi kupitiliza baadhi ya magonjwa hayo ni
KISUKARI, MAGONJWA YA MOYO, MAGONJWA YA MAPAFU,PUMU, MAGONJWA SUGU YA TUMBO, MAGONJWA YA TEZI YA THYROID nk

Matatizo ya ubongo. Utafiti unaonyesha tatizo la hofu na wasiwasi zinaweza kuhusishwa na mzunguko mbaya katika ubongo unaodhibiti woga na hisia

Mazingira. Hii inahusu matukio yanayomusumbua mtu ambayo ameona au kuishi kupitia matukio ya maisha mara nyingi huweza kuhusishwa na tatizo la hofu na wasiwasi ni pamoja na unyanyasaji wa watoto na kutelekezwa, kifo cha mpendwa, au kushambuliwa au kuona vurugu na kushuhudia baadhi ya matukio ya ajali yenye kuogopesha

Matumizi ya dawa. Dawa zingine zinaweza kutumiwa kuficha au kupunguza dalili fulani za wasiwasi. Shida ya wasiwasi mara nyingi huambatana na ulevi na matumizi ya sigara

Ni muhimu kupata uchunguzi kamili wa mwili ili kudhibiti hali zingine za matibabu wakati wa kuzungumza na daktari wako juu  tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza


DALILI ZA TATIZO LA HOFU NA WASIWASI ULIOPITILIZA (ANXIETY DISORDERS)
Dalili za kawaida kwa mtu mwenye tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza (anxiety disorders) ni pamoja na:

. Kutotulia yani kukukosa utulivu na kujaa wasiwasi
. Kuchoka kirahisi, kuwa mchovu;
. Hupata shida kutuliza mawazo kwenye kitu ambacho kinaweza kuonekana kuwa ni tatizo la kumbukumbu au la kawaida tu
. Kuwa na hisia dhaifu yan kuhisi kuwa ubongo unakuwa mtupu yani unashindwa kupata mawazo mazuri muda wote unajihisi kuhofu hatari 
. Kuwa na hasira za haraka
. Kukakamaa kwa misuli
. Kuumwa kichwa na kuwa na hofu kubwa
. Mapigo ya moyo kwenda mbio kupata shida kupumua
. Matatizo ya usingizi (kukosa usingizi)
. Kupata vidonda vya tumbo na kiungulia
. Kukosa ujasiri wa kupambana na changamoto
Wasiwasi unaohusiana na hofu ya kitu fulani (specific or simple phobia) au wasiwasi wa mambo ya kijamii (social phobia) unaweza kusababisha kuyakwepa mazingira fulani au kukuza dalili zinazoleta panic attack – hofu kubwa ya ghafla inayofikia kilele katika muda mfupi.

VIPIMO NA MATIBABU

Hatua ya kwanza ni kuonana na daktari wako ili kuhakikisha kuwa hakuna shida ya kiafya inayosababisha dalili za hofu na wasiwasi uliopitiliza.
Si kila mtu anayekuwa na wasiwasi sana ana tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza (anxiety disorder) Unaweza kuwa na wasiwasi kwa sababu ya kuwa na majukumu mengi,ratiba kali ya kazi, kukosa usingizi au mazoezi, msongo wa mawazo au majukumu ya ulezi wa familia  nyumbani, au kunywa kahawa kupita kiasi.
Lakini pia kama maisha yako si ya furaha na ni ya msongo wa mawazo na huzuni kila wakati, ni ishara tosha kuwa una tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza hivyo unahitajika kufika hospital kwa uchunguzi zaidi.
Kadhalika matibabu ya tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza hutegemea asili au chanzo cha tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza hivyo hutofautiana kutoka mtu mmoja hadi mwingine
Mara nyingi matibabu ya tatizo hili huchanganywa kutegemeana na hali ya mgonjwa jinsi ilivyo ambapo kuna matibabu ya dawa na ushauri nasaha ambao mgonjwa akipatiwa anaweza kupona pasipo kuhitajika kutumia dawa
Walakini, ikiwa njia ya ushauri haipunguzi athari za dalili za wasiwasi, au ikawa ni chanzo cha kuongeza mashambulizi ya mshtuko na wasiwasi wa ghafla yani dalili kuwa kali daktari wako atawajibika kukupatia huduma ya matibabu mengine yatakayojumisha dawa na ushauri nasaha.
Kadhalika Kuna matibabu ya tabia ya utambuzi (CBT) ambayo ni aina ya tiba ya kuongea, inaweza kumsaidia mtu kujifunza njia tofauti za fikra na kusaidia kuondoa wasiwasi pia dawa zinazotumika sana ni dawa za kupunguza wasiwasi (kwa ujumla zinatumika kwa kipindi kifupi tu) ambazo ni Antidepressants,anxiolytics,beta-blockers ambazo hutumiwa kwa matatizo ya moyo, wakati mwingine hutumiwa kudhibiti dalili za mwili za wasiwasi na mfadhaiko.


HATUA ZA KUFATA KUPAMBANA NA TATIZO LA HOFU NA WASIWASI ULIOPITILIZA (ANXIETY DISORDERS)
Mpendwa msomaji nina imaani ya kwamba umejifunza mambo mengi kuhusu tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza (anxiety disorders)
Napenda nihitimishe kwa kukupatia ufumbuzi wa kuweza kupambana na tatizo hili ukiwa una shaka au kuhofia kuwa unalo hili tatizo
Kwa kufanya yafuatayo unaweza kupunguza wasiwasi na kudhibiti dalili za hofu na wasiwasi uliopitiliza na kupunguza ukubwa wa tatizo


EPUKA KUKAA PEKE YAKO,JICHANGANYE NA WENGINE.
Upweke unaweza kukuletea au kukuongezea wasiwasi, jitahidi kuwa muwazi zungumzia matatizo yako kwa watu wako wa karibu na changamana nao ili uweze kujipunguzia hofu na kupata matumaini na kuwa ni mwenye kujiamini
Jitahidi kila wakati kukutana na marafiki zako, jiunge na vikundi vya kusaidiana, au mshirikishe mambo yanayokusumbua mtu umpendaye.
 Kama huna mtu wa namna hii, hujachelewa kuanza kujenga mahusiano mapya yenye kukujenga


DHIBITI MSONGO WA MAWAZO
Kama unasumbuliwa sana na msongo wa mawazo jitahidi kupata ushauri wa kuondokana na msongo wa mawazo au dawa zitakazokusaidia kuondokana na msongo wa mawazo kadhalika Unaweza pia kuona ni majukumu yapi ya kuyaacha, kuyapunguza au kuwaachia wengine ili yasiushughulishe ubongo wako kiasi cha kupata hofu na wasiwasi uliopitiliza (anxiety disorder)

JENGA TABIA YA KUFANYA MAZOEZI KILA SIKU
Kufanya mazoezi ya mwili ni njia ya asili ya kupunguza msongo wa mawazo na kuondoa wasiwasi pamoja na mfadhaiko
Ili Kupata matokeo bora kabisa, lenga kufanya mazoezi ya kuongeza mapigo ya moyo na kutoa jasho (aerobic exercises) kwa muda wa dakika 30 kila siku.
Mazoezi au shughuli za kuifanya mikono na miguu kuwa katika mwendo kwa wakati mmoja (rhythmic activities) ni ya manufaa sana. Jaribu kutembea, kukimbia, kuogelea, kucheza,kurukaruka nk itasaidia Kupunguza hatari na dalili za hofu na wasiwasi uliopitiliza

PATA USINGIZI WA KUTOSHA
Kukosa usingizi wa kutosha kunaweza kukuza tatizo la kuwa na wasiwasi kwa hiyo jitahidi kupata wasaa wa kulala masaa 8 hadi 9
Kulala usingizi mzuri ni miongoni mwa mambo yanayouweka mwili katika hali nzuri ya afya


JIAMINI NA PINGA(UKATAE) WASIWASI
Unapopatwa na hali ya  kuhofu au kuwa na wasiwasi uliopitiliza ikatae hiyo hali kwa kuamua kutoogopa kitu chochote jipatie ujasiri jiamini na ishinde hofu uliyonayo tena jitengenezee mkakati wa kufanya mambo yote ambayo unayapatia hofu hii itakusaidia kupambana na tatizo hili ambalo ni hatari kwa afya ya akili na mwili

EPUKA POMBE, SIGARA, MADAWA NA KAHAWA
Ikiwa unapambana na tatizo la kushinda wasiwasi, unatakiwa kupunguza au kuepuka kabisa matumizi ya pombe, kahawa,sigara na madawa ya kulevya kwasababu vitu hivi hasa pombe inafanya hali ya wasiwasi kuongezeka tofauti na kule kudhania kuwa inapunguza wasiwasi. Kadhalika na sigara inaonekana kama ni kitulizo bila ya kujua kua kuna sumu ya nikotini ambayo ndio kichocheo kikubwa cha kusababisha ongezeko la wasiwasi.
Unashauriwa iwapo una nia ya kupona tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza (anxiety disorders) epukana na matumizi ya vitu hivyo.


VIFAHAMU VYAKULA VYENYE KUSAIDIA KUONDOA WASIWASI
Ni vyema ukafaham kuwa kuna vyakula ambavyo ukila kwa wingi vinakusaidia kupunguza ukali wa dalili za tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza kutokana na uwezo wa vyakula hivyo kusaidia  ubongo kufanya kazi ipasavyo
Baadhi ya vyakula hivyo ni ÷
1)MAFUTA YA SAMAKI (FISH OIL)

Mafuta ya samaki yana faida nyingi sana katika mwili wa mwanadamu na yanasaidia kupunguza hofu na wasiwasi.
Hii ni kutokana na kua yana virutubishi ambavyo vinakuza afya ya ubongo, pamoja na vitamini D na asidi ya asidi ya omega-3 eicosapentaenoic acid (EPA) na asidi ya dosahexaenoic (DHA) 

EPA na DHA zinaweza kusaidia kudhibiti homoni na kemikali za neurotransmitters  na serotonin kuondoa tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza.


2)BINZARI NYEMBAMBA (TUMERIC)
 Unaweza ukastaajabu kusikia kiungo hiki kina uwezo wa Kupunguza na kuondoa tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza
Ukweli ni kwamba binzari nyembamba ina uwezo wa kupambana na Kupunguza dalili za hofu kwa Kusaidia ufanyaji kazi katika ubongo

3) CHOCOLATE NYEUSI
4)MAZIWA MGANDO
5)MBEGU ZA CHIA(CHIA SEEDS)
6)KOROSHO NA LOZI(CASHEWS NUTS&ALMONDS)
7) MATUNDA YENYE VITAMIN C NYINGI
8)MAYAI NA NYAMA



 TATIZO HILI LA ANXIETY DISORDERS NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo hili au ndugu yako ana hili tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza (anxiety disorder) na magonjwa mengine mbalimbali na mmejaribu njia kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)


Green health consultation center tutakufanyia uchunguzi kujua chanzo cha tatizo kisha tutakupatia ushauri au dawa za kuondoa tatizo la hofu na wasiwasi uliopitiliza (anxiety disorder)na tutakupatia ushauri sahihi wa kupambana na ugonjwa huo na magonjwa yote yanayokusumbua karibu sana ofisini kwetu tuweze kukuponya tatizo lako

NOTED;
Mpendwa msomaji iwapo wewe au ndugu yako ana tatizo hili fanya haraka ya kupata ufumbuzi wa Matibabu kwakua tatizo hili lina athari nyingi katika mfumo wa mwili 
Miongoni mwa madhara ya kuwa na tatizo hili la hofu na wasiwasi uliopitiliza ni kujiweka katika hatari ya kupata magonjwa mengine makubwa kama
KUPATA SHINIKIZO LA DAMU, MFADHAIKO,MATATIZO KATIKA MFUMO WA UPUMUAJI,KINGA YA MWILI HUSHUKA,KUKOSA USINGIZI,KUPATA MATATIZO KATIKA MFUMO WA MMENG'ENYO WA CHAKULA NK

Tunamuomba ALLAH HIFADHI NA SALAMA TUWE WENYE KUNUSURIKA NA MARADHI MAKUBWA 
AMEEN


Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )


MATIBABU YA TATIZO LA WANAWAKE KUTOKWA NDEVU NA VINYWELEO MWILINI (HIRSUTISM) 



Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, ni matumaini yangu unaendelea vyema mpendwa msomaji
Kwa upande wangu namshukuru Allah kariim kwa kunikirimu afya njema mimi pamoja na familia yangu na kuniwezesha kupata wasaa wa kuwajibika katika majukumu yangu

Naam ni jambo la kumshukuru Allah kuiona siku mpya kila siku haijalishi unaumwa ama una magumu unapitia USITAMANI KUFA KWANI KILA TATIZO LINA SULUHISHO LAKE hivyo mshukuru Allah kwa kila kitu katika maisha yako

Leo ninakumbushia kuelezea suluhisho la tatizo ambalo nilishawahi kulielezea miaka ya nyuma kidogo ambalo hadi sasa limekua likiendelea kusumbua vichwa vya wanawake wengi juu ya upatikanaji wa tiba sahihi


TATIZO LA HIRSUTISM NI NINI?


Ni tatizo ambalo huwatokea  wanawake kwa kupatwa na mabadiliko ya  kuotwa manyoya/vinyweleo sehemu ambazo kikawaida wanawake huwa hawaoti au hawapendezi kuwa na manyoya/vinyweleo maeneo hayo.

mfano wa maeneo hayo ambayo mwanamke hafai kuotwa na vinyweleo ni kupata manyoya kidevuni yani anaonekana kuwa na ndevu kama mwanaume,au kuotwa na manyoya kifuani, usoni, na mgongoni wakati mwingine manyoya magumu kama ya kiume miguuni na mikononi kitu ambacho sio cha kawaida kutokea kwa mwanamke

Kikawaida wingi wa manyoya mwilini mwa binadamu hutegemea sana vimelea vya ukoo husika, kitaalamu kama genetics lakini mwanamke anapokua na manyoya mengi sehemu ambazo haifai au haipendezi  kwa mwanamke kua vinyweleo mfano mwanamke kuwa na ndevu kuna mambo makuu mawili kwamba anaumwa au ukoo wake uko hivyo japokua waathirika wengi wa shida hii wengi ni wagonjwa wa matatizo ya homoni.

Kuna imaani nyingi zimejengeka juu ya mwanamke kuota ndevu na manyoya mwilini lakini sio katika uhalisia kuwa eti mwanamke akiotwa na ndevu ATAKUA TAJIRI NA MANENO MENGINE MENGI MENGI YASIYO NA UKWELI


CHANZO CHA TATIZO



Kawaida mwanamke akibaleghe huanza kutengeneza homoni za kiume na za kike ndio maana manyoya huota kwapani na maeneo ya uke lakini sasa inapotokea homoni za kiume zikiwa nyingi kitaalamu kama adrogens mwanamke hupata hali hii ya kuota manyoya sehemu ambazo hazihusiki kama nilivyotaja hapo juu
 lakini pamoja na hali hii ugonjwa huu una vyanzo vingine kama vifuatavyo.

POLYCYSTIC OVARY SYNDROME: 
huu ni ugonjwa unaowasumbua wanawake kwa kutokuwa na uwiano sawa wa homoni za kike ambapo kitaalamu tunasema mwanamke kuwa na tatizo  la homornal imbalance hivyo mwanamke hupata mzunguko wa damu ambao sio wa kawaida, kua mgumba,  kunenepa na kupata uvimbe kadhaa kwenye ovari za kutengeneza mayai yake na kupata shida mbalimbali za kuhusu uzazi

MATUMIZI YA DAWA NA VIPODOZI VYENYE KEMIKALI
Chanzo hiki huenda pia ndio kikawa chanzo kikuu cha wanawake wengi kuota ndevu na manyoya  kwa tabia ya kutumia dawa fulani bila maelekezo ya daktari pia siku hizi kuna maduka ya urembo yanauza dawa hizi na kuzigeuza dawa za urembo wakati ni hatari  sana kiafya kwa watumiaji.
kuna dawa kitaalamu zinaitwa steroids huingilia mfumo wa kiungo kinachohusika na utengenezaji wa homoni (Adrenal gland) hivyo zikitumika kwa muda mrefu huleta manyoya ambayo sio ya kawaida kwa wanawake
mfano wa dawa hizi za steroids ni PREDINISOLONE vidonge na cream, SONADERM, CANDIDERM, GENTALINE, na dawa zingine zote zenye mchanganyiko huu kwani zipo nyingi ila mchanganyiko ni uleule ila majina tofauti ya viwanda.
 Dawa hizi hutakiwa zitumike kwa angalau wiki moja tu kutibu ugonjwa wa ngozi lakini wengine wamezigeuza kama mafuta ya kujipaka hivyo kama na wewe unapaka hizo aina za dawa ujue Umejitengenezea mazingira hatarishi ya kuweza kupatwa na tatizo hili la kuotwa vinyweleo

UVIMBE WA KANSA
kansa za kiungo hichi kilichopo juu ya figo[adrenal gland] huongeza wingi wa homoni hizi kwenye mfumo wa binadamu na kuleta ndevu na manyoya magumu ya mwili.

CONGENITAL ADRENAL HYPERPLASIA:
huu ni ugonjwa wa tezi ya adrenal ambao mtu huzaliwa nao na kuanza kutoa homoni nyingi za uzazi na matokeo yake mtu huota ndevu na manyoya mengi mwilini..

CUSHING SYNDROME:
hali hii hutokea baada ya mgonjwa kupata matibabu ya dawa zenye homoni ya  cortisol mwilini mwake kwa muda mrefu. Mfano matumizi ya dawa ya prednisolone vidonge  kwa wagonjwa wa allergy na asthma.

Wakati mwingine ugonjwa huu hutokea bila sababu yeyote hasa kwa jamii za kiarabu na kihindi




DALILI ZA TATIZO


Kawaida mgonjwa wa hirsutism huwa na dalili za kua na manyoya mengi kama nilivyotaja hapo juu lakini pia mgonjwa huweza kua na sauti nzito kama mwanaume, kuota kipara, kinembe kua kikubwa, chunusi na kupungua ukubwa wa matiti


VIPIMO


Mgonjwa anashauriwa kufika hospital kuonana na daktari na kupata vipimo kuangalia wingi wa homoni mwilini wake hasa testosterone kama zitakua zipo juu Au kupiga picha ya ultrasound ya ovary kuangalia kama kuna tatizo lolote au kupima kuangalia uvimbe wa adrenal gland  mara nyingi ni moja ya vyanzo vikuu.


MATIBABU

Matibabu ya tatizo hili hujulikana mara baada ya kutafuta chanzo cha ugonjwa na ni moja ya matibabu bora zaidi kutibu kwa kudhibiti chanzo cha tatizo lakini pia pale ambapo  chanzo hakionekani dawa za uzazi wa mpango na zinginezo hutumika kutatua tatizo hilo kwa hisia ila jambo lenye ubora ni kujua chanzo cha tatizo
Baadhi ya dawa zingine ni zifuatazo ;

SPIRONOLACTONE
Dawa hizi hutumika kuzuia homoni za kusababisha manyoya lakini ukitumia dawa hizi lazima utumie uzazi wa mpango kwani zinasababisha madhara makubwa sana kwa mtoto ikitokea  ukibeba  mimba wakati unaendelea na dozi hiyo.

DAWA YA KUPAKA YA EFLORNIRITHINE;
 Dawa ya  Eflornithine  kitaalamu hutumika kupakwa maeneo yalioathirika na nywele nyingi kuzuia kasi ya kukua lakini hazitoi manyoya yaliyopo.

LASERS THERAPY
 hii ni miale ya mwanga ambayo inapita ndani ya ngozi kuzuia vyanzo vya ngozi{hair follicles} kuota tena mara nyingi hufanya kazi vizuri lakini gharama yake ni kubwa mno na huenda haipatikani kirahisi.

VEET CREAM :
 hii ni cream inayopatikana madukani kwa bei za kawaida ukipaka inanyoa manyoya yote japokua baada ya muda yataota tena lakini inasaidia sana hasa ukipaka mara mara kwa mara au mara moja au mbili kwa wiki.

 ELECTROLYSIS:
hii inahusisha kuweka sindano ndogo  maalumu kwa kila shimo la unywele na kuharibu chanzo chake ni moja ya matibabu mazuri ila ina maumivu makali sana na dawa za nganzi za kupakwa hutumika kupunguza maumivu hayo.

NOTED; kama wewe ni mwanamke una ndevu au manyoya ambayo sio ya kawaida na huenda mwanzoni hayakuepo angalia kwa makini vipodozi vyako huenda ndio vinasababisha lakini pia nenda hospitali ukachunguzwe wingi wa homoni na upigwe picha ya viungo vya uzazi kama viko salama. ushauri wa bure ni kwamba serikali imekua ikipiga marufuku baadhi ya vipodozi na kuvichoma moto lakini watu wanahisi wanaonewa na kuvitafuta kwa magendo, ukiona kitu kimepigwa marufuku acha kutumia kiepuke



HATUA ZA KUFATA KUTIBU NA KUDHIBITI KUENDELEA KWA TATIZO LA WANAWAKE KUOTWA NDEVU NA VINYWELEO

Kuna hatua kadhaa za kiasili ambazo zimethibitishwa kuonyesha matokeo baada ya watumiaji kuleta mrejesho wa matokeo mazuri
Hatua hizi zimegawanyika katika utaratibu mzuri ambapo ukizingatiwa na kutekelezwa ipasavyo inaleta matokeo mazuri na kudhibiti kuendelea kuota kwa ndevu na vinyweleo
Hatua za kufuata ili kudhibiti tatizo ni

1) BADILISHA MFUMO WAKO WA CHAKULA

Utafiti unaeleza waathirika wengi wanaopatwa na tatizo hili ni wale waliothirika na lishe mbovu ambao wanasumbuliwa na uzito mkubwa sana na uzito mdogo sana hali inayopelekea watu hao husumbuliwa na tatizo la homoni kutokua katika uwiano sawia PCOS.
kama yalivyo magonjwa mengine yanayohusiana na lishe bora hivyo hivyo ili mtu aweze kujitibia na kudhibiti kuendelea kuota ndevu na vinyweleo na chanzo cha tatizo lake ni kutokua na uwiano sawa wa homoni atatakiwa kubadilisha mfumo wake wa chakula ili kuweza kutatua matatizo hayo kwa kupungKup uzito mkubwa au kubalansi uzito wake kuwa katika uwiano wa usawa na umri wake

Hapa chini kuna vidokezo vichache vya lishe bora ili kupambana na tatizo hili

Unashauriwa kujitahidi kula mboga mboga za majani kwa wingi na vyakula vilivyomo katika kundi la PROTEINS kama vile nyama,kuku,samaki,mayai,karanga,korosho nk kila siku itasaidia kusawazisha sukari iliyopo katika damu na kuondoa sumu mbalimbali mwilini na hivyo kusaidia kurekebisha mfumo wa homoni

Epuka kabisa kula vyakula vilivyopo katika kundi la Carbohydrates kama vile ugali,wali,viazi,chips,chapati,maandazi,mihogo nk 

Pendelea kunywa maji na maziwa kwa wingi na Epukana na sukari sababu sukari ndio adui yetu namba moja katika kusababisha magonjwa mengi

 Ukizingatia hiyo lishe utapungua mwili wako ikiwa wewe ni mnene na itakusaidia kupambana na tatizo la PCOS na kudhibiti kuendelea kuota kwa ndevu na vinyweleo.


2)ONDOA NA EPUKANA NA MAWAZO AU MFADHAIKO

Huenda ukashangaa hili ukajiuliza  mawazo yanahusiana vipi na tatizo la kuota ndevu, lakini ukweli ni kwamba tezi zetu za adrenal hushughulika Sana kuzalisha homoni ya adrenal mtu anapopatwa na mfadhaiko pia. Tunapokuwa na mawazo sana kuhusu watoto, mambo ya kifedha au mahusiano na hata kitu kingine chochote, tunaunda homoni za mfadhaiko zaidi.
Homoni za mfadhaiko kama cortisol huathiri vibaya udhibiti wa sukari katika damu ambapo huathirika katika hali tofauti na mfadhaiko usio dhibitiwa huweza kusababisha kuongezeka kuzalishwa kwa  homoni za androjeni, haswa DHEAS.
Homoni za Adrojeni kama hizi zinaweza kubadilishwa kuwa DHT, fomu yenye nguvu zaidi ya homoni ya testosterone katika kiwango cha tishu ambayo huchochea chunusi, kuotwa na ndevu na vinyweleo na kupuputika kwa nywele kichwani

Mambo unayoweza kufanya kuondokana na mfadhaiko na mawazo

Fanya mazoezi ya yoga ya kila siku

Pendelea kutafakari na kutambua utukufu na ukubwa wa mwenyezimungu ambaye amekuumba wewe na viumbe vyote vilivyopo ulimwenguni.

Kunywa chai ya kutuliza mfadhaiko na mawazo kama lavender, chamomile, lemon, tulsi nk
Changanyikana na marafiki zako epuka kujitenga
Shiriki tendo la ndoa mara kwa mara ikiwa tayari umeolewa
Pendelea kula vyakula vyenye Omega 3 na vitamins nyingi

3)EPUKA KUJIDHURU NA KEMIKALI TUMIA VITU VYA ASILI KUDHIBITI VINYWELEO

Badala ya kuhangaika kutafuta dawa zenye kemikali  kuondoa ndevu au vinyweleo usoni
Faham tiba rahisi na nzuri za nyumbani zinazoweza kukusaidia kuondoa vinyweleo usoni

1)PAPAI NA MANJANO


Tengeneza mchanganyiko wa papai na manjano ili kudhibiti kuendelea kuota kwa ndevu na vinyweleo mwilini
Chukua bakuli andaa vipande vinne vya papai,vijiko viwili vya unga wa manjano(tumeric powder) vichanganye vizuri upate uji mzito wa mchanganyiko huo kisha jipake mahali palipoota vinyweleo visivyohitajika
Acha kwa dakika 20 hadi ukauke na kubakia mkavu kisha jibandue kwa kusugua ili kuzuia kuota kwa vinyweleo tena
Kupata matokeo mazuri fanya hili zoezi kwa week mara 3

2)LIMAO NA ASALI

Kamua juisi ya limao changanya na asali  vijiko viwili koroga hadi upate uji mzito kisha paka sehemu iliyoota vinyweleo na kaa kwa dakika 15_20 ujibandue kwa kusugua ili kuondoa nywele zilizopo na kudhibiti kuendelea kuota vinywele
Kupata matokeo mazuri fanya hili zoezi kila siku kabla hujaingia kulala

3) KITUNGUU THAUMU NA CHUMVI

Chukua punje kumi za kitunguu thaumu ziponde pamoja na kitunguu thaumu kisha jisugulie mahali penye vinyweleo na kaa kwa dakika 15 kisha nawa na maji safi na jikaushe kwa kitambaa
Kitunguu thaumu kinasaidia kuzuia kuendelea kuota kwa vinyweleo na kufanya ndevu na vinyweleo kupotea
Kupata matokeo mazuri fanya zoezi hili kila siku

4)MSHUBIRI (ALOE VERA) NA PAPAI

 Chukua vipande vinne vya papai liloiva kisha changanya na ute ute wa mshubiri (aloe vera)
Visage hadi upate uji mzito kisha paka sehemu iliyoota vinyweleo na sugua taratibu ili kuzuia kuendelea kuota vinyweleo hivyo kisha kaa kwa dakika 15 nawa na maji safi kisha jifute kwa taulo safi
Kupata matokeo mazuri fanya zoezi hili kila siku kabla hujaingia kulala

Mpendwa msomaji hizo hapo juu ni baadhi ya njia unazoweza kutumia kujitibia au kudhibiti kuendelea kuota ndevu na vinyweleo mwilini

Noted;

Matibabu ya tatizo hili huchukua muda mrefu kidogo takriban miezi 3 hadi miezi 6 kulingana na vyanzo vya tatizo hili kutofautiana uzito katika matibabu


MATIBABU YA TATIZO HILI LA HIRSUTISM NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER


Mpendwa msomaji Kama una tatizo hili au ndugu yako ana hili tatizo la hirsutism na magonjwa mengine mbalimbali na umejaribu njia kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)


Green health consultation center tutakufanyia uchunguzi kujua chanzo cha tatizo kisha tutakupatia dawa za kuondoa hirsutism na tutakupatia ushauri sahihi wa kupambana na ugonjwa huo na magonjwa yote yanayokusumbua karibu sana ofisini kwetu tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud ) 

TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KULA KWA KUHOFIA KUNENEPA (ANEROXIA NERVOSA)





Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, Ni matumaini yetu unaendelea vyema mpendwa msomaji wetu,
Tunakuombea afya njema zaidi wewe pamoja na familia yako na wote unaowapenda
MWENYEZIMUNGU MTUKUFU AZIDI KUWAHIFADHI NA KUWAJAALIA REHMA ZAKE 
AMEEN!

Naam leo nimeona ni khery tukaongelea juu ya mada hapo juu kutokana na athari tunayoiona katika jamii zetu kwa watu wengi kuathirika kisaikolojia kwa kukosa hamu ya kula kwa kujinyima kwao kula kwa hoja ya kuhitaji kuwa wembamba zaidi kwa kujiona kua wao ni WANENE WENYE UZITO MKUBWA Jambo ambalo sio la kweli isipokua fikra zao ndio zenye kuwatuma kujiona hivyo.



Je, TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KULA KWA KUHOFIA KUNENEPA (ANEROXIA NERVOSA) NI TATIZO GANI?

Hili ni tatizo la kukosa kabisa hamu ya kula na kumfanya mtu apungue sana uzito kutokana na kuathirika kisaikolojia kwa dhana ya kuogopa kula kwa kuhofia kunenepa au kuongezeka uzito na kujihisi au kujiona kuwa yeye ni MNENE wakati kiuhalisia ni mwembamba.
Watu wanaopata zaidi tatizo hili ni wale waliokusudia hasa kwa dhati kujinyima kula ili wapungue uzito na mwili kuwa mwembamba hivyo hujinyima kula kwa kiasi kikubwa kwa kujihisi kuwa wana uzito au miili mikubwa au kujihisi wanene
Hali ambayo huwapelekea kujibiidiisha au kuhangaika kwa kila njia kwa kujinyima kula na kunywa,kutumia dawa za Kupunguza mwili na hamu ya kula,kwa kujitapikisha baada ya kula,kufanya mazoezi makali ili mradi tu wapungue mwili bila ya kujali au kutambua ni kiasi gani cha uzito alionao yeye bado huhofu kuhusu uzito wake

Tatizo hili la kujihisi unene ni tatizo la kuathirika kisaikolojia zaidi kwani tunaposema fulani ni mnene lazima upime “BMI” ambayo ni uwiano wa uzito na urefu.
Hivyo ni vema ukajifahamu ‘BMI’ yako ikoje kabla ya kuanza kupanga utaratibu wa kupunguza uzito.


Ifahamike kuwa Uzito mkubwa kupita uwezo wa mwili wako ni tatizo, na uzito mdogo kuliko mwili wako unavyostahili pia ni tatizo hasa katika mfumo wako mwilini na taswira yako kwa nje kimuonekano (appearance)



Chanzo Cha tatizo



Chanzo Cha tatizo hili hasa hakijajulikana kama yalivyo magonjwa mengine.
Isipokua tafiti zimeonyesha kua Kupoteza hamu ya kula kunasababishwa na mambo mbalimbali, mojawapo ni kutokana na muendelezo wa kuzoea kujinyima chakula, t,atizo la kiugonjwa na inaweza kuwa hali ya kurithi.
Lakini pia chanzo halisi mbali ya hilo la kukusudia kujinyima bado hakijulikani rasmi lakini inaweza kuwa matatizo ya kimwili, matatizo ya kisaikolojia na matatizo ya kijamii kutegemea na aina ya vyakula vinavyopatikana katika jamii husika.

Katika tatizo la kimwili ambapo kitaalam tunasema ‘Physiological’ hali ya kuvurugukika kwa mfumo wa kichocheo cha ‘Serotonin’ huchangia tatizo hili kwa kiasi kikubwa

Tatizo hili pia hurithiwa endapo katika familia kuna watu wa aina hiyo wasiopenda kula.

Wanawake wajawazito huweza kuathirika na tatizo hili la kupoteza hamu ya kula kutokana na hali ya ujauzito na kusababisha apate tatizo la upungufu wa damu, kisukari, kifafa cha mimba, matatizo katika kondo la nyuma na matatizo kwa mtoto aliye tumboni na hata mtoto akishazaliwa.

Wengine wanaopatwa na tatizo hili ni wagonjwa hasa wale wenye homa kama malaria au wenye matatizo katika mfumo wa chakula. Watu wenye magonjwa sugu au wanaotumia dawa kwa muda mrefu pia hupatwa na tatizo hili.

DALILI ZITAKAZOKUJULISHA KUWA UNA TATIZO HILI


Dalili zitakazokujulisha kama una tatizo hili ni Mtu hupoteza hamu ya kula, wengine kupoteza hamu ya kula hata kwa kutumia dawa ili kupunguza mwili au kujipunguza uzito hali kuwa wala yeye si mnene au mwenye kuhitajika Kupunguza uzito
 Mtu anapojinyima kula lengo ni kujikondesha na kujikondesha pasipo kufuata maelekezo ya kitaalamu kuna madhara kiafya kama tutakavyokuja kuyabainisha huko mbele

Mtu anayejikondesha anaweza kuwa na dalili za utapia mlo kama vile ngozi kuzeeka na kunyauka, mifupa ya usoni, mabega kujitokeza na mbavu kuhesabika kirahisi, kuchoka mara kwa mara na mwili kukosa nguvu, misuli kukaza na baadhi ya viungo vya mwili kuathirika mfano ubongo, moyo na figo hata ini.

Tatizo hili la kujikondesha kwa makusudi au kutokana na maradhi humfanya mtu apate tatizo la kiafya liitwalo ‘Hypokalaemia’  na madini ya ‘potassium’ mwilini hupungua, hivyo hulalamika mapigo ya moyo kutokwenda vizuri, kufunga kupata choo kikubwa, uchovu wa mwili na wakati mwingine mwili kupooza.

Dalili nyingine ni kupoteza kabisa hamu ya kula, kufunga kupata hedhi, nywele kichwani kuwa nyepesi, shinikizo la damu hushuka na kuhisi moyo kwenda mbio wakati wa kuongea au kutembea, kuwa na msongo wa mawazo, tumbo kujaa gesi na kutoa harufu mbaya ya mwili, ngozi huwa kavu na ngumu.


UCHUNGUZI WA VIPIMO


Vipimo vya uchunguzi wa tatizo hili hufanywa pale daktari wako anapohisi kwamba una tatizo la anorexia nervosa, kwa kawaida atafanya majaribio kadhaa na uchunguzii kusaidia kubaini tatizo,ili atoe sababu za matibabu kwa kupoteza uzito, na huangalia shida zozote zinazohusiana kwa kufuata hatua zifuatazo za kiuchunguzi

Uchunguzi wa Kimwili.
Hii inaweza kujumuisha kupima urefu na uzito wa mgonjwa na kuangalia ishara zote muhimu, kama kiwango cha moyo, shinikizo la damu na joto; kuangalia rangi ya ngozi na kucha,kusikiliza mapigo ya moyo  na mapafu na kuchunguza tumbo lako.

Vipimo vya maabara.
Hatua hii inaweza kujumuisha kufatilia hesabu kamili ya damu (CBC) na vipimo maalum vya damu ili kuona wingi wa damu na protini na utendaji wa ini yako, figo na tezi.


Tathmini ya kisaikolojia.
Daktari au mtaalamu wa afya ya akili atauliza juu ya mawazo yako, hisia na tabia ya kula kwako. Unaweza pia kuulizwa kukamilisha maswali ya uchunguzi wa kisaikolojia ya kujitathmini.

Vipimo vingine.
Kipimo cha X ray kinaweza kuchukuliwa ili kuona uwiano wa mifupa yako, kuangalia kupunguka kwa mfadhaiko au mifupa iliyovunjika, au kuangalia shida ya pneumonia au ya moyo.


MATIBABU


Matibabu ya anorexia kwa ujumla hufanywa kwa kutumia mbinu ya timu, ambayo ni pamoja na madaktari, wataalamu wa afya ya akili na wale wa lishe, wote wenye uzoefu wa shida za kula. Kuendelea na matibabu na lishe ni muhimu sana kwa kuendelea kupona.

Kuna hatua nyingi za kufuata ili kuweza kupata tiba sahihi ya tatizo la aneroxia nervosa

1)Mipango ya hospital

Ikiwa maisha ya mgonjwa  yako katika hatari ya haraka, unaweza kuhitaji matibabu katika chumba cha dharura cha hospitali kwa maswala kama moyo kuvurugika, upungufu wa damu, ukosefu wa usawa wa umeme au dharura ya akili.
Kulazwa hospitalini kunaweza kuhitajika kwa shida za kimatibabu, shida kali za akili, utapiamlo mzito au kuendelea kukataa kula.

Kliniki zingine huratibu Mipango katika kutibu watu wenye shida ya kula. Wanaweza kutoa mipango ya siku au mipango ya makazi badala ya kulazwa hospitalini kamili. Programu maalum za shida ya kula zinaweza kutoa matibabu zaidi kwa muda mrefu zaidi.


2)Huduma ya matibabu

Kutokana na athari za tatizo la anorexia, mgonjwa anaweza kuhitaji ufuatiliaji wa mara kwa mara ili kutizama kiwango cha upumuaji, pamoja na mabadiliko mengine ya mwili. Katika hali mbaya, watu walio na anorexia hapo awali wanaweza kuhitaji kulishwa kupitia bomba ambalo limewekwa kwenye pua zao na huenda kwenye tumbo


3)Kurejesha uzito wenye afya

Lengo la kwanza la matibabu ni kurudi kwenye uzito wenye afya. Hauwezi kupona mwenye tatizo la aneroxia nervosa bila kurudi kwenye uzani mzuri na kujifunza lishe sahihi. Wale wanaohusika katika mchakato huu wanaweza kujumuisha:

Daktari wako wa huduma ya msingi, anayeweza kutoa huduma ya matibabu na kusimamia mahitaji yako ya kalori na kupata uzito

Mtaalam wa saikolojia au mtaalamu mwingine wa afya ya akili, anayeweza kufanya kazi na wewe kuunda mikakati ya tabia kukusaidia kurudi kwenye uzito wenye afya

Mtaalam wa chakula, anayeweza kutoa mwongozo wa kurudi kwenye hali ya kawaida ya kula, pamoja na kutoa mipango maalum ya chakula na mahitaji ya kalori ambayo hukusaidia kufikia malengo yako ya uzani

Familia yako, ambayo itahusika katika kukusaidia kudumisha tabia ya kawaida ya kula

4)Ushauri na tiba ya kisaikolojia

Aina hii za tiba za tiba zinaweza kuwa na faida kwa anorexia:

Tiba inayotegemea familia. Hii ndio matibabu ya msingi kwa ushahidi kwa vijana wenye anorexia. Kwa sababu kijana mwenye anorexia haiwezi kufanya maamuzi mazuri juu ya kula na afya wakati yuko katika hali hii mbaya, matibabu haya huwahamasisha wazazi kumsaidia mtoto wao kwa kulisha tena na kurejesha uzito hadi mtoto aweze kufanya uchaguzi mzuri juu ya afya.

Tiba ya mtu binafsi. Kwa watu wazima, tiba ya tabia ya utambuzi - tiba ya tabia ya utambuzi iliyoimarishwa - imeonyeshwa kusaidia. Lengo kuu ni kurekebisha mitindo ya tabia ya kula na tabia ili kuunga mkono kupata uzito. Lengo la pili ni kusaidia kubadili imani na mawazo yaliyopotoka ambayo yanadorora kula chakula

5)Dawa

Hospital hakuna dawa ya Moja kwa moja iliyopitishwa kutibu anorexia kwa sababu hakuna iliyopatikana kufanya kazi vizuri. Walakini, antidepressants au dawa zingine za akili zinaweza kusaidia kutibu shida zingine za afya ya akili ambazo unaweza kuwa nazo, kama unyogovu au wasiwasi na kukosa usingizi.

Madhara 


Tatizo la kukosa hamu ya kula kama tulivyoona mtu hukonda na unapofikia hali hiyo unaharibu mifumo mbalimbali ya mwili na hukufanya uwe mgonjwa. Mfumo ambao huathirika zaidi na kuonesha dalili za wazi ni mfumo wa uzazi kwa mwanaume na mwanamke.

Mwanaume hupoteza uwezo wa kufanya tendo la ndoa kutokana na matatizo mbalimbali ya mfumo wa mwili yanayotokana na upungufu wa lishe bora.

Mwanamke hupoteza hedhi, hupoteza uwezo wa kuzaa na hamu ya tendo la ndoa na hata wakati wa tendo.

Uwezo wa kuzaa unapotea ndipo tunaposema ugumba, hapa vichocheo au homoni za uzazi huvurugika na kupungua kwa kiasi kikubwa.

Madhara mengine ya anorexia ni pamoja na:

Mtu kupata ugonjwa wa Anemia

Matatizo ya moyo, kama prolapse of mitral valve, mitindo ya moyo isiyo ya kawaida au kufeli kwa mishipa ya moyo

Kupotea kwa mfupa (osteoporosis), na kuongeza hatari ya kupunguka mifupa

Kupoteza misuli

Kukosa usingizi na kupata mfadhaiko

Vidonda vya tumbo, kusumbuliwa na hali za kukera Kama kuvimbiwa kutokwa na damu au kichefuchefu

Kupungua kwa potasiam chini ya damu, sodiamu na kloridi

Matatizo ya figo


Noted

Epuka kujipunguza uzito bila ya kuwa na elimu fuata ushauri wa daktari kama unahisi uzito wako ni mkubwa na unataka kupungua ili kuepuka matatizo.

Mwanamke au mwanaume aliye katika mpango wa kuzaa inampasa azingatie kanuni bora katika uzito unaostahili ili aweze kupata mimba haraka au aweze kumpa mwanamke ujauzito katika kipindi muafaka.

Uzito mkubwa kupita uwezo wa mwili wako ni tatizo, na uzito mdogo kuliko mwili wako unavyostahili pia ni tatizo hasa katika mfumo wako wa uzuri

Je,unawezaje KUJIKINGA na tatizo la anorexia nervosa?


Huenda ukawa na shauku ya kujua jinsi unavyoweza kujikinga dhidi ya tatizo hili ambalo lina madhara makubwa lakin kwa bahati mbaya hakuna njia iliyohakikishwa ya kuzuia tatizo hili la anorexia nervosa. Madaktari wa utunzaji wa kimsingi (watoto, waganga wa familia na wafizi wa masomo ya ndani) wanaweza kuwa katika nafasi nzuri ya kutambua viashiria vya mapema vya anorexia na kuzuia ukuaji wa ugonjwa uliopigwa kabisa. Kwa mfano, wanaweza kuuliza maswali juu ya tabia ya kula na kuridhika na kuonekana wakati wa miadi ya matibabu ya kawaida.

NOTED;

IWAPO utagundua kuwa mtu wa familia au rafiki yako ana tabia ya kutopenda kula na kuhofia kunenepa licha ya kuwa ni mwembamba ila anajiona ni mnene Fikiria kuzungumza naye kuhusu maswala haya na msaidie juu ya kupata matibabu



MATIBABU YA TATIZO LA ANEROXIA NERVOSA NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo hili au ndugu yako ana hili tatizo la ANEROXIA NERVOSA na magonjwa mengine mbalimbali na umejaribu njia kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tutakupatia dawa za kuondoa tatizo la anorexia nervosa na tutakupatia ushauri sahihi wa kupambana na ugonjwa huo na magonjwa yote yanayokusumbua karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako

Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )



TATIZO LA TINDIKALI TUMBO KURUDI KWENYE KOO LA CHAKULA(GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASE) NA KIUNGULIA (HEARTBURN)


Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul
Ni matumaini yangu unaendelea vyema mpendwa msomaji wa makala hii
Kwa upande wangu namshukuru Allah kwa kunijaalia uzima na nafasi ya kuwajibika katika majukumu yangu
Kutokana na harakati na shughuli kuwa nyingi leo nimepata nafasi ya kuandaa somo hili ambalo watu wengi wamenitumia email na meseji kwa ajili ya kupata suluhisho la kudumu
Ila kabla ya kutoa suluhisho nimeona kuna haja ya kupata elimu ya matatizo haya na jinsi ya kujiepusha na kupata Matibabu.

Je, TATIZO LA TINDIKALI TUMBO KURUDI KWENYE KOO(GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASE) ni tatizo gani?


Hili ni tatizo linalotokea katika mfumo wa mmeng'enyo ambapo hutokea hitilafu ya chakula au maji kurudi katika koo la chakula(umio)mara baada ya kuwa chakula Hiko kimeshamezwa.
Au
Ni kitendo cha kupanda kwa acids (tindikali) ya tumbo hadi kwenye umio la chakula kwa muda mrefu na matokeo yake husababisha kiungulia(HEARTBURN)

Ili kuelewa vizuri tatizo hili linavyotokea tunatakiwa kujua vizuri jinsi chakula kinavyofika tumboni.
Kawaida Mara baada ya mtu kutafuna chakula au kunywa maji,chakula husafirishwa kupitia mrija wa chakula (Esophagus) hadi tumboni lakini juu kidogo kati ya tumbo na mrija huu wa chakula kuna kizuizi kilicho na sura ya bangili ( lower esophageal spincher )
kibangili hiki hufanya kazi ya kuzuia chakula kisurudi mdomoni au kwenye koo baada ya kuwa kimeshamezwa pia kibangiri hiki ndicho kinacho mfanya mtu aweze kula chakula huku amening'iniza kichwa chini miguu juu na chakula kisirudi tumboni.
 baada ya chakula kuingia tumboni huchanganyikana na vimeng'enya pamoja na tindikali ambayo hufanya kazi ya kuua vimelea vyote vilivyoingia tumboni pamoja  na chakula
mchanganyiko huu husababisha chakula kupata chachu(acids) ambayo matokeo yake huwa ni rahisi sana kuweza kurudi katika koo la chakula endapo kizuizi cha juu ya tumbo kitakua kimepata hitilafu au maambukizi.


Je, Kiungulia (HEARTBURN)NI NINI?


Ni hali ya kukera inayoweza kumtokea mtu yoyote na husababisha maumivu makali kwenye kifua na upande wa juu wa tumbo. 
Hali hii inaendana kwa ukaribu wa kupanda kwa tindikali(acid reflux). 
Lakini pia Kuna utofauti kati ya acid reflux na heartburn.
Kama nilivyoeleza hapo juu kuwa acid reflux ni kitendo cha kupanda kwa tindikali kutoka tumboni kurudi juu kwenye umio la chakula na kusababisha maumivu ya kifua ambayo tunaita ni kiungulia (Heartburn)
Kwahiyo acid reflux ndio inayoweza kusababisha Kiungulia (HEARTBURN)
Hali ya kiungulia ni kitendo cha kawaiada kutokea kwa watu wengi na inatokea kwa kila mtu, lakini kama tu haiambatani na maumivu makali ya kifua, kama maumivu yakizidi kuwa makali na yanatokea mara kwa mara hapo ndipo tatizo huanza. Kama tatizo likiendelea zaidi basi hufikia hatua ya tatu na kuitwa gastroesophageal reflux disease(GERD), kwa hiyo kadiri kiungulia kinachukua muda mrefu mpaka kuathiri tishu za umio GERD ni hatari zaidi kwasababu inaweza kupelekea uwezekano wa kupata Saratani ya Koo 

CHANZO CHA MATATIZO


Uchunguzi unaonyesha kuna sababu nyingi zinazoweza kuambatanishwa na matatizo haya ambayo ni;

1. Kudhohofika kwa utendaji kazi wa kizuizi cha juu ya tumbo ( Lower esophageal sphincter)

kudhohofika kwa kizuizi hiki husababishwa na utumiaji wa madawa kama nitrates,bisphosphonates,estrogen,oral contraceptives,progesterone,alpha adrenergic agents,theophyline,calcium channel blockers,benzodiazepines,anticholinergics, na tricyclic antidepressants nk baadhi ya dawa zimeonekana kuharibu sana utendaji kazi wa kizuizi hiki.

2.Mfumo dhaifu wa mmeng'enyo wa chakula
Mfumo wa mmeng'enyo huwa dhaifu kutokana na lishe kuwa mbovu
watu wanaokula zaidi vyakula vilivyosindikwa, sukari, chocolate, vyakula vyenye caffeine kama kahawa wapo kweye hatari zaidi ya kupata matatizo haya

3.Tindikali ( Hydrochloric acid) kuzidi tumboni.

4.Upungufu wa madini kama Magnesium na Potassium

5.Uzito mkubwa na kitambi na msongo wa mawazo kupita kiasi ni chanzo cha kupata matatizo haya.

6.Wamama wajawazito na wazee wenye umri mkubwa wako kwenye hatari zaidi ya kupata matatizo haya

7.Wenye historia ya kuwa na ugonjwa wa hernia(ngiri) pia wapo katika hatari zaidi ya kupata matatizo haya

DALILI ZA KUKUJULISHA UNA TATIZO LA GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASE


Dalili kuu ya matatizo haya ni kupatwa na kiungulia mara kwa mara ambapo huambatana na koo la chakula kuwaka moto pia maumivu ya kifua na hali hii huzidi zaidi pale mtu anapolala kichwa kimeinama.
Kiungulia hiki huanza baada ya lisaa limoja na kuisha baada ya masaa mawili baada ya kula.
Pia dalili za tatizo hili kwa watoto hujionesha pale mtoto anapotapika kupita kiasi au kupaliwa mara kwa mara wakati wa kula chakula
Dalili zingine ni kama;
Tumbo kuunguruma na
Kukosa hamu ya kula chakula na kuhisi kichefuchefu.
Mdomo kunuka kutokana na kurudi juu kwa chakula cha tumboni chenye tindikali
Kupata hali ya kuunguza kwenye kifua karibu na moyo, hali inayotokea baada tu ya kula na kupata shida wakati wa kumeza chakula
Kukohoa au kupaliwa mara kwa mara ikiambatana na kuweweseka.
Mdomo kuwa mchachu muda mwingi
Kupata usingizi kwa shida kutokana na maumivu
Mdomo kukauka
Meno kupoteza uimara na kuanza kumomonyoka kutokana na uwepo wa tindikali.
Tumbo kujaa na kujamba sana baada ya kula


UCHUNGUZI NA VIPIMO

Uchunguzi wa matatizo haya hufanyika kwa njia kipimo cha  x-ray,ambapo mgonjwa hupewa kimiminika maalumu ambacho hukimeza ili kuonesha utendaji kazi wa mfumo wa chakula pindi atakapofanyiwa x-ray
lakini iwapo tatizo linapokua kubwa zaidi kipimo aina ya Endoscopy hutumika,hiki ni kimrija chenye kamera ni kadogo sana huingizwa kupitia koo la chakula hadi tumboni kisha kuonesha kwenye screen jinsi mfumo ulivyo.

MATIBABU 

Mara nyingi baada ya vipimo na uchunguzi kufanyika
Ushauri wa lishe na dawa za antiacids hutolewa juu ya kupambana na magonjwa haya pia ukubwa wa tatizo hupelekea watu kufanyiwa upasuaji baada ya kutumia dawa  za kupunguza tindikali ( antacid) na zingine kama cholinergic agenys,Hestimamine H2 Antagonists,Prokinetic Agents na proton Pump Inhibitors.

Lakini pia wapo baadhi ya wagonjwa kadiri wanavyoendelea kutumia dawa hizi huongeza magonjwa mengine ya mfumo wa chakula na kuharibu bacteria wazuri walioko tumboni, matumizi ya dawa za antiacid  zinaweza kusababisha kukosa choo ama kupata choo kwa shida, kuharisha, matatizo kwenye figo na kushuka kwa kinga ya mwili

MAMBO YA kUFANYA KUJITIBU KIUNGULIA CHA MARA KWA MARA UKIWA NYUMBANI ILI KUJIEPUSHA NA TATIZO LA GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASES


Mpendwa msomaji kama unavyofahamu kinga ni bora kuliko matibabu hivyo napenda kukushauri Kama unasumbuliwa na kiungulia cha mara kwa mara sio ishara nzuri hivyo unaweza kufanya yafuatayo ili kujitibia na kukomesha hiyo Hali  kusudi tatizo lisije kuwa kubwa zaidi
 Badilisha mfumo wako wa chakula jitahidi kuepuka vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
Punguza au jiepushe kuwa na uzito mkubwa
Epuka aina ya vyakula vyote unavyohisi vinaweza kuchangia kukupa Kiungulia
Sitisha unywaji wa vinywaji vyenye caffein vyote.
Kula kwa mpangilio ili chakula kiweze kumeng'enywa taratibu tumboni,sio kila wakati unakula tena kwa kuchanganya changanya.
Acha sigara na pombe.
Punguza msongo wa mawazo
Lala masaa matatu mpaka manne baada ya kula.
Hakikisha unalala kichwa chako kiwe juu,yaani weka mto kichwa pindi unapolala.

Pia wakati unayafanya yote hayo hapo juu tumia baadhi ya vyakula kujitibu kiungulia

 TANGAWIZI(GINGER)


Tangawizi ina vitamin A, C, E, B complex, chuma,zinki, magnesium, phosphorus, sodium, calcium, na beta carotene hivyo hutumika kutibu tatizo la gesi na acids kuwa nyingi 
Chemsha kikombe kimoja cha maji ya tangawizi kunywa kila siku asubuh kabla ya kula kitu na usiku lisaa limoja kabla ya kwenda kulala kwa muda wa siku 14 au zaidi


JUISI YA MSHUBIRI (ALOEVERA JUICE)


Mshubiri ni tiba nzuri sana kwa matatizo ya tumbo
Kama utainywa, hutibu vidonda vya tumbo na kiungulia, na kwa ujumla ni kuwa husafisha mfumo wote wa mmeng’enyo wa chakula. Chukua jeli ya aloe vera nusu kikombe (ml 125) changanya na maji ya kawaida nusu kikombe tena kupata ujazo wa  robo lita, changanya vizuri mchanganyiko huu na unywe kutwa mara 2 kwa siku 3 hadi wiki 1 kujitibu matatizo ya Kiungulia,tumbo kuuma, kuondoa sumu, kuunguruma, kuhara na hata kutibu malaria.

KITUNGUU THAUMU NA ASALI (GARLIC AND HONEY)


Kitunguu swaumu ni miongoni mwa tiba za asili kwa miaka mingi hasa katika maswala ya kuua fungals hutoa majibu haraka sana kwa upande wa Kiungulia
Chukua punje 3 hadi 4, menya na ukate vipande vidogo vidogo lakini siyo vidogo sana na uchemshe kwenye moto na maji kikombe kimoja (robo lita), ongeza kijiko kikubwa kimoja chaasali mbichi ndani yake na uache kwenye moto kama dakika 5. Ipua na unywe kwa pamoja kutwa mara 2 hadi utakapopona Kiungulia lakini pia utakua umejitibu baadhi ya maradhi mengine mwilini mwako

SIKI YA TUFAHA (APPLE CIDER VINEGAR)

Imeonekana kuwa ni msaada miongoni mwa maradhi mengi ya mfumo wa mmeng'enyo hivyo inashauriwa kunywa walau vijiko viwili kwa siku

MATIBABU YA TATIZO LA GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASES NA MAGONJWA MBALIMBALI CHINI YA UONGOZI WA GREEN HEALTH CONSULTATION CENTER

Mpendwa msomaji Kama una tatizo hili la GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASES na magonjwa mengine mbalimbali na umejaribu njia kadhaa kupata tiba bila kupata mafanikio ya kukuridhisha,tunakukaribisha ofisini kwetu ilala,Dar es salaam pia unaweza kutuandikia Ujumbe wa Meseji katika Namba na email zetu  ili upate maelezo na ushauri zaidi (+255746465095/+255657041420)
(nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com)
Green health consultation center tutakupatia dawa za kuondoa tatizo la GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASES na tutakupatia ushauri sahihi wa kupambana na magonjwa yote yanayokusumbua karibu sana tuweze kukuponya tatizo lako


NOTED;

Kutopata matibabu mapema ni hatari kwa afya yako kwa vile huweza kusababisha magonjwa makubwa zaidi kama vile;
Uvimbe joto sehemu za koo la chakula ambapo uvimbe huu huharibu koo la chakula kwa vile huweza kusababisha vidonda na koo kupoteza uwezo wa kufanya kazi.
Kutengenezwa kwa kovu katika koo la chakula ambako kunapelekea koo la chakula kupoteza uwezo wa kufanya kazi.
Kubadilika kwa seli za koo la chakula kunakopelekea koo la chakula kupoteza asili yake ambapo tatizo hili kitaalamu huitwa Barrett's esophagus na mwishowe ukapata saratani ya Koo na magonjwa ya Moyo
Tunawaombea wahanga wa ugonjwa huu wapate Matibabu mapema na waepukane na maradhi makubwa zaidi
AMEEN.


Mpendwa msomaji nina imaani umejifunza katika makala yangu hii ninashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zetu za afya tunasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI TUANDIKIE UJUMBE  KUPITIA EMAIL AU NAMBA ZETU HAPO CHINI
KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 GREENHEALTHC.BLOGSPOT.COM

 Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na uongozi wa green health consultation center
E-mail nsalum998@gmail.com/nmasoud998@gmail.com
+255746465095/+255657041420(Dr Naytham S Masoud )

Copyright © 2017 Green health consultation centre